Tetesi: TRA yainunua Klabu ya Tabora United

Tetesi: TRA yainunua Klabu ya Tabora United

Hivi hapo nini kinakuwa kimeuzwa ikiwa kila kitu kinakuwa kipya. Hawa TRA si wangeanzisha tu timu yao?
wanayo ila haiko ligi kuu, hivyo wameona wanunue iliyo ligi kuu, na makao makuu yake yatakuwa Dsm, watakuwa wanachezea pale KMC
 
Ila hawa jamaa wana timu first league kama sijakosea inaitwa TRA Kilimanjaro. Nadhani wataiuza ili kuendana na kanuni za fifa zinazozuia taasisi au mtu mmoja kumiliki timu zaidi ya moja
 
Timu ziongee na viongozi vizuri huu ndio muda wa kupiga pesa
 
Hiyo timu iitwe hivyohivyo TRA kama URA ya Uganda
 
TRA wana usafiri mzuri, wana basi la timu yao inayocheza daraja la chini, sasa wakiichukua Tabora united itaimeza hiyo timu ya daraja la chini
 
Is this a Money Making project au Money consuming Project; Na kama ni Money Consuming wametu consult wenye pesa zetu ?!!! Sababu kama hii ni kweli na sio Story za Kitaa sioni inaendana vipi hii na ufanisi wa makusanyo
 
Club ya Tabora united Imeuzwa rasmi Na sasa itamilikiwa na Mamlaka ya Mapato Nchini TRA makao makuu Dar es Salaam

Uongozi wa TRA umewapa muda wa miezi mitatu waliokuwa Viongozi wa Tabora united kuhakikisha wanatafuta kazi sehemu nyingine kabla ya kukabidhi Rasmi nyaraka za Club kwa mmiliki mpya na Timu kubadilishwa jina rasmi pamoja na Anwani

Kilichotokea kwa Ihefu , kimewapitia pia Nyuki wa Tabora
Kama Hii ni Kweli basi Yale ya NHIF kutaka Kufilisika yataikuta Nchi.. TRA inayohusika kukusanya inaanza Kutumia Makusanyo tena Kwenye Kuwekeza Tena Kwenye Timu zetu hizi ambazo namba 1 na Namba Mbili Lazima Awe Yanga au Simba tu miaka nenda Rudi
 
hii nchi ni ya kishenzi sana, yani sisi tunalipa kodi wao wanatufa michongo ya kuzila pesa na kuteketeza pesa
 
Timu nyingine chini ya Mwigulu Nchemba....kuifunga Yanga afirika kumewagharimu kina christina mwagala..

Tabora United inakwenda kuwa chini ya utawala wa mbogamboga
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom