Tuache kujifariji 'kipuuzi' kuwa hata sisi tuliwafunga 5 - 0 mwaka 2012, ukweli ni kwamba kipigo chao kimetuuma mno

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,638
109,001
Halafu msisahau Sisi tulipowafunga wao walikuwa na Kikosi dhaifu na Mgogoro mkubwa Klabuni kwao wakimtaka aliyekuwa Kiongozi wao Lyoed Nchunga ajiuzuru.

Na nakumbuka Usiku wa kuelekea Mechi hiyo Mchezaji na Rafiki yangu mkubwa tu Jerryson Tegete alinipigia Simu na kuniambia kuwa Mechi yao ya Kesho wanaenda kuachia Wafungwe nyingi na sisi Simba SC ili huyo Kiongozi aondoke kwani hata wao Wachezaji walikuwa hawamtaki.

Na nakumbuka baada ya Kichapo kile cha Goli 5 kwa 0 tulizowafunga Kesho yake Mashabiki wa Yanga SC wenye Hasira Kali walienda Nyumbani kwa Nchunga huku wakiwa na Mapanga, Visu na Madunu ya Mafufa ya Taa wakimtaka atangaze kuachia ngazi la sivyo wanamdhuru Yeye na Familia yake.

Kilichotokea baada ya hali kuwa mbaya vile na Yanga SC ni Timu Kubwa na yenye Maslahi kwa nchi (hasa Kisiasa) ni Watu wa Usalama wa Taifa (TISS) kumtaarifu Rais wa wakati huo Kikwete (ambaye ni mwana Yanga SC lia lia kama Mimi GENTAMYCINE nilivyo mwana Simba SC kindakindaki) juu ya Hatari hiyo ya Kiusalama ndipo haraka sana Kikwete akampigia Simu Nchunga na kumwambia awaachie Yanga SC Timu yao wasije kumuua bure.

Na kweli baada ya muda mfupi tu aliyekuwa Kiongozi wa Yanga SC wakati huo Lyoed Nchunga akatangaza kuachia Ngazi Yanga SC ndipo pakatulia na Amani kurejea.

Sasa wana Simba SC Wenzangu kwa Simba SC yetu hii ya sasa tuliyokuwa tunatamba nayo Kutwa kuwa tumesajili vizuri, tuna Mastaa wengi, tuna Utajiri mkubwa, tuna Uongozi thabiti, imefika Robo Fainali ya CAFCL mara Nne, ni ya Saba (7) kwa Ubora wa Viwango vya CAF Barani Afrika na kwamba imeweza Kuvihenyesha hadi Vigogo vya Afrika akina Wydad Casablanca FC na Al Ahly FC tunapata wapi uhalali wa Kipumbavu kujifariji kuwa hata Sisi mwaka 2012 tuliwafunga Yanga SC Goli 5 kwa 0?

Wala tusidanganyane hapa Jamiiforums na tusizuge Ukweli ni kwamba kwa Simba SC yetu tuliyokuwa tukijitapa/tukijifaragua nayo Kutwa Kufungwa Goli zile Takatifu na za Kishalubela 5 kwa 1 Jana kwa Mkapa ni Aibu na Fedheha Kubwa sana Kwetu na tena tungekuwa na Akili timamu ni bora tu tungenyamaza ili wana Yanga SC watukoge (watucheke) mpaka hamu yao iishe na Sisi tuje Kuibuka kivingine huko mbeleni kama sehemu ya Kujipoza na kujipa tu Moyo.

Naomba katika Upuuzi, Ushamba na Unafiki wenu huu Mimi mwana Simba SC Mwenzenu mnitoe na ukweli ni kwamba Kipigo Kimetuumiza, Kimetuaibisha na Kimetutia Adabu kuwa tucheze na tutambe na Wote hapa Barani Afrika ila siyo kwa Yanga SC na Yanga SC ndiyo Wababe wetu na tusipokuwa makini wataendelea Kutuadhibu na hata mwaka huu (Msimu huu) wanaenda tena Kuchukua/Kubeba hili Kombe kwa mara ya Tatu mfululizo na hili nilishalisema hata katika moja ya Uzi wangu hapa Jamiiforums kabla hata ya Msimu huu mpya wa 2023/2024 kuanza, ila tatizo lenu baadhi yenu huwa mnanichukulia Poa sana (Kimazoea mno) Mimi GENTAMYCINE "Purely Talented, Charismatic Fella, Game Changer and Entertainer" hapa Jamiiforums mkisahau kuwa Mimi ni ZAWADI YENU KUU NA TUKUKA YA KIMAONO NA KIFIKRA TUNDUIZI hapa Jamvini.

