TRA-Tegeta wanahitaji pongezi kubwa sana kwa hatua hii

Jamal Akbar

JF-Expert Member
Oct 9, 2014
413
471
Kwa kipindi kirefu sasa, nchi yetu imekuwa ikitumia mabavu ili kuwafanya wananchi walipe kodi hasa wafanyabiashara wakubwa. Wazungu wanasema ili kupata "compliance" linapokuja suala la kukusanya kodi sisi kama nchi tulichagua njia ya mabavu (Coercive means) na ndio maana mambo kama task force yamekuwa yakirindima hasa kipinidi kilichopita cha utawala.

Lakini kwa mujibu wa wataalamu mbalimbali, kuota zawadi (rewarding) ni njia mojawapo ya kupandisha morali ya kufanya kazi ili kupata matokeo chanya.

Katika pitapita zangu nimekutana na tangazo toka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mkoa wa kikodi wa Tegeta ambalo linawahamasisha wananchi kudai risiti baada ya manunuzi ili kupata nafasi ya kujishindia kati ya 250,000 mpaka 1,000,000 katika bahati nasibu itakayofanyika mwisho wa mwezi.

Hili ni jambo kubwa na la kuigwa na linaakisi maono ya Rais Samia ya kukusanya kodi bila mabavu, kwani kwa mwananchi kudai risiti tayari serikali inapata mapato stahiki katika muamala uliofanyika. Kutoka zama za kutegeana njiani Kariakoo kunyang'anya wafanyabiashara mizigo yao kwa kukosa risiti, kutoka kujibanza kwenye vituo vya mafuta kuwavizia wasio na risiti hadi kuweka mfumo wa wananchi kujishindia pesa taslimu kwa kuwa na risiti halali, hakika TRA_Tegeta wameonesha mfano unaopaswa kuigwa na nchi nzima.

Wananzengo ninyi mnaonaje hatua hii ya TRA-Tegeta ambayo pia itaongeza Database ya wateja, tujadili hapa.

TRA.jpeg
 
Pongez gani.. ujinga ujinga unaita pongez
Wacha nikusamehe tu.

ูˆูŽู„ูŽู…ูŽู† ุตูŽุจูŽุฑูŽ ูˆูŽุบูŽููŽุฑูŽ ุฅูู†ู‘ูŽ ุฐูŽูฐู„ููƒูŽ ู„ูŽู…ูู†ู’ ุนูŽุฒู’ู…ู ูฑู„ู’ุฃูู…ููˆุฑู
 
hao jamaa ni wahuni watatafuta watu wao kazi hizo zitafanywa kwa vivuli vyao na pesa watapiga hatari
 
Kwani hizo risiti hua zinaonyesha jina la mlipa Kodi? Kama hazionyeshi watampataje mahindi wa Bahati na sibu? Au mtu yeyote anaweza kukusanya risiti zozote akapeleka?
 
Wacha nikusamehe tu.

ูˆูŽู„ูŽู…ูŽู† ุตูŽุจูŽุฑูŽ ูˆูŽุบูŽููŽุฑูŽ ุฅูู†ู‘ูŽ ุฐูŽูฐู„ููƒูŽ ู„ูŽู…ูู†ู’ ุนูŽุฒู’ู…ู ูฑู„ู’ุฃูู…ููˆุฑู
Ikiwa utafanya subrah na ukasamehe hakika hilo ni jambo kubwa sana linalotakikana na lililo zuri

Tafsiri isiyo sahihi
 
Wangesema tu wanaume watakaodai risiti kupewa Dawa za nguvu za kiume bure. Risiti zingegombewa na wanunuzi
 
Ni vizuri haijaanza kitaifa, hapo hata ikiwa na matokeo mabaya waziri atakemea na kulaani maisha yataendelea, ikiwa na matokeo mazuri wengine wataiga.
 
Wametibu jeraha kwa juu juu hawajatibu ugonjwa halisi..hakuna asiyependa kulipa kodi kupitia kipato chake.tatizo lipo namna wanavyokukadiria unaweza kufunga biashara ukaamua kubeti.

Kwa mfano unauza duka la vifaa vya shuleni.chukulia kwenye Kila bidhaa dukani kwako hakuna faida Zaidi ya mia tano .zote ni kuanzia mia tano kushuka chini.ikitokea umeuza rim paper cotton moja kwa shilingi 10000 itakupasa uandike risiti ya efd kwa mnunuaji.katika hiyo elfu unayoandika kwenye risiti TRA watakata asilimia yao kumi na nane.

Baada ya kukata hiyo asilimia yao usisahau ukigeuza kwenye tsh wanakiwa wamekata elfu moja na mia nane Huku wamekuachia elfu nane mia mbili.kwa mahesabu rahisi ukitoa faida yako na kodi ya TRA unajikuta kila bidhaa unayouza inaliwa mpaka mtaji wake.mwisho wa siku ndio kuanza kulalamika chuma ulete kumbe ni vijana wa kaisari unawafanyia kazi bila kujua

kwa ushauri wangu wa jioni ya leo .Watengeneze mazingira mazuri ya kulipa kodi kutokana na biashara husika ili muuzaji asione ugumu wa kulipa kodi
 
Wamefanya jambo la tofauti sana labda ni baada ya kuona mibunduki & mifaini ya kichawi haiwatishi watu
 
Back
Top Bottom