TRA Tanga, nihurumieni jamani

TRA Tanga, nihurumieni jamani

Hiyo elfu50, ni asilimia 10 ya pango ya mwaka mzima. Hapo bado cjaanza hata kutoa mapato yao
Na kisheria hiyo kodi ya pango anatakiwa kuilipa mwenye nyumba ila wanaku
Hiyo elfu50, ni asilimia 10 ya pango ya mwaka mzima. Hapo bado cjaanza hata kutoa mapato yao
Hiyo inatwa withholding tax na kisheria inatakiwa ilipwe na mwenye nyumba ila kwakuwa TRA inashindwa kuwabana wenye nyumba zigo linakuangukia mpangaji!!halafu wanakuambia eti nenda ukakae na mwenye nyumba akikubali atakurejeshea!!na ndio maana huwa wanataka uwapelekee mkataba wa upangishaji li wajue kodi unayolipa!!
 
Wakuu HV nikienda kuwaambia biashara imenishinda watanielewa kweli au bado watataka niwalipe nimekosa aman, hii nchi yetu jaman inakoendea mbona ....
Waandikie barua wasilisha kwao nawe uwe na copy ya kufunga biashara.
 
Wakuu HV nikienda kuwaambia biashara imenishinda watanielewa kweli au bado watataka niwalipe nimekosa aman, hii nchi yetu jaman inakoendea mbona ....
Waandikie barua kuwa biashara ni ngumu hauna uwezo wa kulipa kodi wanayoitaka watakupa miezi 3 ya kujaribu ikifika ukaona huwezi kulipa utaandika barua ya kufunga biashara
 
Yaani wanenipa tin, alafu wakaniambia nikalipe asilimia 10, ya Kofi yangu ya mwaka mzima. Nikalipa elfu hamsini hapo hata cjafungua, nikamwambia ndugu yangu cjaanza hata biashara yenyewe hii pesa mliyonikadilia ntaitoa wapi?, wakasema Dada hiyo ndo kima cha chini kwa wenye biashara ndogo. Niliondoka TRA huku machozi yananitoka nikakaa home siku3 sijafungua nawaza nifanyaje alafu nilipo nisehemu ambayo haijachangamka kabisaaaa.

500 000/- kwa mwaka ni kubwa sana!!
 
500 000/- kwa mwaka ni kubwa sana!!
Halipi 500,000/-. Analipa withholding tax ambayo ni 10% ya thamani ya pango la sehemu anayofanyia biashara hivyo atalipa 50,000/-.

Kodi hii inabidi uizuie(withhold) kutoka kwa mwenye nyumba yaani uumpe 450,000 badala ya 500,000 halafu hio 50,000 ndio uipeleke tra. Shida kubwa hamna mwenye nyumba anakubali
 
Wakuu HV nikienda kuwaambia biashara imenishinda watanielewa kweli au bado watataka niwalipe nimekosa aman, hii nchi yetu jaman inakoendea mbona ....
Dada kama biashara imeshindikana, imeshindikana, hakuna cha kuwalipa.
 
Kuna watu wawili wanaweza kukuelewa na kukusaidia!
1. Afisa elimu wa kodi yuko hapo ofisini.
2. Meneja wa mkoa!
Ni waelewa mno, nenda kwa meneja moja kwa moja umweleze haya uliyosema!
Ahsante Huyo meneja wa mkoa office yke IPO wapi au palepale TRA
 
Vitumbua nayo ni biashara kama biashara zingine, tatizo lako unaitazama kwa jicho la dharau ndio maana wengi wanabaki walipo,itakuwaje hapo baadae mtaji wako utakuwa mkubwa na unataka kuiendesha biashara yako kisasa ( Kwa mf:Omar Ndama Bites and Snacks) jambo linalohitaji ufuate taratibu za kiserikaliunadhani hapo TRA utawakwepea wapi?ndugu huyu hana budi kwenda TRA kama kuwaelezea kuwa anafunga biashara kama alivyokwenda kuwaambia anaanzisha biashara.Huo ni ushauri tu kukubali au kuukataa ni juu yake.
Nimekuelewa ndugu, ntaenda kuwaambia wanipunguzie kodi au wanipe hata miezi3 nifanye biashara sababu ndo naanza
 
Nenda waambie nimeshidwa kulipa hiyo kodi naona sitaimudu kulingana na aina ya biashara mtaji wake na gharama za uendeshaji, kwa hiyo umeamua kuifunga, pia ingekua vizuri ukaonana na meneja wa tawi au yule anaepitisha kiwango cha kodi kilichokadiriwa na maafisa wa chini yake unaweza kuongea nae ukamuomba akakupunguzia,
Angalizo, kama uliwaambia kua ushafungua biashara lazima uwalipe kwa kipindi ulichofanya biashara, kama ndivyo andika barua mapema ya kufunga biashara yako hata kama utakua hujalipa deni ili kukwepa deni kuongezeka kila mwezi.
Ndo naanza, nimeanza mwezi huu tar 5
 
Hapo cha kufanya ni rahisi tu hata mimi nilishakutana na hali hiyo!!unaandika barua kwa meneja wa tra mkoa kumjulisha kuwa umefunga biashara kutokana na sababu yoyote tu hivyo unamuomba hiyo TIN waisimamishe,utakapo taka kufungua biashara tena utawajulisha,unaandika barua mbili unaenda nazo zote watazigonga mihuri ya kuzipokea moja watakupatia kama kumbukumbu yako!!hiyo ndio ya kuitunza sana uhakikishe imegongwa mhuri wa received!!basi umemaliza ila sasa hujasema hiyo biashara ina muda gani kama kwani hapo kuna installment mbili za kikodi sept na dec!!kwa maelezo zaidi waweza PM,
Biashara nianza mwezi huu tar5, na natakiwa nilipe kodi ya mwaka mzima hata kama nimeanzia kati ya mwaka na nimepewa awamu mbili sept_dec
 
Biashara nianza mwezi huu tar5, na natakiwa nilipe kodi ya mwaka mzima hata kama nimeanzia kati ya mwaka na nimepewa awamu mbili sept_dec
Hapo kuna kodi aina mbili kwanza kuna withholding tax,ambayo ndio hiyo 10% ya rent ya pango kwa mwaka,hiyo ndio unatakiwa kuilipa kwa mwaka,kama mwenye nyumba wako ni muelewa mnaweza lipa nusu kwa nusu kwani ndiye alitakiwa kuilipa!!hiyo nyingine ni income tax amabayo ni makadilio utakayotakiwa kulipa !!ndio maana wamekufanyia awamu mbili badala ya nne kwa kuwa umeanzia katikati ya mwaka,jaribu tu ukiona umeshindwa andika barua ya kusimamisha biashara tu.
 
TRA ni jipu maana wanafanya makadirio makubwa mno, nadhani na wewe wamekupa makadirio ya 7,800,000 kipato cha mwaka kitu ambacho hakina uhalisia na mapato ya biashara yako
 
Dada jaribu kutafuta information kwa waelewa wa kodi. Hio ya 10% ni withholding tax kwenya pango, tena kuna additional 1% stamp duty. Hii anatakiwa alipe mwenye nyumba bahati mbaya tra wanatudai wapangaji inakera na kuumiza sana.
Umefafanua vyema. Inaonekana dhahiri dada hana taarifa na wala hajaelimishwa anachokilipia ni kitu gani.
 
Back
Top Bottom