Tuambie interview mbaya uliyowahi kuifanya

Tuambie interview mbaya uliyowahi kuifanya

Mwanakulipata

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2018
Posts
718
Reaction score
1,202
Habari wana JF, katika harakati za kutafuta ajira unaweza kupata nafasi ya kufanya interview kwa ajili ya ajira, share nasi interview ambayo hutokaa huisahau katika maisha yako

Mimi yangu ilikuwa hivi, baada ya kumaliza elimu ya sekondari na kutofanikiwa kuendelea na masomo kwa muda nikaamua nijikite kutafuta ajira, nilifanikiwa kufanya interview 2 ambazo sitokaa nizisahau

Ya kwanza ilikuwa tigo customers service wenyewe wanaita PCCI, nilikuwa na wenge sijawahi kufanya hizo mambo niliwahi mapema kabisa nilivyofika kwenye kile chumba nikakutana na wale wanaohoji wa 3 nikasema hapa nikichomoka sijui, nikaulizwa kwanini unaitaka hii kazi nikajibu kwa kuzunguka weee mara maisha ya mtaani magumu mara sina hela walibaki wanacheka tu na ndo ikawa tamati yangu

Ya pili kuna bro alikuwa Engineer alinifanyia mpango kwenye kampuni flani hivi ya ujenzi walikuwa wanataka Storekeeper, nikajua nitakuwa pekee yangu kufika nakuta tupo 2 mimi na mdada kuna jamaa mfanyakazi akasema tulitegemea aje mmoja lakini kama mpo wawili sio mbaya tutafanya ka interview kadogo, akaanza yule mdada baadae nikafata mimi baada ya mahojiano madogo nikatoka nikaambiwa nisubirie nje then akatoka akanambia kusema ukweli mdogo wangu interview umefaulu lakini wewe bado mdogo sana muachie yule dada hii kazi anamajukumu nikamwambia bro mimi mwenyew naitaka hii kazi akaondoka nilichukia nikamfikishia ujumbe yule bro aliyenipa mchongo akasema huyo jamaa anapenda sana wanawake huenda aliona ampe yule dada kwa kusudi flani.

Wewe yako unayoikumbuka ilikuaje?
 
Yangu nilifanya na watu wanaitwa Wezesha wazawa microfinance, Hawa jamaa walipigia simu kazi ambayo nishaomba miezi nane ishapita,,, Wakasema Njoo kwa ajiri ya interview ,nafika pale ofisin pao nawaambia niliitwa kwa ajili ya interview wanabaki wananishangaa tuu, Kumbe aliyebipigia simu hata hakutoa taarifa kwa wenzake.

Nilikaa pale Kama saa moja hivi ,nikawafata nikawambia Kama hamna interview naombeni mnirudishie gharama zangu za usumbufu, niliwapelekesha hawatakuja sahau , baadaye Wakasema tutafanya mida ya saa nane nikawambia sawa,, nikatoka pale nikaenda kunywa k- vant na safari mbili, mda ulivyofika wa saa nane maana nilikuwa Niko peke yangu tunafika kwenye interview room nikawaambia mie nahitaji hela zangu na mda niliyopoteza.

😂😂😂Nilivyokuwa nimechange walitoa nauli wajinga wale.
 
Bana we mi kama mbili tatu hivi nilimbwela yani na uhakika hadi nilivyogeuza shingo, walibaki kusema huyu dogo hayuko makini na maisha.

Nayo kumbuka vizuri ni International Organization for Migration (IOM) ni kama watu wa UN vile. Walikuwa wanataka mtu yani kamaliza tu school hana hata miezi 12 toka amalize shule. Wakanipata.

Picha linaanza sikuona mail yao iliyotaka kuconfirm kama ntakuepo kwenye interview au nko mbali wafanye utaratibu mwingine. Siku ya interview kama siku 7 baada ya email yao, wananipigia DanbyHR hujaconfirm kama utakuepo kwenye interview, vipi utakuja au tukufanyie phone/Skype interview? Nkafikiria nkaona sielewi nkasema nakuja. Hapo muda saa 4 interview saa 8.

