Nyerere alikosea sana pale alipoowaaminisha Watanzania kuwa ni ufanyakazi na ukulima pekee ndivyo ambavyo vinaweza kuwaendeleza kingine chochote ni uvivu.hebu tazama maeneo mengi yanayokaliwa na waislamu hapa TZ,mfano Tanga,Lindi,Mtwara,Kigoma,Tabora,Ruvuma,Zanzibar utagundua ndio maeneo yaliyo nyuma kiuchumi kutokana na watu wake kuwa wavivu wasiopenda kufanya kazi.huku kwetu kanda ya ziwa kuna maeneo kama Mhunze-Kishapu,Nyanguge-Magu nayo yamechelewa sana kuendelea kutokana na kutopenda kazi kunakoletwa na kukosa maarifa flani.
Waislamu ndiyo wahanga wa kwanza wa falsafa hii ya nyerere kwa vile wengi wao si wafanyakazi na wakulima bali ni wafanyabiashara.
Badala ya nyerere kuuangalia ufanyabiashara na kuusaidia yeye aliupiga vita kwa njia kama za kuweka ugumu kuingiza vitu nchini,ugumu wa kusafiri nk.
Suala jingine ni asili ya Waislamu wenyewe kujiwekea malengo makubwa kimaisha, mfano kwa kijana wa Kiislamu kufanyakazi ya mshahara mdogo kwake yeye ni sawasawa na utumwa, atakuwa radhi akae bila kazi kuliko kufanya kazi ya namna hiyo na ndiyo maana utawakuta kuchwa wakiwaza namna ya kwenda nje kwenye maslahi zaidi.
Na kweli wakienda nje utawakuta wakifanya kazi na kusaidia makwao, mfano ukienda Tanga sehemu za sahare na mwambani nyumba karibu zote zilizojengwa kule ni za Watanga wenyewe waliopo nje lakini kwa vile zimepangishwa wahamiaji halafu WaTZ wameaminishwa kuwa "Waislamu ni wavivu" basi wengi huamini kuwa mji unajengwa na wahamiaji.
Kodi zinazopatikana na nyingine zinazotumwa kutoka nje ndizo zinazofanya nyumba nyingi "jiko nalo likafufuka moshi" vinginevyo ingekuwa ni janga kwa vile tu serikali ya nyerere ilitambua ukulima (ufugaji na uvuvi) na ufanyakazi pekee ndivyo ambavyo vinaweza kumletea maendeleo Mtanzania.
...bado kosa na kasumba za nyerere zinaendelea kuwatafuna Watanzania.