TRA: Ufafanuzi kwa umma kuhusu kodi ya pango

TRA: Ufafanuzi kwa umma kuhusu kodi ya pango

lord atkin

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2018
Posts
205
Reaction score
769
TAARIFA KWA UMMA

UFAFANUZI KUHUSU KODI YA PANGO

Dar Es Salaam, 25 Agosti, 2022:
Mamlaka ya mapato ya Tanzania (TRA) inapenda kutoa ufafanuzi kuwa Kodi ya pango hulipwa kama Kodi ya zuio inayotokana na mapato ya pango la nyumba Kwa asilimia 10

Tunaenda kuwahamisha watanzania kuwa Kodi hii si mpya bali wigo umeongezwa Ili wapangishaji wa nyumba binafsi wenye pato linaloanzia shilingi 500,000/= Kwa mwaka na kuendelea wamejumuishwa kwenye wigo wa Kodi kuanzia Julai mosi 2022.

Mwenye nyumba atapata cheti Cha Kodi ya zuio kama ushahidi wa malipo ya Kodi iliyolipwa kutokana na zuio la asilimia 10

Kwa maelekezo zaidi wasiliana nasi Kwa namba za bure;
0800-750075 au 0800-780078 au Whatsapp namba 0744-233333

"Pamoja tunajenga Taifa letu"

Imetolewa na;

IDARA YA HUDUMA NA ELIMU KWA MLIPAKODI
IMG-20220825-WA0074.jpg
 
TRA wanaelemewa
TRA wanakurupuka
TRA hawana mikakati

Sipingi hiyo kodi kutozwa ila najua fika hawawezi kuratibu hilo zoezi.

Ushauri wangu ni huu.
Zoezi liachiwe shirika la nyumba.

Biashara ya kupangisha irasimishwe

Kuwe na leseni kwa ajili ya hii biashara mtu asipangishe kama hana leseni husika.

Kodi iwe 5% na sio 10%

Sidhani kama kuna mtu atakataa kulipia.

Ila kwa niwajuavyo tiharaei hili zoezi wataishia kulamba lamba sehemu chache.

Watu hawana vision, wapo kuunga juhudi na kungoja mishahara.

Wenye sifa, wenye uwezo, wenye maono ya kuongoza hizi taasisi hawapewi nafasi.
 
TAARIFA KWA UMMA

UFAFANUZI KUHUSU KODI YA PANGO

Dar Es Salaam, 25 Agosti, 2022:
Mamlaka ya mapato ya Tanzania (TRA) inapenda kutoa ufafanuzi kuwa Kodi ya pango hulipwa kama Kodi ya zuio inayotokana na mapato ya pango la nyumba Kwa asilimia 10

Tunaenda kuwahamisha watanzania kuwa Kodi hii si mpya bali wigo umeongezwa Ili wapangishaji wa nyumba binafsi wenye pato linaloanzia shilingi 500,000/= Kwa mwaka na kuendelea wamejumuishwa kwenye wigo wa Kodi kuanzia Julai mosi 2022.

Mwenye nyumba atapata cheti Cha Kodi ya zuio kama ushahidi wa malipo ya Kodi iliyolipwa kutokana na zuio la asilimia 10

Kwa maelekezo zaidi wasiliana nasi Kwa namba za bure;
0800-750075 au 0800-780078 au Whatsapp namba 0744-233333

"Pamoja tunajenga Taifa letu"

Imetolewa na;

IDARA YA HUDUMA NA ELIMU KWA MLIPAKODI
View attachment 2335063

Tatizo kubwa la hii kodi inawaumiza wapangaji,wenye nyumba wengi hawakubali kabisa kulipa,yeye anataka kodi yake iliyokamilika,na mpangaji hasa wa vyumba vya biashara anapoenda kufanyiwa makadirio ya biashara yake tra wanamkomalia na hii kodi na huku mwenye nyumba hataki kuilipa,ukimlazimisha sana anakupa notice uhame hivyo mpangaji anajikuta mzigo unakua mkubwa na ili kupunguza maumivu kama kodi ni laki tano kwa mwezi anasema laki mbili.