Nkajivuta vuta saa 8 na unusu mchana nko pale getini nkaruhusiwa nkachoma ndani, in short nlikuwa mwenyewe tu, so nkaingizwa interview room nkakuta panel ya mtu tano pale kati nkapatwa na kizunguzungu cuz ilikuwa mara ya pili kupiga interview sikujua watu wanaweza kuwa wengi wananishambulia kwa maswali.

Ukapigwa utambulisho pale swali zikaanza "Tell us about yourself?" Sielewi nasemaje nkajikanyaga pale, nkaulizwa unatujuaje IOM, hapo nkasema kabisa sijui kitu kuhusu IOM, wakauliza job responsibilities and duties za HR walizozisema, nkajibu kiukweli mmeniita fasta sana na katika harakati zangu za kutafuta ajira si mambo yote au matangazo yote ntakumbuka. Wakaanza maswali mengine yani nilikuwa najikanyaga sana.

Moja ya interview ambazo nilikaa saa naongea tu licha ya kwamba nilikuwa naenda chaka ni hiyo. Mwishoni nilipomaliza maswali yao nkaambiwa "Asante kwa kuja".

Cha msingi ni kutojutia bali ni kurekebisha makosa yanayotokea, na kufurahia ikibidi hiyo ndo histori yenyewe.
 
Kulikuwa na nafasi moja ya kuzibua vyoo katika taasisi fulani hivi ikatangazwa mtandaoni, kutokana na shida zilizonizonga nje ya taaluma yangu nikasema potelea mbali ngoja nitose ndoana yangu.

Kuitwa kwenye interview nakuta tupo watu 138 km sijakosea.nikasema haya sasa kigezo ilitakiwa ni form four tu nami nna diploma ingawa wapo waliokuwa na bachelor nao wakajifanya ni form four tu.

Interview ilikuwa na maswali manne moja wapo kuhusu corona (mwaka huu hiyo) baada ya pale kutokana na yale maswali kiukweli matatu nilikuwa najiamini nayo mnoo ila matokeo yake nikapata alama wastani wa 13.7@swali na tulipita alama hizo 50 watu kama 13 hivi wakachukua watu5 wale wa juu kuwapeleka kwenye oral siku inayofuata.

Ila maswali yao na vitu nilivyokesha usiku kusoma ni tofauti niliumia sana. Nilitegemea kujikwamua kidogo nikapata hasira kwani hata nauli nilikopa na bado sijailipa
 
Kulikuwa na nafasi moja ya kuzibua vyoo katika taasisi fulani hivi ikatangazwa mtandaoni, kutokana na shida zilizonizonga nje ya taaluma yangu nikasema potelea mbali ngoja nitose ndoana yangu.

Kuitwa kwenye interview nakuta tupo watu 138 km sijakosea.nikasema haya sasa kigezo ilitakiwa ni form four tu nami nna diploma ingawa wapo waliokuwa na bachelor nao wakajifanya ni form four tu...
Mkuu uko vizuri ipo siku bahati itakuangukia...ila ushauri mwaka huu upige degree Mungu atakujahalia upate mkopo wa Magufuli 👏
 
Aisee niliitwa kufanya interview kwenye Hotel flani Financial Assistance kufika pale nikakutana na mtoto mkali wa Kijerumani.

Balaaa likaanza kwenye lugha gongana kijerumani kiengereza baadae akaelewa akapunguza makali.

Alikuja kuniuliza swali niko Single utajiskiaje kufanya kazi na Boss wako mwanamke ndo Mimi alafu ananiangalia kimahaba.

Nilikosa kazi kwa hili swali tuko conference room wawili tuu wazungu wana interview za mitego sana.
 
