gimmy's
JF-Expert Member
- Sep 22, 2011
- 3,283
- 3,274
Siku chache zilizopita niliandika kueleza ugandamizwaji unaofanywa na TRA uliomuhusu dereva mmoja wa semi ambae alipigwa faini ya 3,000,000/= kisa kapakia tenga 20 za parachichi na alipoulizwa risiti ya transport hakuwa nayo kwani mzigo ule haukuhusu ofisi,ilikuwa ile kawaida ya madereva kujiongezea kipato kwa vimizigo vya njiani ambacho kilimponza akapoteza ajira.
Sasa huyu ni muendelezo wa vitimbi vingine kwani dereva mwingine amepigwa faini ya 3,500,000/= kisa kapakia tenga 27 za nyanya na alipoulizwa risiti ya transport hakuwa nayo. Dereva huyu analazimika kukatwa hii pesa na ofisi kwenye mshara mpaka deni litakapoisha.
Kwakweli kama hizi ndio sheria zilizotungwa kwa ajili ya kutetea wanyonge basi hiki ni kituko.
Hivi mshahara wa Rais ni sh ngapi, mawaziri pesa ngapi, wabunge je? Hawa hawatusikii kwakuwa wao wanalipwa pesa ndefu, hivi dereva mwenye mshahara wa laki tatu kwa mwezi atakatwa hilo deni mpaka lini?
Ushauri wa bure ni kwamba;hii miradi mikubwa ilioanzishwa nchini inasababisha mateso kwa raia,ni bora tukarudi kwenye mgao wa umeme kuliko haya maisha ya karaha tunayoishi sasa.
Kwakweli nachuma dhambi ila kama Mungu anasikia vilio vyetu basi.
Sasa huyu ni muendelezo wa vitimbi vingine kwani dereva mwingine amepigwa faini ya 3,500,000/= kisa kapakia tenga 27 za nyanya na alipoulizwa risiti ya transport hakuwa nayo. Dereva huyu analazimika kukatwa hii pesa na ofisi kwenye mshara mpaka deni litakapoisha.
Kwakweli kama hizi ndio sheria zilizotungwa kwa ajili ya kutetea wanyonge basi hiki ni kituko.
Hivi mshahara wa Rais ni sh ngapi, mawaziri pesa ngapi, wabunge je? Hawa hawatusikii kwakuwa wao wanalipwa pesa ndefu, hivi dereva mwenye mshahara wa laki tatu kwa mwezi atakatwa hilo deni mpaka lini?
Ushauri wa bure ni kwamba;hii miradi mikubwa ilioanzishwa nchini inasababisha mateso kwa raia,ni bora tukarudi kwenye mgao wa umeme kuliko haya maisha ya karaha tunayoishi sasa.
Kwakweli nachuma dhambi ila kama Mungu anasikia vilio vyetu basi.