Tra tafuteni namna ya kuwabana wenye nyumba direct.
 
TAARIFA KWA UMMA

UFAFANUZI KUHUSU KODI YA PANGO

Dar Es Salaam, 25 Agosti, 2022:
Mamlaka ya mapato ya Tanzania (TRA) inapenda kutoa ufafanuzi kuwa Kodi ya pango hulipwa kama Kodi ya zuio inayotokana na mapato ya pango la nyumba Kwa asilimia 10

Tunaenda kuwahamisha watanzania kuwa Kodi hii si mpya bali wigo umeongezwa Ili wapangishaji wa nyumba binafsi wenye pato linaloanzia shilingi 500,000/= Kwa mwaka na kuendelea wamejumuishwa kwenye wigo wa Kodi kuanzia Julai mosi 2022.

Mwenye nyumba atapata cheti Cha Kodi ya zuio kama ushahidi wa malipo ya Kodi iliyolipwa kutokana na zuio la asilimia 10

Kwa maelekezo zaidi wasiliana nasi Kwa namba za bure;
0800-750075 au 0800-780078 au Whatsapp namba 0744-233333

"Pamoja tunajenga Taifa letu"

Imetolewa na;

IDARA YA HUDUMA NA ELIMU KWA MLIPAKODI
View attachment 2335063
Kodi hii atakayelipa kama kawaida ni mpangaji. Maskini ataendelea kuwa Maskini tu! Poor government planners! CCM MUST GO by hooks or crooks! come 2025
 
Tulipe kodi ya nyumba zisizokua zetu kupitia luku huu wizi wakaubariki.

Kinabakia ni kushusha tuu bei za vyumba kwenye mkataba. Masta 40,000 au chumba 40,000 kwa mwaka ni 480,000. Ikishindikana iyo ni ku declare waliokwenye nyumba ni ndugu.

Sensa hii ilikua pia inautambuzi wa nyumba na idadi ya wapangaji kitaumana
 
TAARIFA KWA UMMA

UFAFANUZI KUHUSU KODI YA PANGO

Dar Es Salaam, 25 Agosti, 2022:
Mamlaka ya mapato ya Tanzania (TRA) inapenda kutoa ufafanuzi kuwa Kodi ya pango hulipwa kama Kodi ya zuio inayotokana na mapato ya pango la nyumba Kwa asilimia 10

Tunaenda kuwahamisha watanzania kuwa Kodi hii si mpya bali wigo umeongezwa Ili wapangishaji wa nyumba binafsi wenye pato linaloanzia shilingi 500,000/= Kwa mwaka na kuendelea wamejumuishwa kwenye wigo wa Kodi kuanzia Julai mosi 2022.

Mwenye nyumba atapata cheti Cha Kodi ya zuio kama ushahidi wa malipo ya Kodi iliyolipwa kutokana na zuio la asilimia 10

Kwa maelekezo zaidi wasiliana nasi Kwa namba za bure;
0800-750075 au 0800-780078 au Whatsapp namba 0744-233333

"Pamoja tunajenga Taifa letu"

Imetolewa na;

IDARA YA HUDUMA NA ELIMU KWA MLIPAKODI
View attachment 2335063
Awamu hii nchi inajengwa kwa kishindo kikubwa.
 
Nyumba nijenge kwa gharama zangu! Halafu mapato tugawane, huku ukiwa hujachangia chochote!

Yaani nitahakikisha hiyo kodi hainiathiri kwa namna yoyote ile. Na mpangaji akileta za kuleta, nampandishia tu kodi ya pango. Hataki aondoke, ampishe mwenye uwezo wa kulipa hiyo kodi.
 