Hongereni Yanga SC kwa Kutunyoosha na hakika mmetunyoosha na Kuthibitisha kuwa nyie huwa MNASAJILI na Sisi huwa tunafanya MAJARIBIO ya USAJILI na tutaendelea Kuharibikiwa kila Msimu huku tukiwa na Kauli yetu ya Kipumbavu kuwa Yanga SC inahonga au inabebwa wakati ukweli ni kwamba Yanga SC wako imara marudufu ya Simba SC yetu yenye Mwekezaji Muongo na Tapeli (Samjo na Panjuani) anayesema Kawekeza Tsh Billioni 20 lakini ukimuuliza au ukihoji ziko Benki gani hakupi Jibu na sana sana ataanza Kukununia au kuwatupia Mpira FCC.

Na tutafungwa mno tu Kudadadeki.
 
Watu walisema usajili wenu ni wa ki mihemko na mlitumia ha nyingi ila kikosi hamna kitu. mkakataa

Mkaambiwa mpira wenu ni papatu papatu haueleweki mkasema mnatizama Objective

Mkambiwa siku mkijichanganya kwenye timu yenye uwezo mtaumia mkasema tumetoa dro na timu bora Africa hivyo hakuwa wakuwafunga

Haya sasa yamewakuta
 
Wacha tujikumbushe...kila mtu afanye anachokiweza....
IMG-20231105-WA0049.jpg
 
Watu walisema usajili wenu ni wa ki mihemko na mlitumia ha nyingi ila kikosi hamna kitu. mkakataa

Mkaambiwa mpira wenu ni papatu papatu haueleweki mkasema mnatizama Objective

Mkambiwa siku mkijichanganya kwenye timu yenye uwezo mtaumia mkasema tumetoa dro na timu bora Africa hivyo hakuwa wakuwafunga

Haya sasa yamewakuta
Sema Genta Mara zote alikuwa anazungumza ukweli ikiwemo uhalisia wa ubovu wa kikosi chao.
 
Watu walisema usajili wenu ni wa ki mihemko na mlitumia ha nyingi ila kikosi hamna kitu. mkakataa

Mkaambiwa mpira wenu ni papatu papatu haueleweki mkasema mnatizama Objective

Mkambiwa siku mkijichanganya kwenye timu yenye uwezo mtaumia mkasema tumetoa dro na timu bora Africa hivyo hakuwa wakuwafunga

Haya sasa yamewakuta
Mvua imenyesha, tumeona panapovuja, pamoja na kuwa, matundu yalikuwa yanaonekana wazi! Swali linakuja, wahusika, wataziba hiyo sehemu?
 
Halafu msisahau Sis tulipowafunga Wao walikuwa na Kikosi dhaifu na Mgogoro mkubwa Klabuni kwao wakimtaka aliyekuwa Kiongozi wao Lyoed Nchunga ajiudhuru.

Na nakumbuka Usiku wa kuelekea Mechi hiyo Mchezaji na Rafiki yangu mkubwa tu Jerryson Tegete alinipigia Simu na kuniambia kuwa Mechi yao ya Kesho wanaenda Kuachia Wafungwe nyingi na Sisi Simba SC ili huyo Kiongozi aondoke kwani hata Wao Wachezaji walikuwa hawamtaki.

Na nakumbuka baada ya Kichapo kile cha Goli 5 kwa 0 tulizowafunga Kesho yake Mashabiki wa Yanga SC wenye Hasira Kali walienda Nyumbani kwa Nchunga huku wakiwa na Mapanga, Visu na Madunu ya Mafufa ya Taa wakimtaka atangaze kuachia ngazi la sivyo wanamdhuru Yeye na Familia yake.

