Treni yaanza kwa hujuma

UZINDUZI wa safari za treni ya abiria jijini la Dar es Salaam, nusura uingie dosari jana wakati kibaka aliyetambuliwa kwa jina la Vincent Michael alipoamua kuiba vyuma vya breki katika moja ya mabehewa yaliyoegeshwa katika kituo cha Yombo.

Tukio hilo lilifanyika muda mfupi kabla ya treni iliyombeba Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe haijafika katika kituo hicho.

Msafara wa Dk. Mwakyembe aliyeambatana na waandishi wa habari pamoja na maofisa wa Sumatra na wale wa Shirika la usafirishaji la Tanzania na Zambia (TAZARA), ulikuwa unarejea stesheni ya Dar es Salaam, ukitokea katika kituo cha Mwakanga nje ya jiji.

Safari hiyo ilikuwa ni baada ya Waziri Mwakyembe kuzindua usafiri wa aina hiyo kwa treni ya Shirikla la Reli nchini (TRL), uliofanyika eneo la Ubungo Maziwa.

Mmoja wa maofisa wanaolinda katika eneo hilo la Yombo, aliyeomba jina lake lihifadhiwe kwa kuwa si msemaji, alisema kuwa walimkamata kibaka huyo wakati akitekeleza uhalifu wake pasipo kuhofia athari zitakazojitokeza endapo behewa hilo lingeanza kufanya safari zake.

Kufuatia tukio hilo kibaka huyo alibebwa katika moja ya mabehewa yaliyombeba Waziri Mwakyembe na kisha kufikishwa katika Kituo cha Polisi Tazara kwa hatua zaidi.

Pamoja na mambo mengine lakini hii biashara ya vyuma chakavu nayo imekua tatizo siku hizi wafanya biashara hiyo
wanang'oa kila kitu chenye asili ya chuma, wanatoa mifuniko ya karo barabarani, wanang'oa nguzo za taa barabarani,
wanato anondo za madirisha, yaani wamekua kama vichaa fulani!
Kuna haja ya kudhibitiwa, ili kunusuru uharibifu wa mali za watu na umma mzima!
 
UZINDUZI wa safari za treni ya abiria jijini la Dar es Salaam, nusura uingie dosari jana wakati kibaka aliyetambuliwa kwa jina la Vincent Michael alipoamua kuiba vyuma vya breki katika moja ya mabehewa yaliyoegeshwa katika kituo cha Yombo.

Tukio hilo lilifanyika muda mfupi kabla ya treni iliyombeba Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe haijafika katika kituo hicho.

Msafara wa Dk. Mwakyembe aliyeambatana na waandishi wa habari pamoja na maofisa wa Sumatra na wale wa Shirika la usafirishaji la Tanzania na Zambia (TAZARA), ulikuwa unarejea stesheni ya Dar es Salaam, ukitokea katika kituo cha Mwakanga nje ya jiji.

Safari hiyo ilikuwa ni baada ya Waziri Mwakyembe kuzindua usafiri wa aina hiyo kwa treni ya Shirikla la Reli nchini (TRL), uliofanyika eneo la Ubungo Maziwa.

Mmoja wa maofisa wanaolinda katika eneo hilo la Yombo, aliyeomba jina lake lihifadhiwe kwa kuwa si msemaji, alisema kuwa walimkamata kibaka huyo wakati akitekeleza uhalifu wake pasipo kuhofia athari zitakazojitokeza endapo behewa hilo lingeanza kufanya safari zake.

Kufuatia tukio hilo kibaka huyo alibebwa katika moja ya mabehewa yaliyombeba Waziri Mwakyembe na kisha kufikishwa katika Kituo cha Polisi Tazara kwa hatua zaidi.

Huyoo atakuwa chadema tu.
 
"I am inherently gloomy about the prospects of Africa (because) all our social policies are based on the fact that their intelligence is the same as ours, where as all the testing says not really" - James Watson!
 
Huyo kibaka atakua katumwa na wamiliki wenye Daladala, nampongeza sana Dr. Mwakyembe kwajuhudi zake lakini nilishawahi kusema je muheshimiwa Mwakyembe atawezana na wamiliki wa Mabasi makubwa na wamiliki wa Daladala??
 
Ingekuwa china huyu tungekuwa tunaongea mengine.
China wanapiga lisasi tu hawana mjadala na watu kama huyu!
 
vincent michael kwa nini wewe hujasoma kama wenzako waliomo humu ndani wanaojisifia jamii yao wanaakili kuliko jamii nyingine

hehehe! Kafika form six mkuu kapata two . ..kakosa chuo!.. We hujui wenzetu wote wasomi ... Hehehe!
 
Napenda sana maendeleo, lakini USALAMA KWANZA. Mwakyembe anachezea roho za watu, yangu macho
 
kama huwapi elimu watu ,tegemea uchawi,mazingaombwe, udokozi n.k
Maisha yakikosa matumaini watu hupoteza hamu ya kuishi na hili likitokea inakuwa liwalo na liwe (Pinda) jamii ikifikia hapo ambapo watanzania wengi wa kawaida tumefikia hufanya watu kujivunia kufanya mambo mabaya kwa hisia za kuwaharibia wale ambao inaaminika kwamba wao ndio wanaofaidi utulivu wa maisha ya taifa hili.
 
wallahi angekuwa omary au mohamed topic ingejaa matusi na kashfa, ubwabwa, madrasa, na mengine meeeengi. au jina limekosewa nn?
 
Back
Top Bottom