Fixed Point
JF-Expert Member
- Sep 30, 2009
- 11,304
- 12,753
- Thread starter
-
- #301
nyie nanyi karibu nitawatimua na huyo mume wenu, ndo maana kuutwaa mnadanganywa mwili na roho, lol!hehehehehehe! Mwali upo?? Ni salamu tu wangu! Salamu kwa mume wetu na wanangu!
ha haaa, rafiki ni jambo gumu, lakini tunapaswa kulizingatia sanaNiliposoma kichwa cha mada nilidhan ni ya zamani kumbe ni yajana tu
'
Dah!Jambo gumu hili,trust!!!!
ha haaa, rafiki ni jambo gumu, lakini tunapaswa kulizingatia sana
ha haaa, kila la heri best, pata ambaye mtakuwa mnajieleza wote, lol!....... Mimi hapa ndipo nsipoelewa. Mtu kama anathamni mahusiano yake na kumjali mpenzi wake kama kuna mabadiliko ya ratiba kuna ugumu gani kumweleza?? Eh pengine ndio maana mimi huambiwa ninajiexpress sana................... and may be am dating the wrong men. Honestly sielewi. Yaani nikimweleza mtu ratiba yangu anaona kama am feeding him too much of unnecessary information!!! Labda nianze kudate hawa wa JF ambao wanaonekana kidogo ni waelewa!!:angry:
ha haaa, una mahusiano ya kudumu?Nikuambie kitu,nina zaidi ya miaka 30,lakini kwenye suala la mahusiano sijawahi kukutana na mkweli na zaidi hakuna kitu kinachoitwa trust,hakipo kabisa!
kumbe wewe denti best?
sasa midevu hiyo ya nini? au ndo uongo wenyewe unauanzia hapa JF kwa kutuonyesha kuwa mzee? ha haaa
cc. Lady doctor, Passion Lady, charminglady, King'asti, Smile, KOKUTONA, amu......
jamani kuna aliyenionea Nyamayao? nimemmissije sasa hapa kumwaga maujuzi yake!
mimi naona upo sahihi kabisa hapa......Kutokuwa mwaminifu, uongo, na mengine ni nadhiri ya mtu kutoka moyoni mwake. Usipojenga wewe uaminifu basi ipo shida. Wapenzi wote wanawajibika katika hili na ni ngumu sana kutanabaisha tatizo lipo wapi.
Tunatofautiana toka mtu mmoja kwenda mwingine na malezi tulikotoka ndo chanzo cha yote haya. Kinachobakia ni awaye yote kujitathimini kwamba; Je, anamthamini kwa kiwango gani mpenzi wake? anaweka mzingira gani ya kuaminika na mpenzi wake? anahitaji mpenzi wake amwamini kwa kiasi gani? anataka nini toka kwa mpenzi wake ili awe wa kumthamini zaidi?
Hii yote ni kutaka kuweka mazingira thabiti na sahili kwa mpenzi wake ili maisha yapate nafuu yake......
Poleni na majukumu wanaMMU...
Leo hili jambo la trust kwenye mahusiano limekuwa likijirudiarudia sana katika kichwa changu. Mahusiano mengi sana yanavunjika sababu ya kukosa uaminifu. Kuna vitu vingi nimekuwa nikijiuliza na kujijibu na vingine kukosa kabisa majibu. Kwa mtazamo wangu UAMINIFU ni jambo muhimu sana katika mahusiano. Mara nyingi napenda sana niwe katika hali ambayo namuamini mpenzi wangu, pia napenda sana kwa gharama yoyote ile kumfanya mpenzi wangu aniamini. Kama nikigundua ana wasiwasi na kitu ninachomwambia huwa najitahidi kumwuliza aniambie nifanye nini ili aniamini sababu sipendi akae akiwa na wasiwasi, na ukweli nitafanya hicho kitu ili tu aridhike.
Inawezekana mimi nipo complicated kidogo, huwa napenda sana mtu aniambie ukweli hata kama ni mbaya kiasi gani. Kwa kuujua ukweli nakuwa na uhuru wa nini la kufanya baada ya hapo.... kukusamehe na kuendelea na mahusiano au kukusamehe na kusitisha mahusiano (kusamehe kwangu huwa siyo option, lazima nisamehe ili niweze kuendelea na mambo yangu mengine).
Katika huu uzi nitazungumzia sana uaminifu wa mambo ya kawaida tu, siyo kutoka nje ya mahusiano (cheating). Utakuta sometimes mtu anaamua tu kudanganya kwa sababu yoyote anayoijua. Kwa mfano mtu anamwambia mpenzi wake naenda sokoni wakati anaenda salon, au naenda kwa dada wakati anaenda kwa shangazi.
Hivi ikatokea ndo upo kwa shangazi halafu dada akaja nyumbani kukuulizia wakati wewe uliaga kwenda kwa dada itakuwaje? hata kama kweli mpenzi ataamini kuwa ulikuwa kwa shangazi, utakuwa umejenga hisia gani kwake kuhusu wewe? kwa nini umdanganye?
Wenzangu mnalizungumziaje hili?
