Amri kuu ni Upendo
JF-Expert Member
- Oct 18, 2012
- 789
- 493
Unashangaa hilo mkuu?
Sijui ameshangaa nini huyu ndugu, wakati sababu iko wazi kabisa;Alishindwa kuongea kiingereza kwa sababu hakuwa Uingereza bali TANZANIA!!
Unashangaa hilo mkuu?
Mbona umekurupuka?Sasa sema basi nimedanganya nini?Au hutaki kuwa wabongo lugha yetu ni kiswahili?
Ulaya kwenyewe wazungu hawajui kiingereza,sasa ndo iwe aibu kwa polisi wa wilaya sijui ya Kankonko
wachangiaji wote mmeongea point, tusiwe watumwa kwa lugha za wenzetu, na ww mleta mada ................pia ......
Askari wa usalama barabarani wilaya ya kakonko anayejulikana kwa jina MBAYA ameshindwa kuwasiliana na Raia wa kigeni aliyekuwa anaendesha gari T7610BVV,mpaka akamuita askari mwenzake anaitwa Rudo,
Mkuu ni kweli kuwa Kiswahili ndio Lugha yetu ya Taifa, ila hilo halim-halalishii huyo Trafiki kutofahamu Kiingereza kwani amepata hiyo "ajira" kuwa kudhaniwa kuwa ana elimu stahiki itakayomwezesha kumudu majukumu yake! Na kwa hapa Tz kama nilivyodokeza mwanzo, ni kwamba Elimu bado inatolewa kwa Kiingereza! Kama ni kweli hajui hiyo lugha ina maana kwamba kachakachua vyeti ili apate ajira! Vinginevyo useme kapatia Elimu yake wasikotumia Kiingereza kufundishia!
Tatizo wabongo tunaona kiingereza kuongea eti ufahari wakati masomo yote shule ya msingi yanafundishwa kiswahili,ona fahari ya lugha yako,ndo maana hatuendelei,unanikumbusha mzee mmoja binti yake karudi toka uingereza na watoto wake mzee kuona wajukuu wanaongea kiingereza safi kaanza kumsifia binti yake "ehh mwanangu umesomesha yani vijukuu vinakata lugha kuliko hata rais"
Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
Eish! Panua mawanda ya mawazo mkuu, je angekuja mchina, au muitaliano au muhispaniola, nk bado ungeng'ang'aniza tu uache kushughulikia mambo kwa lugha yako ukomae kichwa kwa lugha za kigeni kwenye nchi yako yenye lugha yake?? Wewe tembelea nchi zao uone kama suala la kujua lugha yao ama kutoijua litawafanya wasikutie sheriani pale utakapoenda kinyume na utaratibu wa sheria zao!
sasa ndo kusema akija mfaransa nisipojua kifaransa nimechakachua vyeti,!wewe mwenyewe hujui kingereza acha hizo
Mkuu kwa Tanzania ili uajiriwe na Jeshi la Polisi unadhaniwa kuwa na Elimu isiyopungua kidato cha Nne! Na Elimu hiyo inatolewa kwa Kiingereza! Tusiwe wepesi kumtetea huyo Trafiki kwani kama hilo ni kweli limetokea basi kuna walakini mahali fulani! Na kama "Forum ya Great Thinkers" tujiulize hii tabia ya "uchakachuaji" itadhibitiwa vipi! "Mwana-usalama" aliyechakachua Elimu/Vyeti ni hatari kuliko tunavyoweza kufikiri!!
Kaka elewa kuna tofauti kubwa kati ya kufahamu lugha kwa kuiandika na kuijua lugha kwa kuongea.Pamoja na kwamba nipo upande wa traffik njoo hata huku vyuo vikuu wanazuoni kibao wenye vichwa vizuri tu katika taaluma ya lugha ya kuandika sio wazuri kabisa katika lugha ya kuongea na vyeti vyao ni genuine.
Mimi naona wachangiaji wengi hapa JF ni vilaza. Lugha ya kiingereza ndiyo inatumika kufundishia na mitihani yote inaandikwa kiingereza huyo askari alifaulu vipi hadi kupata ajira? Vyuoni kuanzia ukuruta hadi uafisa masomo ni kimombo sasa huyo askari wa wapi asijue kiingereza? Mimi naona tatizo labda mtasha mwenyewe alikuwa anaongea kiingereza cha kuchapia ndio mana jamaa akaona anampotezea wakati.
Askari wa usalama barabarani wilaya ya kakonko anayejulikana kwa jina MBAYA ameshindwa kuwasiliana na Raia wa kigeni aliyekuwa anaendesha gari T7610BVV,mpaka akamuita askari mwenzake anaitwa Rudo,
Askari wa usalama barabarani wilaya ya kakonko anayejulikana kwa jina MBAYA ameshindwa kuwasiliana na Raia wa kigeni aliyekuwa anaendesha gari T7610BVV,mpaka akamuita askari mwenzake anaitwa Rudo,
Duuu mbona m cxhangai kuxkia huyo trafic kaxhndwa kuongea kiingereza coz mbona ronaldinho A.K.A mijino alikaa man u ila mpaka leo hajui ngel, xembuxe trafic wa tz bhana