Yangu nilifanya na watu wanaitwa Wezesha wazawa microfinance, Hawa jamaa walipigia simu kazi ambayo nishaomba miezi nane ishapita,,, Wakasema Njoo kwa ajiri ya interview ,nafika pale ofisin pao nawaambia niliitwa kwa ajili ya interview wanabaki wananishangaa tuu, Kumbe aliyebipigia simu hata hakutoa taarifa kwa wenzake...

🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Natamani kuendelea lakini hapo kwenye mkopo ndio shida maana hela zenyewe zinakuwa hazitoshi na bado nina malengo fulani hivi
Jaribu kusoma hivyo hivyo...nimeona watu wamekosa kazi diploma ila baada ya degree wakapata kazi nzuri,ukali wa maisha ukapungua.
Kila la kheri ukipata chuo karibu na nyumbani na kozi nzuri mkopo waweza tosha👏👏
 
Jaribu kusoma hivyo hivyo...nimeona watu wamekosa kazi diploma ila baada ya degree wakapata kazi nzuri,ukali wa maisha ukapungua.
Kila la kheri ukipata chuo karibu na nyumbani na kozi nzuri mkopo waweza tosha
Nachukua ushauri wako ili niutafakari upya.
Lakini kupata kazi ni bahati na wala si ukubwa wa vyeti
 
Yangu nilifanya na watu wanaitwa Wezesha wazawa microfinance, Hawa jamaa walipigia simu kazi ambayo nishaomba miezi nane ishapita,,, Wakasema Njoo kwa ajiri ya interview ,nafika pale ofisin pao nawaambia niliitwa kwa ajili ya interview wanabaki wananishangaa tuu, Kumbe aliyebipigia simu hata hakutoa taarifa kwa wenzake.

Nilikaa pale Kama saa moja hivi ,nikawafata nikawambia Kama hamna interview naombeni mnirudishie gharama zangu za usumbufu, niliwapelekesha hawatakuja sahau , baadaye Wakasema tutafanya mida ya saa nane nikawambia sawa,, nikatoka pale nikaenda kunywa k- vant na safari mbili, mda ulivyofika wa saa nane maana nilikuwa Niko peke yangu tunafika kwenye interview room nikawaambia mie nahitaji hela zangu na mda niliyopoteza.

Nilivyokuwa nimechange walitoa nauli wajinga wale.
 
Miaka kama 7 iliyopita niliitwa kwenye usaili kwenye International Organization moja yenye ofisi hapa nchini, hawa wako chini ya UN..Tulikuwa watatu kwenye nafasi yetu na walihitajika watu wawili tu. mimi nilikuwa wa mwisho kabisa kuingia kwenye chumba cha usaili lakini kila mtu aliekuwa anatoka kwenye room ya usaili alikuwa na sura ya upole sana. Ikafika zamu yangu maana ndiye nilikuwa wa mwisho.

Waendesha usaili wote walikuwa wazungu then wanatumia lafudhi ile ya ndani kabisa. Nilipigwa maswali technical, nikawa sijui hata ninachojibu wala lugha ninayoongea . Wale mainterviewer wakawa hoi kwa kicheko. Walivyoona akili haiko pale ishahama kwa panick, wakanipa swali dogo angalau nirudi kwenye hali ya kawaida. Wakaniuliza kwa kiingereza " Bendera ya taifa ina rangi ngapi na maana ya tafsiri ya hizo rangi" huwezi amini Nilipuyanga 😀😀 naongea vitu hata mwenyewe sivielewi,Jamaa wakaangua kicheko tena. Kiukweli ile interview nilipanick sana

Mpaka leo sijui aina ya lugha niliyokuwa natumia kujibu maswali kwenye ile interview. Nikaambulia kumla mdada aliyekuwa anatuita kwenda kwenye room ya usaili angalau nikajipooza machungu ya kuchekwa.
 
