Wanajamvi......Ntawaletea taarifa kuhusu kashfa moja ndani ya hili shirika. Wataalamu wa TTCL na baadhi ya viongozi waandamizi wamekasirika kweli kweli. Wameudhiwa na urasimu unaoendelea ya kiutawala. Najaribu kutafuta nyaraka muhimu kisha ntawatumia. Kwa kifupi ni kwamba, kuna kampuni moja kubwa sana ya mawasiliano (satellite) ambalo kwa gharama yake ilikuwa tayari kuinyanyua TTCL. Jamaa walikuwa tayari kuja kuwekeza katika miundombinu ya TTCL na baada ya miaka mitano, hii miundombinu ingekuwa ya serikali kwa 100%. Sharti tu ni wagawane mapato yatakayotokana na huduma za hawa jamaa wa satelite.
Nasikia jamaa wamefukuzwa na shirika, huku shirika ikinunua huduma zao kupitia third party (dalali) kwa gharama za juu zaidi. Hii issue ni serious kwa maana kwamba, serikalii hii inatafuta wawekezaji wa kila aina lakini hawafanikiwi kuwapata hawa wakubwa. Ninawahaidi, Nikishapata nyaraka muhimu ntakuja kuzianika humu ndio mjue hii serikali kamwe haitafanikiwa.