Trump ataka Waislamu wazuiwe kuingia Marekani

Trump ataka Waislamu wazuiwe kuingia Marekani

Status
Not open for further replies.
Trump akili yake haina akili. Trump ni disgrace to Americans. Candidates wote wa republicans wanamatatizo ya akili si Trump, Carson au Jeb.

However, huwa nashangazwa na waislam walio wengi mf. hawa CAIR huwa wanakimbilia kupinga na kutoa matamko kwa nguvu zao zote maneno kama ya trump ila mambo yanayochafua dini yao na kufanya wote waonekane wabaya huwa hawayapigii kelele na kuyapinga kwa nguvu zote.
 
So ata Mike Tyson na mastaa wengine Muslim watafukuzwa?
Wabadili imani tu wawe wapagani ilo wasifukuzwe. By the way, mtu kama Tyson kujiita muisilamu bado naona ni utani tu
 
Kuna viumbe viliumbwa ili kuwa mfano usiofaa kuigwa kwa mfano huyu bwana Obama
 
Iko hv kaka kuna baadhi ya waislamu huelewa vbaya mafundisho ya dini uislam wenyewe unakataza kuua NAFSI na mwenye kuua mmtu 1ni sawa na ameeua ulimwengu mzma na kuokoa mmtu ni kuokoa ulimwwngu mzma kaka so dini cyo uadui bali upendo na amani

Nakiri hadharani mimi ni muislam,lakini baadhi ya waislam wenzetu wachache wajinga wametumika na hao hao wamarekani kuuchafua uislam kwa kuwaingizia kichwani wrong scriptures amabazo aya hizo kwa tafsri yao mbaya wamezitumia kuuharibu uislam kwa kuchinja watu au kujilipua kwa kudanganywa eti watakutana viwanja vya peponi (jannat) Kitu ambacho sio sahihi. Mtume mwenyewe S.A.W alihakikishiwa hiyo pepo lakini hata siku moja hakuacha ibada na alisimama kisamamo hadi miguu ilimvimba na kutokwa jasho! Na alipoulizwa ma maswahaba kuhusu yeye kuingia peponi alijibu mwenye uhakika na hilo ni Allah S.W ! Kama mtume wa mwenyezi Mungu hana uhakika na pepo inakuwaje wewe udanganywe na ustadhi uchwara eti " Hey brother, or Sister, do you wanna have a ticket going to the jannat grounds? and you say, yeah! and he tells you, Kill as many people as possible and blow your self up" na muislam kwa ujinga unaamini wakati hata Nabii Muhamad hana uhakika wa kuingia jannat grounds japo alihakikishiwa hilo na Mungu! Sasa waislam wachache kama hawa ndio wanaoufanya uislam uchukiwe duniani. Kuna vijana siku hizi kila kitu cha duniani kwao ni kibaya! wamefuga madevu kibaao na vikanzu vifupi wanajiona wao ni zaidi hata ya maswahaba wa mtume au hata kuona kuwa baadhi ya maswahaba walikosea sana na wao ndio wamekuja eti kuulingania na kuusafisha uislam! huu ni ujinga! Mtume alifanya biashara na manaswara na aliingia nao mikataba mizuri tu. Leo hii kama yupo muislam atakayenionyesha aya au hadithi sahihi ya mtume kuwa alilipua au kuchinja hata mtu mmoja anionyeshe na mimi ntamuunga mkono, au hata kama aliwahi kumfunga mwanae au swahaba wake mabomu na akamwambie akajilipue atuonyeshe aya hiyo sio kutuletea ujinga hapa.
 
Pesa za dunia zimemlevya, bado tu kumtukana Mungu mana kila siku anaongea upumbavu.Juzi tu kawatunana watu weusi, mwache achezee hela zake, wamarekani wanamcheki tu

teh teh teh teh

huyo huyo mwenye sera za kishenzi ndiye atakuwa rais wa dunia,amini hivyo mkuu!!!
 
Ghosryder


Ghosryder maelezo yako yako vizuri, lakini tatizo ni jamii ya kiislam ambayo inaonekana imewakumbatia magaidi ( NAOMBA UNIELEWE). sijasema imewakumatia magaidi. sababu yakusema hayo ni hizi;

1. Viongozi wa dini wameshindwa kukemea ugaidi na vitendo vinavyofanywa na magaidi. Katika jamii yoyote viongozi wa dini ndio kioo cha dini wanayo iongoza, sasa basi viongozi wa dini ya kiislam wasipo kemea vitendo vya kigaidi na ugaidi wenyewe tafsiri yake katika jamii ni kuwa ugaidi ni uislam na uislam ni ugaidi.

Naamimi viongozi wa dini ya kiislam wanaelimu ya juu ya dini na wanelewa hao wanaojiita magaidi ambao wanasema wanaupigania uislam wanasimamia sehemu gani katika maandiko ya vitabu vya dini na na fikiri ndio maana hata viongozi wa dini wanashindwa kuwakemea. (hayo ni mawazo yangu tu).

2. Ni jamii ya kiislam kushindwa kukemea matendo ya kgaidi na ugaidi wenyewe. Naamini waislam wauwezo mkubwa wa kupinga vitendo vya ugaidi. lakini kuna mgawanyiko mkubwa katika hili na ndio kinachofanya waislam kushindwa katika vita ya ugaidi. kunawanao shabikia na kuunga mkono vitendo vya kigaidi na ugaidi na kunawanao upinga ugaidi lakini hawa wanaoupinga ugaidi hawana nguvu wala ujasiri wakufanya hivyo kwa sababu zifuatazo.
a) kuogopa kuonekana wasaliti wa dini yao.
b)kuhofia maisha yao.
c) kukosa ushirikiano na viongozi wao wa dini.

Haya ni maoni yangu tu.
 
Last edited by a moderator:
Nchi za kiislam ni zipi? Kuna wakimbizi wangapi wa Kimarekani kwenye hizo nchi?
'
Yuko sahihi. Wakae kwao. Na atakuwa raisi kwa sababu hategemei kura za waislam na hagombei uraisi wa waislam.

Nadhani hukunielewa, walifata nini Iraq, Libya, Saudia, Kuwait, Syria, Afghanstan, Sudan,sasa utanielewa.Huko wanapopaponda, ndio wanapopatia utajiri wa nchi zao.Wanafiki sana.hawa watu.Utakuwa umenielewa
 
Kama kuna watu nyumbani mwako ni wezi, kama na wewe unajua kwamba ni wezi na unaishi nao bila kuwakanya, lakini ukiambiwa familia yako inapenda wezi ukabisha lazima utakuwa unafaidika na wizi unaofanyika na hivyo unaunga mkono. Ukiitwa mwizi usilalamike :A S 103::A S 103::A S 103:
 
Hivi inakuwa je mtu Kama Huyu bado
Yuko juu ? Ina maana wa Marekani wengi
Wanamkubali au wanakuliana na anachosema ??
 
Hivi inakuwa je mtu Kama Huyu bado
Yuko juu ? Ina maana wa Marekani wengi
Wanamkubali au wanakuliana na anachosema ??
hi mzima wewe!
umepote sana

ndio wanamkubali kwa kuwa jamaa ni mkweli hata kama huo ukweli ni mchungu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom