Traffic wamezidi

Traffic wamezidi

Mi ninayo ile App ya kutambua wapi kuna camera. Cha ajabu unaweza kupita sehemu ukasikia simu inaashiria uwepo wa camera. Cha ajabu ukiangalia hakana alama yoyote ya kuonyesh speed limit (50). Huu umekuwa ni wizi wa trafiki kama ulivyo wizi mwingine kwenye vyombo vya usafiri kama road licence, stika ya nenda kwa usalama, zimamto nk
 
Huo ni wizi kwa kuwa hatujitambui tunaendelea kuibiwa tuu Camera inatakiwa kibao cha Camera na Speed inayotakiwa hapo basi na speed inapozidi ukamatwe hapo hapo uandikiwe faini yako au kwa wenzetu unakutana na fine nyumbani maana gari zote zina address sasa Trafik wamekuwa wao police na mahakimu wenyewe kwa kuendelea kutumia simu zao hiyo sishangai Nchi yetu Masikini hata fikra na maamuzi ya kimasikini...
Nini kifanyike ilikuondoa adha hii?
 
Huwa napenda sana mambo ya short cut chakufanya hao traffic police wenye kiherehere akitenguliwa kiuno siku moja watajifunza aisee. Watubwanatafuta pesa kwa nguvu wao wanachukua kirahisi tuu. Ngoja nikipata safari kwenda Irnga nione upumbavu huo
 
Jaman hii tabia ya Traffic anapiga picha gari na speed kwa kujificha anamtumia Traffic wa mbele yake Dereva ataamin vp iyo picha Imepigwa eneo la speed limit?
Kwanini wanajificha?kwani lengo langu traffic ni kusaidia kuzuia au kuondoa tatizo au nini?
Tusifumbie macho hii tabia.....
Waale wa mbewe nao yao ndo haya haya njia ya kwenda TAnga
 
Tanzania bado tuna imani kwamba, mtu mwenye gari basi ana hela nyingi sana. Mfano, ukipita taa nyekundu na gari utatozwa faini. Lakini kama ukivuka hapo hapo kwa mguu kabla taa hazijakuruhusu wala polisi hakugusi wakati kosa lipo.
 
Dah.... Jumamosi nilipita na 49kph kwenye 30kph matuta ya Mikumi National park ....sikumuona askari yoyote ila nilijua ni kweli niliover speed.... nikalipa fain na kuwapongeza askari kwa kazi nzuri....na nikawaachia maji ya kunywa
Mwingine kama wewe ndio anakuja kulialia humu utafikri hakuzidisha speed.
 
Hapa daraja la kigamboni mwanzo mwanzo nilichezea mikeka "risiti" mbaka nikataka kugombana, yani ukipigwa mkonotu we toa leseni kabisa, hawakuelewi hatakama umezidi spd1.
Sasahivi tume nyooka tukifika kwenye kona ya daraja la reli tunakaa foleni taratiiiibu wana tukodolea machotu hawampati mtu tena hapa.
 
Wahamie na waenda kwa miguu...kuna jamaa wanatembea fasta sana inaweza kuwa hatari kwa usalama😛
 
Jaman hii tabia ya Traffic anapiga picha gari na speed kwa kujificha anamtumia Traffic wa mbele yake Dereva ataamin vp iyo picha Imepigwa eneo la speed limit?
Kwanini wanajificha?kwani lengo langu traffic ni kusaidia kuzuia au kuondoa tatizo au nini?
Tusifumbie macho hii tabia.....

Hahaha! Ni kweli I say. Mie nilikuwa na Landcruiser natokea Moshi kuja Dar. Sasa pale mto Wami wameandika speed limit ya 50km/hr. Nikawa nateremka lile bonde kwa spidi ya 70km/hr yaani nikaona kama natambaa. Kufika mbele nikapigwa mkono eti kwa nini nilishuka bonde la mto Wami kwa spidi ya 70km/hr kinyume na sheria.

Nikamuuliza yule askari msimamizi hivi ni busara na akili kweli kutegemea mimi nikiwa ni hii Landcuriser V8 nishuke kwa spidi ya semitrailer yenye mzigo bonde la mto Wami kwa lengo la kuweza kudhibiti gari? Nikawauliza kwani lengo la ile spidi ya 50km/hr kushuka Wami ni kwa usalama wa waenda kwa miguu au uwezo wa kumiliki gari?

Nikamwambia kama Landcruiser inatakiwa ishuke bonde la mto wami kwa 50km/hr basi semitrailer na malori yanatakiwa yashuke kwa 30km/hr. Lakini huwezi kuniambia Landcruiser na gari ndogo ni hatari kushuka bonde la mto wami kwa 70km/hr.

Kwa sababu askari wengi huwa hawana uwezo wa kufikiri na kutafakari mazingira ya sheria, walinikomalia hadi nikalipa faini kwa kushuka na Landcruisee V8 bonde la mto Wami kwa spidi ya 60-70km/hr badala ya 50km/hr nikihatarisha kudhibiti gari langu mtelemko mkali!
 
Ukidai kuletewa camera unaletewa na unaoneshwa picha yako
Utaletewa tatizo mda ndo cha msingi huwezi zalisha mda,lkn Pesa unaweza zalisha we toa tu tutunishe mfuko wa taifa.Picha italetwa ila hadi Jamaa porini amalize kazi km ulikamatwa Asubui kaa tu usubirie Picha,sijajua kama wameshapata vifaa vya kutuma picha toka porini kwenye camera had utakapokamatiwa.cha muhimu ni kuheshimu sheria tu,au andaa tu hela ya kuchangia pato la taifa.
 
Mi nikiona 50 natembea 30 au 40

Nikiona 30 ndio nasukuma kama LENA vile....

Basi wanakoma hawajawah niotea
Hata uwe makini huwezi kaa mwezi mzima bila kupewa cheti cha ubatizo labda upaki,90% ya magari yote yaliyosajiriwa yashawahi pewa cheti.
 
Wahamie na waenda kwa miguu...kuna jamaa wanatembea fasta sana inaweza kuwa hatari kwa usalama😛
Sio mbaya hata waje vitandani waangalie spidi za pampu tunazowapiga wenziwetu kama zinazidi kiwango kilichowekwa na jumuiya za wanawake.
 
This behaviour is not acceptable at all. Picha inatakiwa ioneshe position na speed limit ili kuonesha kwamba eneo ulilozidisha mwendo ndilo lenyewe. Inaudhi sana siyo siri.
 
Jaman hii tabia ya Traffic anapiga picha gari na speed kwa kujificha anamtumia Traffic wa mbele yake Dereva ataamin vp iyo picha Imepigwa eneo la speed limit?
Kwanini wanajificha?kwani lengo langu traffic ni kusaidia kuzuia au kuondoa tatizo au nini?
Tusifumbie macho hii tabia.....
Kujificha ni sahihi sio kosa
Kwani Dereva anapaswa kuheshimu alama za barabarani
kwa lugha nyepesi alama za barabarani ni sawa na traffic police ukishindwa kuziheshimu huna haja ya kumuona police ili upunguze mwendo.

Nchi za wenzetu wameweka camera's zikikunasa lazima utoe faini. Mim pia ni muhanga wa speed limits barabarani lakini siwezi laumu hawa jamaa kujificha kwani nilipaswa kutii alama za barabarani
 
Back
Top Bottom