Miaka kama 7 iliyopita niliitwa kwenye usaili kwenye International Organization moja yenye ofisi hapa nchini, hawa wako chini ya UN..Tulikuwa watatu kwenye nafasi yetu na walihitajika watu wawili tu. mimi nilikuwa wa mwisho kabisa, kuingia lakini kila mtu aliekuwa anatoka kwenye room ya usaili alikuwa na sura ya upole sana. Ikafika zamu yangu maana ndiye nilikuwa wa mwisho...
hahaha Pole mkuu ndo ilikuwa interview yako ya kwanza nini?.....kitu nilichojifunza kwenye interview yoyote inabidi ujiamini na uwe na taarifa za kutosha bila hivyo utapanick......maana watu wote kwenye interview wanakuwaga na panicking ya ajabu sana ndio maana kuna umuhimu wa presentation vyuoni zile zinasaidia kutengeneza kujiamini na kujieleza
 
hahaha Pole mkuu ndo ilikuwa interview yako ya kwanza nini?.....kitu nilichojifunza kwenye interview yoyote inabidi ujiamini na uwe na taarifa za kutosha bila hivyo utapanick......maana watu wote kwenye interview wanakuwaga na panicking ya ajabu sana ndio maana kuna umuhimu wa presentation vyuoni zile zinasaidia kutengeneza kujiamini na kujieleza
Ilikuwa interview ya kwanza kufanyiwa na wazungu halafu wanaongea rafudhi ile ya ndani.Asilimia kubwa ya maswali sikuyaelewa, nikawa napuyanga tu. Walicheka sana wale jamaa nadhani walibaki kusimuliana😀😀
 
Ilikuwa interview ya kwanza kufanyiwa na wazungu halafu wanaongea rafudhi ile ya ndani.Asilimia kubwa ya maswali sikuyaelewa, nikawa napuyanga tu. Walicheka sana wale jamaa nadhani walibaki kusimuliana😀😀
sipati picha mizungu ilivyokua inacheka
 
Ilikuwa interview ya kwanza kufanyiwa na wazungu halafu wanaongea rafudhi ile ya ndani.Asilimia kubwa ya maswali sikuyaelewa, nikawa napuyanga tu. Walicheka sana wale jamaa nadhani walibaki kusimuliana😀😀
Wanalafudhi ngumu sana inahitaji umakini sana kuelewa wanazungumzia nini na wao wenyewe wapunguze speed ya uongeaji.....

Ila kama wapo wazungu tu njia ambayo niliyotumia mara 3 kupata ajira ni licha ya kuwa na quality nzuri ila pia kutia huruma, yani nagusa quality zangu na najivisha umasikini ambao hauelezeki....
 
Miaka kama 7 iliyopita niliitwa kwenye usaili kwenye International Organization moja yenye ofisi hapa nchini, hawa wako chini ya UN..Tulikuwa watatu kwenye nafasi yetu na walihitajika watu wawili tu. mimi nilikuwa wa mwisho kabisa, kuingia lakini kila mtu aliekuwa anatoka kwenye room ya usaili alikuwa na sura ya upole sana. Ikafika zamu yangu maana ndiye nilikuwa wa mwisho...
kuna interview nlifanya na clown paints, ilikuwa interview yng ya pili kufanya, nakumbukaga maswali tu majibu waga najaribu kukumbuka mpaka leo lkn wap
 
Yangu nilifanya na watu wanaitwa Wezesha wazawa microfinance, Hawa jamaa walipigia simu kazi ambayo nishaomba miezi nane ishapita,,, Wakasema Njoo kwa ajiri ya interview ,nafika pale ofisin pao nawaambia niliitwa kwa ajili ya interview wanabaki wananishangaa tuu, Kumbe aliyebipigia simu hata hakutoa taarifa kwa wenzake...
😁😁😁😁😁😁
 
Back
Top Bottom