Trafiki wengi ilikuwa vijiwe vya kukusanya Rushwa kwa madereva na kuchelewesha safari za watu

chotera

JF-Expert Member
May 19, 2016
6,305
15,034
Wakuu,

Hivi mnajua huo utrafiki ulikua unatafutwa kwa nguvu sana ikiwamo askari wenyewe kuhonga ili wapangiwe kua trafiki? Hapa ukweli wanaujua vizuri wao wenyewe.

Tunapenda ukaguzi barabarani wenye tija lakini kama alivostuka mzee kinana ndio watu wengi hujiuliza kila hatua chache unasimamishwa, ilimradi vurugu tu barabarani, unatoka Dar hadi Mwanza au Dar hadi Mbeya ushasimamishwa zaidi ya mara hamsini hivo kupoteza muda wa safari yako bila sababu ya msingi.

Kisa wakusanye 1000 au 2000 au 5000.
Halafu faini za tochi zinazoandikwa kwa siku nchi nzima ni chache kuliko ambazo haziandikwi yaani kwenye tochi wanakanyaga elfu tano hadi elfu kumi kama wanaigiza vile.

Iwekwe idadi kwamba kila mkoa au wilaya au highway vituo vya ukaguzi ni sehemu fulani na sehemu fulani sio usimame maili moja, usimame kongowe, usimame misugusugu yaani unahisi wanakagua serious kumbe wanataka rushwa hawana lolote.

Wana madudu mengi sana afadhali wazee kama Kinana wameyaona na kuwaeleza kwa staha kiutu uzima lakini sisi tunawachana tu hali halisi.
 
Nchi imekuwa kama ina vita
Bora wangebadilishiwa na gwanda kabisa wakawa na mabaka
Maana wanakera mpaka wakati mwingine napita bila kusimama maana kama umesimamishwa mara nne kwa maili kadhaa inakera sana.
 
Mimi kuna siku niliwahi safiri Dodoma kwenda Arusha kipindi ndo ile shortcut imeanza kutumika asee kuna traffic mpaka nkajiuliza hichi ni nini?nina mda sijapita njia hiyo sijui hali ikoje kwa sasa.
 
Waondolewe tu kwa kweli. Tena waondolewe mapema iwezekanavyo. Tija yao ni ndogo sana barabarani.

Ikiwezekana wakae kwenye zile zebra tu ili kuwasaidia wanafunzi kuvuka barabara.
 
Wabaki na mauzo ya stika zao

Leo nimetoka Dar Kimara temboni saa 6:49 mchana nimeingia Morogoro 88 saa 9:34 alasiri, Kilosa saa 11:26 jioni ukitazama njiani ni kama wote wamekwenda msibani.
 
Mimi kuna siku niliwahi safiri dodoma kwenda arusha kipindi ndo ile shortcut imeanza kutumika asee kuna traffic mpaka nkajiuliza hichi ni nini?nina mda sijapita njia hiyo sijui hali ikoje kwa sasa.
Ukitoka babati kuitafuta Arusha mitaa ya minjingu

Traffic wanavaa nguo za kimasai na wanatochi unapigwa ukifika mbele unapewa picha yako kwenye whatsup
 
Wakuu,

Hivi mnajua huo utrafiki ulikua unatafutwa kwa nguvu sana ikiwamo askari wenyewe kuhonga ili wapangiwe kua trafiki? Hapa ukweli wanaujua vizuri wao wenyewe.

Tunapenda ukaguzi barabarani wenye tija lakini kama alivostuka mzee kinana ndio watu wengi hujiuliza kila hatua chache unasimamishwa, ilimradi vurugu tu barabarani, unatoka Dar hadi Mwanza au Dar hadi Mbeya ushasimamishwa zaidi ya mara hamsini hivo kupoteza muda wa safari yako bila sababu ya msingi.

Kisa wakusanye 1000 au 2000 au 5000.
Halafu faini za tochi zinazoandikwa kwa siku nchi nzima ni chache kuliko ambazo haziandikwi yaani kwenye tochi wanakanyaga elfu tano hadi elfu kumi kama wanaigiza vile.

Iwekwe idadi kwamba kila mkoa au wilaya au highway vituo vya ukaguzi ni sehemu fulani na sehemu fulani sio usimame maili moja, usimame kongowe, usimame misugusugu yaani unahisi wanakagua serious kumbe wanataka rushwa hawana lolote.

Wana madudu mengi sana afadhali wazee kama kinana wameyaona na kuwaeleza kwa staha kiutu uzima lakini sisi tunawachana tu hali halisi.
Hata mjini kama dar ni wasumbufu sana hasa kwa magari ya biashara. Nilitoka tegeta kwenda mbezi stendi nikiwa na canter tulisimamishwa vituo vitano na dereva alikuwa anatoa hela kila tulisimamishwa. Matokeo yake gharama za usafirishaji zinakuwa juu na kumwangukia mlaji wa mwisho, mlala hoi
 
Back
Top Bottom