Hii nzuri Sana ubunifu mzuri hongera TRA
Kodi ilikuwepo tokea kitambo na baadhi ya watu waliyofanya uwekezaji
Kwenye maeneo yao wamekuwa wakilipa
Sahivi inabidi TRA itoe elimu za kodi zote ambazo zinatakiwa kulipiwa
Ili raia wawe wanazijua na wakiambiwa wazilipe wasishtuke
Raia wengi bado elimu ya kodi hawaijui vizuri

Ova
 
Hapo ndo wametoa ufafanuzi gani.hii taasisi mbona majibu mepesi kiasi hiki.huo ufafanuzi haujajibu mambo ya msingi yaliyoulizwa na wananchi.swala la kodi sio mpya hayo siyo majibu sahihi kwasababu kama ilikuwepo toka zamani niwao wenyewe ndio walioshindwa kuweka utaratibu mzuri wakuikusanya.Watu wanataka kujua niutaratibu gani utakaotumika kuikusanya ili usimuumize mpangaji wao wanakuja na kodi sio mpya.
 
TRA wanaelemewa
TRA wanakurupuka
TRA hawana mikakati

Sipingi hiyo kodi kutozwa ila najua fika hawawezi kuratibu hilo zoezi.

Ushauri wangu ni huu.
Zoezi liachiwe shirika la nyumba.

Biashara ya kupangisha irasimishwe

Kuwe na leseni kwa ajili ya hii biashara mtu asipangishe kama hana leseni husika.

Kodi iwe 5% na sio 10%

Sidhani kama kuna mtu atakataa kulipia.

Ila kwa niwajuavyo tiharaei hili zoezi wataishia kulamba lamba sehemu chache.

Watu hawana vision, wapo kuunga juhudi na kungoja mishahara.

Wenye sifa, wenye uwezo, wenye maono ya kuongoza hizi taasisi hawapewi nafasi.
Kwa nini kusiwe na vetting za kutosha kwa wanaopewa hizi nafasi?

Kaa na Watu chini watoe abcd za nini wanaenda kufanya, uwezekano, ufanisi, uzoefu n.k.

Tatizo nadhani pia ni kuangalia lini alivaa shati la rangi fulani kama sifa kuu na weledi kuja baadae.
 
TAARIFA KWA UMMA

UFAFANUZI KUHUSU KODI YA PANGO

Dar Es Salaam, 25 Agosti, 2022:
Mamlaka ya mapato ya Tanzania (TRA) inapenda kutoa ufafanuzi kuwa Kodi ya pango hulipwa kama Kodi ya zuio inayotokana na mapato ya pango la nyumba Kwa asilimia 10

Tunaenda kuwahamisha watanzania kuwa Kodi hii si mpya bali wigo umeongezwa Ili wapangishaji wa nyumba binafsi wenye pato linaloanzia shilingi 500,000/= Kwa mwaka na kuendelea wamejumuishwa kwenye wigo wa Kodi kuanzia Julai mosi 2022.

Mwenye nyumba atapata cheti Cha Kodi ya zuio kama ushahidi wa malipo ya Kodi iliyolipwa kutokana na zuio la asilimia 10

Kwa maelekezo zaidi wasiliana nasi Kwa namba za bure;
0800-750075 au 0800-780078 au Whatsapp namba 0744-233333

"Pamoja tunajenga Taifa letu"

Imetolewa na;

IDARA YA HUDUMA NA ELIMU KWA MLIPAKODI
View attachment 2335063
Mtoa taarifa alipewa kazi TRA kwa kubebwa, alichoandika hapo hakieleweki utadhani mtoto wa darasa la kwanza?
 
Tanzania raha sana

Utasikia watu wakilalama kuhusu tozo, kodi lakini ukienda baa unakuta wamejaa
Wanaojaa Baa ni wangapi? na je umepita na kule kwenye draft na kahawa...mbona nako wapo wengi tu?.

Na kama Baa wapo wengi basi wakamueni hao hao maana uzembe wenu wa kuwatafuta waenda Baa na Mpirani mnakusanya mpaka wanaoshindia mihogo ya mia tatu kutwa nzima.

Sasa jiulize wewe Mtumishi wa TRA unaweza kula chai ya rangi au maji na mihogo ya mia mbili asubuhi ukaenda kazini?.
 
Back
Top Bottom