Juliana Shonza
JF-Expert Member
- Dec 19, 2012
- 2,009
- 1,607
Yapo mambo mengi yamekuwa yakiendelea katika kipindi hiki, ambapo mengi katika mambo hayo ni ya hovyo, machafu na yasiyofaa katika jamii lakini yanahalalishwa kwa jina SIASA. Mambo yenye kushusha heshima ya mtu, kudhalilisha utu wake na kufedhehesha jamii yake siku hizi hayakemewi tena, sio na watu wenyewe ama taasisi bali hata Serikali yenyewe imekalia kimya mambo hayo na jamii wameyapa jina jipya, hauitwi tena UDHALILISHAJI bali inaitwa SIASA CHAFU.
Kwa muda mrefu, binafsi nimekuwa nikitukanwa sana hapa jamvini, tena na watu wenye heshima zao na wengine nawajua kwa sura na majina halisi lakini hata hawashtuki, nao huingia kwenye mkumbo huu wa matusi, kunidhalilisha na kunishushia heshima..wakati mwingine tunalazimika kuvumilia kwa sababu ndivyo ilivyo jamii yetu lakini hakika ni lazima tukemee tabia hizi zinazoimarika ndani ya jamii yetu...Watanzania walikuwa ni watu wenye kutolewa mfano kwa kuheshimiana, kupendana na kuishi kijamaa lakini hali ya sasa ni ya mazungumzo ya chuki, uhasama, kudhalilishana na kuvunjiana heshima.
Nimeiona VIDEO inayozunguka kwenye mitandao ya kijamii, ikimdhalilisha Mama Regina, huyu ni Mwanamke mwenzangu lakini pia ni kama Mama yangu mzazi kwa umri wake na mtu mwenye heshima ya kipekee katika jamii yetu, si jambo jema hata kidogo, Mimi nalipinga jambo hili kwa namna yeyote ile itakavyotafsiriwa.
Hii sio siasa, na nawaonya Vijana wenzangu wa CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) ikiwa wao ndio wanaozisambaza video hizi, wajue wanafanya makosa kisheria na ni kukosa adabu na heshima kwa wazazi wetu. Nimewataja Vijana wenzangu wa CCM kwa sababu VIDEO hiyo nimeiona kwenye simu ya mmoja wao akidai ametumiwa na kijana anayeitwa Peter Kasera (ambaye nae ni kijana wa UVCCM) hizi sio tabia za wanachama ama Vijana wa CCM, MNATUDHALILISHA. Na nimeamua kukutaja kwa jina halisi ili uone haya kokote ulipo na ujutie kitendo chako, ikiwezekana uombe radhi kwa kitendo hicho.
Lakini pia hawa wapiga picha wanaokuwepo kwenye shughuli za CHADEMA na UKAWA hivi mnaishi nao vipi..? maana event ile ni ya "wanamabadiliko" imekuwaje VIDEO ile imevuja..? It's obviously kuwa mpigaji picha deliberately ameamua kuitoa kwa maslahi yake na ya wale anaowajua yeye.
Maoni yangu:
Watu hawa wote wachukuliwe hatua, kuanzia yule aliyefanya kitendo kile, aliyevujisha VIDEO pamoja na hawa wanaoendelea kusambaza..kwani ni hatua ya juu kabisa ya UDHALILISHAJI aliyofanyiwa Mama Regina.
NB:
Sitoiweka VIDEO hiyo hapa, na siitaji mtu yeyote katika uzi huu ama mwingine aweke VIDEO hiyo ama yenye mfano wa hiyo, hata kama ni SIASA jamani kuna maisha baadae..TUACHE UDHALILISHAJI, imetosha sasa.
Kwa muda mrefu, binafsi nimekuwa nikitukanwa sana hapa jamvini, tena na watu wenye heshima zao na wengine nawajua kwa sura na majina halisi lakini hata hawashtuki, nao huingia kwenye mkumbo huu wa matusi, kunidhalilisha na kunishushia heshima..wakati mwingine tunalazimika kuvumilia kwa sababu ndivyo ilivyo jamii yetu lakini hakika ni lazima tukemee tabia hizi zinazoimarika ndani ya jamii yetu...Watanzania walikuwa ni watu wenye kutolewa mfano kwa kuheshimiana, kupendana na kuishi kijamaa lakini hali ya sasa ni ya mazungumzo ya chuki, uhasama, kudhalilishana na kuvunjiana heshima.
Nimeiona VIDEO inayozunguka kwenye mitandao ya kijamii, ikimdhalilisha Mama Regina, huyu ni Mwanamke mwenzangu lakini pia ni kama Mama yangu mzazi kwa umri wake na mtu mwenye heshima ya kipekee katika jamii yetu, si jambo jema hata kidogo, Mimi nalipinga jambo hili kwa namna yeyote ile itakavyotafsiriwa.
Hii sio siasa, na nawaonya Vijana wenzangu wa CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) ikiwa wao ndio wanaozisambaza video hizi, wajue wanafanya makosa kisheria na ni kukosa adabu na heshima kwa wazazi wetu. Nimewataja Vijana wenzangu wa CCM kwa sababu VIDEO hiyo nimeiona kwenye simu ya mmoja wao akidai ametumiwa na kijana anayeitwa Peter Kasera (ambaye nae ni kijana wa UVCCM) hizi sio tabia za wanachama ama Vijana wa CCM, MNATUDHALILISHA. Na nimeamua kukutaja kwa jina halisi ili uone haya kokote ulipo na ujutie kitendo chako, ikiwezekana uombe radhi kwa kitendo hicho.
Lakini pia hawa wapiga picha wanaokuwepo kwenye shughuli za CHADEMA na UKAWA hivi mnaishi nao vipi..? maana event ile ni ya "wanamabadiliko" imekuwaje VIDEO ile imevuja..? It's obviously kuwa mpigaji picha deliberately ameamua kuitoa kwa maslahi yake na ya wale anaowajua yeye.
Maoni yangu:
Watu hawa wote wachukuliwe hatua, kuanzia yule aliyefanya kitendo kile, aliyevujisha VIDEO pamoja na hawa wanaoendelea kusambaza..kwani ni hatua ya juu kabisa ya UDHALILISHAJI aliyofanyiwa Mama Regina.
NB:
Sitoiweka VIDEO hiyo hapa, na siitaji mtu yeyote katika uzi huu ama mwingine aweke VIDEO hiyo ama yenye mfano wa hiyo, hata kama ni SIASA jamani kuna maisha baadae..TUACHE UDHALILISHAJI, imetosha sasa.