Kibesenii
😀😀 ,jibu bwana,au mpaka kakobe akupe ruhusa?omba hata misukule wenzio wa akina justice kwanza wakusaidie, maana ndio mmekaririshwa neno "upumbavu"maneno yako mengi jamani sio hilo tu,mwambieni awafundishe kuwa watii wa mamlaka pia
warumi 13.,kibesenii sikuhizi ni mwanateknolijia.
Shetani naye anatumia maandiko, Mfano Mathayo 4: 5 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, 6 akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
andiko hilo shetani amelichukua katika Zaburi 91:11 Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote.
Kwahiyo wewe ni ajenti wa ibilisi, nawe umesimama kinyume na Kweli ya Neno la MUngu. ndiyo maana una ujasiri wa kuwanenea mabaya Watumishi wa Mungu kama Kakobe.
Maandiko yanaposema tuitii mamlaka, haimaanishi tutatii kila kitu hata kama kipo Kinyume na Neno la Mungu; Mfano, Shadraka na Meshaki na Abednego walikata amri ya Mfalme ya Kuabudu sana ambayo Nebukadreza aliisimamisha; Je waliitia mamlaka? jibu ni hapana; Je walifanya Dhambi? jibu ni hapana, ndiyo maana MUngu aliwaokoa hata baada ya kutupwa katika tanuru la Moto. Danieli 3:1-30; Danieli naye hali kadhalika, Danieli 6;
kwahiyo acha kupotosha maandiko. Hata mashoga na wasagaji hutumia Biblia kwa taarifa yako; wanasema Mungu alimwambia adamu nitakufanyia msaidizi wa kufanana nawe, wanasema mwanamke hafanani na mwanaume, ndyi hao wanaleta mambo ya ushoga. Kaa chini jifunze, acha kiburi.
Ifahamike kwamba maandiko hayafasiriwi kama apendavyo mtu fulani tu, 2 Petro 1:20 Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu.
hii ni ajabu, kwamba ukienda Chuo, unakubali kufundishwa History, Jiografia au Kemia, Lakini kwenye Biblia kila mtu anajifanya mwalimu; Kuna hukumu kubwa kwa walimu. Yakobo 3:1 Ndugu zangu, msiwe waalimu wengi, mkijua ya kuwa mtapata hukumu kubwa zaidi.
Neno la Mungu siyo kama hisabati, kwamba kila mtu atakuwa Mwalimu. Wewe umetoka huko kulewa kangara, unafanya uzinzi na uasherati, bado unataka uwe Mwalimu wa Neno la Mungu. Okoka kwanza, Mungu akupe uwezo wa kushinda dhambi ndipo uanze kufundisha Neno la Mungu.
Maandiko yanasema Kila alitajaye Jina la BWANA na auache uovu. 2 Timotheo 2:19 Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu.
Acha kwanza UOVU ndipo uanze kulitaja Jina la BWANA.