Hivi TTCL lina uongozi? Kama lina uongozi, wana mission na vision? Ni ajabu kuna watz hasa wa kizazi cha sasa hawafahamu kama tuna shirika la mawasiliano la taifa
Tatzo hawajitangazi kabisa nimeingia website yao sijaona hiyo habari ya 4G...kwa nini ttcl hawauzi line za simu kama haya makampuni mengine?
Hii laana tulioirithi ya kutokuwa na uzalendo inatufanya tushindwe kuthamini mashirika yetu mfano TTCL wana bei nafuu kuliko makampuni yote ya simu lakini sisi hatuoni ilo tunabakia kuumizwa na wezi w mchana kina voda tigo na airtel. MUNGU atukomboe toka laana hiyo.
Haya Mimi nimekutana na kadhia hiyo, kwenye web site yao hawajatangaza!
Angalia usichepuke huko...
Nimealikwa uzinduzi.
conflict of interest ndio sababu kwa sababu viongozi wana share Vodacom, Tigo, Airtel , tena mkakati wao ulikuwa ni kuiua kabisa ila wafanyakazi ndo waliiokoa
Angalia vizuri bei za vifurushi vyao. Hakuna kifurushi cha 2,000/=.Sisi tutakuwa wazalendo kama hao ttcl wataonesha juhudi. Tatizo viongozi wengi wana conflict of interest ,wana ubia na tigo, voda, airtel.
Ni bora ninunue Gb ttcl kwa 2000 maana najua pesa itabaki hapa, kuliko ninunue 1gb tigo pesa iende kwa tajiri mzungu ulaya
Ni kama unaisoma akili yangu. Kama kuna shirika lililo wanyanyasa watanzania wazalendo na kuthamini wahindi ni hili TTCL. Walishawahi kubambika wateja bili zisizowahusu. kifupi hawa na Tanesco hakuna tofauti. Linaongozwa na waswahili na mambo yake ni hovyo. Wabaki na mkongo wa taifa, mambo mengine hawataweza.Hakuna laana yoyote ila wenye laana ni Ttcl wenyewe. Walitutesa sana hawa jamaa,ilifika wakati uhonge milioni upate laini ya simu. Hawana tofauti na Tanesco. Unadai shirika halina pesa,mtu akitaka huduma yako ili upate pesa unataka rushwa. Huu ni wazimu. Ttcl wao walitakiwa kuwa wa kwanza kwa simu za viganjani lakini kutokana na rushwa hawakujali hilo,ilivyoanza Mobitel (sijui hata kama wengine wanaijua) walitumia gateway ya Ttcl kwa huduma zao. Cha kujiuliza hapo kwa nini kama walikuwa na facilities hizo hawakuanzisha simu za viganjani wakati ule? Rushwaaaaa
Tujiulize kama hizi bei za vifurushi vyao zimekaa kiushindani kweli na makampuni mengine binafsi. Mimi naona bei ziko juu sana.
nakubaliana nawe mkuu, lakini Viongozi wenye shares kwenye Makampuni hayo si wanajulikana, nafikiri Dk.Magufuli na Waziri wake Mkuu wanapaswa kuwambia Viongozi wenzao wachague moja: kuendelea na ajira Serikalini au kuhachia ngazi na kwenda kufanya biashara kwenye makampuni hayo.Sisi tutakuwa wazalendo kama hao ttcl wataonesha juhudi. Tatizo viongozi wengi wana conflict of interest ,wana ubia na tigo, voda, airtel.
Ni bora ninunue Gb ttcl kwa 2000 maana najua pesa itabaki hapa, kuliko ninunue 1gb tigo pesa iende kwa tajiri mzungu ulaya
Ni kweli mkuu, hapo wamekosea sana!! Hii inanikumbusa majibu ya Mvietnam, niliwahi kumuhoji hivi inakuwaje bei zenu za vifurushi havina tofauti kubwa na providers wengine - unajua alinijibu nini? Hapana, hapana sisi hatuwezi kwenda kinyume na VodaCOM - nilishangaa sana, nikawa najiuliza maswali mengi hivi hawa Vodacom ndio wamechukuwa majukumu ya TCRA au Wizara ya Mawasiliano au wanawatishia wengine wasiwe na bei tofauti na wao au kuna Cartel ya aina fulani hivi!!
Sasa kama Shirika la UMMA linataka kuhiga wenzao basi hapo tumeliwa.
Juzi kwa kipindi cha baragumu mkuu wa masoko aligusia kwa mbali kuwa TCRA ndio kikwazo wanadhibiti bei za 4g. tz hakuna soko huria!
Juzi kwa kipindi cha baragumu mkuu wa masoko aligusia kwa mbali kuwa TCRA ndio kikwazo wanadhibiti bei za 4g. tz hakuna soko huria!