TTCL Mnazingua sana tena sana

TTCL Mnazingua sana tena sana

Mwanongwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2023
Posts
867
Reaction score
805
Hivi ninyi TTCL hii ndiyo nyumbani kumenoga?

Yaani huduma za kifedha kwenu ni chamgamoto kubwa sana tena sana.

Yaani mnashindwa kuunganisha na mitandao mingine.

Pesa zikiingia kwenye namba ya TTCL ni lazima uende kwa wakala na mbaya zaidi mawakala wenu kupatikana ni mtihani mkubwa

Hata huduma ya kulipia bill kwenda mitandao mingine hiyo huduma haipo.

Siyo siri kama mmeshindwa kuendesha shirika kufunga siyo dhambi.


Marekebisho gani mnayafanya mwaka mzima huku wateja wakiendelea kupata shida

Au kwenu ninyi mteja ni fala
 
kampuni ina changamoto hivyo bado uko nao tu, kwa mteja wa namna yako inabidi wakupe tuzo kabisa.
Mpaka unaanika madhaifu yao ilhali kuna kampuni kibao zenye huduma nzuri zaidi yao, ambapo ungeamua tu kubadili laini.
 
Mala ya mwisho kuona vocher ya ttcl ilikua mwaka 2019
 
kwa sasahivi ttcl ni laini ya kupiga simu , kupokea + sms tofauti na hapo unajitafutia janga mwenyewe.
 
Ni wazuri Sana kwenye unlimited data kwenye internet hasa kama mkongo imepita kwako unapata unlimited home internet kwa garama isiyozidi 60,000 kwa mwezi
 
Mimi natumia lain yao tangu 2021 niko arusha,, aise kwenye Internet ni wazuri Sana naenjoy mno vifurishi vyao vingi havina muda wa ukomo
 
TTCL ni wazuri sana kwenye huduma ya Internet na Vifurushi vya kupiga simu. Huduma nyingine zote ni majanga especially kwenye SMS na hizo huduma za kifedha
 
Back
Top Bottom