Kilichotokea baada ya hali kuwa mbaya vile na Yanga SC ni Timu Kubwa na yenye Maslahi kwa nchi ( hasa Kisiasa ) ni Watu wa Usalama wa Taifa ( TISS ) kumtaarifu Rais wa wakati huo Kikwete ( ambaye ni mwana Yanga SC lia lia kama Mimi GENTAMYCINE nilivyo mwana Simba SC kindakindaki ) juu ya Hatari hiyo ya Kiusalama ndipo haraka sana Kikwete akampigia Simu Nchunga na kumwambia awaachie Yanga SC Timu yao wasije Kumuua bure.

Na kweli baada ya muda mfupi tu aliyekuwa Kiongozi wa Yanga SC wakati huo Lyoed Nchunga akatangaza kuachia Ngazi Yanga SC ndipo pakatulia na Amani kurejea.

Sasa wana Simba SC Wenzangu kwa Simba SC yetu hii ya sasa tuliyokuwa tunatamba nayo Kutwa kuwa tumesajili vizuri, tuna Mastaa wengi, tuna Utajiri mkubwa, tuna Uongozi thabiti, imefika Robo Fainali ya CAFCL mara Nne, ni ya Saba ( 7 ) kwa Ubora wa Viwango vya CAF Barani Afrika na kwamba imeweza Kuvihenyesha hadi Vigogo vya Afrika akina Wydad Casablanca FC na Al Ahly FC tunapata wapi uhalali wa Kipumbavu kujifariji kuwa hata Sisi mwaka 2012 tuliwafunga Yanga SC Goli 5 kwa 0?

Wala tusidanganyane hapa Jamiiforums na tusizuge Ukweli ni kwamba kwa Simba SC yetu tuliyokuwa tukijitapa / tukijifaragua nayo Kutwa Kufungwa Goli zile Takatifu na za Kishalubela 5 kwa 1 Jana kwa Mkapa ni Aibu na Fedheha Kubwa sana Kwetu na tena tungekuwa na Akili timamu ni bora tu tungenyamaza ili wana Yanga SC watukoge ( watucheke ) mpaka hamu yao iishe na Sisi tuje Kuibuka kivingine huko mbeleni kama sehemu ya Kujipoza na kujipa tu Moyo.

Naomba katika Upuuzi, Ushamba na Unafiki wenu huu Mimi mwana Simba SC Mwenzenu mnitoe na ukweli ni kwamba Kipigo Kimetuumiza, Kimetuaibisha na Kimetutia Adabu kuwa tucheze na tutambe na Wote hapa Barani Afrika ila siyo kwa Yanga SC na Yanga SC ndiyo Wababe wetu na tusipokuwa makini wataendelea Kutuadhibu na hata mwaka huu ( Msimu huu ) wanaenda tena Kuchukua / Kubeba hili Kombe kwa mara ya Tatu mfululizo na hili nilishalisema hata katika moja ya Uzi wangu hapa Jamiiforums kabla hata ya Msimu huu mpya wa 2023/2024 kuanza, ila tatizo lenu baadhi yenu huwa mnanichukulia Poa sana ( Kimazoea mno ) Mimi GENTAMYCINE "Purely Talented, Charismatic Fella, Game Changer and Entertainer" hapa Jamiiforums mkisahau kuwa Mimi ni ZAWADI YENU KUU NA TUKUKA YA KIMAONO NA KIFIKRA TUNDUIZI hapa Jamvini.

Hongereni Yanga SC kwa Kutunyoosha na hakika mmetunyoosha na Kuthibitisha kuwa nyie huwa MNASAJILI na Sisi huwa tunafanya MAJARIBIO ya USAJILI na tutaendelea Kuharibikiwa kila Msimu huku tukiwa na Kauli yetu ya Kipumbavu kuwa Yanga SC inahonga au inabebwa wakati ukweli ni kwamba Yanga SC wako imara marudufu ya Simba SC yetu yenye Mwekezaji Muongo na Tapeli ( Samjo na Panjuani ) anayesema Kawekeza Tsh Billioni 20 lakini ukimuuliza au ukihoji ziko Benki gani hakupi Jibu na sana sana ataanza Kukununia au kuwatupia Mpira FCC.

Na tutafungwa mno tu Kudadadeki.

Team zote mbovu tu!
 
Back
Top Bottom