Karibuni kwa mjadala
Hakuna mtu ambae hapendi trust kati ya mahusiano. Kila mmoja anapenda siku zote aambiwe ukweli. Upande wa mahusiano kutokuwepo na trust (nazungumza strictly nje ya) husababishwa na aidha mtu wako mwenyewe ama wewe mwenyewe. Kuna mwingine kweli anaweza sema anapenda awe anaambiwa ukweli no matter what! Cha ajabu ukweli ukitoka hapo si Drama hiyo itakayofuata - Kiasi kwamba huyo mtu anajuta anaona heri kuongopa. Take note sihalalishi kukosekana kwa uaminifu, ila najaribu kueleza why kwa wengine hua hawawi waaminifu.
Kikubwa cha kuelewa mahala ambapo hakuna trust ni Kwa nini huyo mtu asiwe wazi na aongope katika suala ambalo ni la kawaida?
Kukosekana kwa uaminifu kwa misingi ya wewe (ulie mpenzi wake)
Mara nyingi kuna masuala ambayo kimsingi ukiyaangalia yanaonekana madogo sana. Kama mfano uliotoa kwa kujifanya waenda Sokoni na hali waenda Salon. Hapo ni wazi kuwa sababu kubwa moja wapo inaweza kuwa huyo mwanamke huwa na matumizi makubwa na kuwa moja ya eneo ambayo anatumia sana pesa ni Saloon. Na wajua siye wanawake, kuna style inakuhiraji uende Saloon walau mara tatu kwa wiki. Inapotokea J/2 ulienda Saloon, J/5 ulienda Saloon na Leo Ijumaa unataka kwenda Saaloon na pengine ulishawahi ongea na mtu wako safari za Saloon zipungue (or hata hamjawahi ongea but wajishuku); the safest unaweza kuaga ni kuwa unaenda Sokoni badala ya Saloon.
Yes kaongopa its a bad thing, but ukiliangalia kwa upande mwingine unatkuta anaongopa tokana na kuwa Mpenzi wake kamuona si mwelewa, ama tu hataji kuonyesha ni to what extent hilo tendo la Saloon limepewa kipaumbele na the like.
Uongo wa disaini hii kati ya wapenzi wengi hauepkiki.
Kukosekana kwa uaminifu kwa misingi ya mpenzi wako
Kuna wengine siku zote wao kuongopa ama kutokuwa wazi ni hulka yao Tena pengine inasukumwa saana na selfishness.. Kutotaka ajue vitu vyote anavyomiliki, Kutoka ajue wapi hua anaenda, kutoka ujue tu kwa sababu yoyote ile! Na mara nyingi pia pamoja na kuwa cheating imetolewa katika kuelewa kukosekana kwa uaminifu wa hivi Mara nyingi cheating ndiyo sababu kubwa sana ya wapenzi kuwa waongo kwa wenza/partners wao.
Mfano kama mliwahi gombana kwa ajili ya mtu uliyemhisi ana interest na huyo mtu anafanya Hotel Magongo, siku akiwa Hotel Magongo si rahisi kusema kuwa yupo hapo. Ama anapokuwekea silent simu ama kutoweza kupokea sababu yupo faragha na mpango wa kando akipokea hawezi sema nilikuwa faragha, atasema lingine lolote ambalo mpenzi wake atalikubali bila shida.
ha haaa, ndo maana nikawaita warembo wangu mujionee mwenyewe denti, msije ingia kwa choo cha kiume, lol!
mada inaongelea sema unaenda chooni, siyo umetoka wala siyo kufanya nini.....umenipata?Kwa hiyo hata nikiulizwa umetoka wapi? Nitowe kavu kavu NATOKA KUNYA, eti sababu nimetokea chooni,
nikisema nimetoka kujisaidia itakuwa "too general"
ha haa, hapo mimi pia nipo guilty, sijawahi taja umri wangu wa kikweli lakini kwa wale ambao hawana tija......
tofauti na hao, mimi huwa naongeza angalau miaka isiyopungua 5....
kiukweli huwa sina sababu yoyote ya msingi ya kufanya hivyo, naamuaga tu, ila kwa vile haina madhara naona poa tu
Kwa hiyo hata nikiulizwa umetoka wapi? Nitowe kavu kavu NATOKA KUNYA, eti sababu nimetokea chooni,
nikisema nimetoka kujisaidia itakuwa "too general"
Msome royna hapo juu ya post yako......
huo uongo unaoona una faida je siku mtu akigundua ulidanganya atajisikiaje?
hata sijui niseme nini hapa...... hii ni surprise.leo naomba niseme hii, tangu nimeingia JF miongoni mwa wadada ninao wapenda ww ni mmoja wao. Unajua kwann? Bse una mambo kadhaa ambayo ninayapenda. Maisha yako huigizi (nionavyo mm)
Huu uzi umenigusa sn ila ctachangia bse nimelate na najua wadau wengi watakuwa wamesema mengi.
Ila unajua nn FP, uaminifu ni kitu kizur sn na unakuwa huru na maisha yako. Yaan huna hofu na uyatendayo.
Naunga mkono mada ni nzur.