TRA mnataka kodi na kwenye sadaka?

TRA mnataka kodi na kwenye sadaka?

Joined
Dec 27, 2017
Posts
36
Reaction score
18
Commissioner wa TRA aliagiza kupitia vyombo vya habari kwenda kuchunguza ili kujua kanisa la FULL GOSPEL BIBLE FELLOWSHIP -lina miradi au Askofu Mkuu Zachary Kakobe kama ana miradi binafsi inayomwingizia kipato ili waweze kupata kodi.

Jumamosi ya tarehe 30/12/2017 barua kutoka TRA ilifika makao makuu ya kanisa FGBF -MWENGE DSM. Na jumanne ya tarehe 02/01/2018, kilitumwa kikosi kikiongozwa na afisa mmoja (.....) ambaye pia ndiye alitajwa kwenye barua kama kiongozi wa msafara.

Walipokelewa na kukawa na mahojiano yalichukua zaidi ya masaa sita. Maana waliingia saa sita kasoro mchana. Walitoa karatasi ilikuwa na listi ya maswali (Questionnaire). Upande wa kanisa alikuwepo Askofu mkuu Zachary Kakobe pamoja na viongozi wa kanisa. Zoezi liliendelea ikafikia maamuzi pia ya kutaka Bank Statements kutokea 2014 mpaka 31/12/2017 katika akaunti zote mbili. Moja ni akaunti ya kanisa la hapa DSM (FULL GOSPEL BIBLE FELLOWSHIP) na ya pili ni akaunti ya Kitaifa ya FULL GOSPEL BIBLE FELLOWSHIP. Pia wakataka akaunti binafsi ya askofu na mama mkuu, wakataka pia akaunti za watoto.

Wiki yote hiyo zoezi la kuangalia kupitia Bank Statements na rekodi za fedha katika akaunti za kanisa. Mwisho wa uchunguzi kama commissioner wa TRA alivyoagiza kuchunguza kama kanisa au Askofu Kakobe wana miradi nje ya sadaka.

Kikosi hicho chini ya Afisa wa TRA (......) baada ya uchunguzi kwa siku kadhaaa, walijiridhisha pasipo shaka kwamba kanisa la FGBF nchi nzima na Askofu Kakobe hawana miradi ambayo ndiyo hutozwa kodi.

Hivyo kiongozi wa msafara huo na kikosi chote walirejesha taarifa na kiongozi huyo akashauri mjadala huo ufungwe.

Kinyume chake baada tu ya huyo afisa kushauri kufungwa kwa mjadala, alipewa uhamisho wa ghafla kwenda mkoani. Na kuteuliwa Kiongozi mwingine na badhii ya maafisa kubadilishwa kwenye kikosi.

Mnamo jumanne 09/01/2018 kikosi kazi kipya. Kilifika kanisani. Kwa awamu walikuja kivingine. Mambo waliyokuja nayo ndiyo ambayo yametupa kujua kuna hila ndani yake.
Walifika wakauliza na kutaka zile bank statements za sadaka, wakapewa. Hawakuridhika. Wakaanza kukagua. Wakaingia kila ofisi kanisani hapo FGBF -Mwenge. Mbaya zaidi walienda nyumbani kwa Askofu Mkuu Zachary Kakobe Kijitonyama, wakapekua mabegi na kutoa nguo moja baada ya nyingine za askofu pamoja na za mama askofu Hellen Kakobe.

Wakachukua simu za mama askofu. Pia wamechukua computer za kanisa. Wakaanza kuhoji matumizi ya sadaka jinsi yanavyotumika.

Bodi ya wadhamini ya kanisa la FGBF walikaa kikao cha dharura alhamisi 11/01/2018, walieleza kila kitu kwamba katika sadaka hakuna matumizi yaliyotumika nje na imani yetu ambayo ni kuhubiri Injili pamoja na uendeshaji wa huduma kama taasisi. Lakini muhtasari na maelezo ya bodi ya wadhamini TRA hakuyapokea, sasa sijui wanataka uthibitisho gani na kutoka kwa nani kama wanakataa vielelezo vya bodi ya wadhamini!!?? Pia waliomba idadi ya washirika na rekodi zao za kutoa zaka na sadaka wakapewa maana kila kitu kiko wazi na kiko nuruni.

Jumamosi ya tarehe 13/01/2018 zililetwa barua ikimtaka Askofu Kakobe na mama wafike TRA -MWENGE leo Jumatatu wameitaka wito. Mnamo saa nne kasoro asubuhi leo jumatatu ya tar 15/01/2018 Askofu Mkuu Zachary Kakobe na mama askofu, bodi ya wadhamini na baadhi ya viongozi wa kanisa wamewasili TRA -Mwenge DSM.

Maswali ya kujiuliza, kama walikosa miradi ina maana wanatafuta kodi kwenye sadaka?? Na iweje wahoji juu uhalali wa matumizi ya fedha ya kanisa wakati bodi yenyewe haina tatizo juu ya hilo??

Mwisho nimalizie kwa kauli ya Askofu Kakobe aliyoitoa jana ibadani

"Shetani wa kuninyamazisha bado hajazaliwa, neno lolote Mungu atakalonipa nitasema kama lilivyo bila kupindisha, kwangu kifo ni promotion ya kwenda kukaa na Baba mbinguni, huwezi kunitishia kifo,nina miaka 62 nikifa leo nitakufa sawa na umri wa Petro na Paulo Mtume, ila nikifa ninapoenda wewe utakuja mbinguni ninakoenda?

Pichani, ni nyumba ya Askofu Kakobe na kibao cha mtaa Kijitonyama DSM

26734146_1244721932338795_4926151626821610731_n.jpg


26238986_1244722039005451_6732083576321121271_n.jpg
 
Hii serikali mbona inataka kuwa dharimu kama ya Roma
au wanafikiri humo kuna miladi imeanzishwa wapate Kodi..!?
Maana serikali yetu kiukweli kimapato inaendelea kushuka.
 
wakimaliza kwa tajiri wa kiroho... wakafutile na wale maaskofu na wanufaika wote wa esklow kama pesa zile zilikuwa sadaka... je walilipa kodi ?!...
 
Jamani nchi ,ni ya wananchi wote,ninaendeshwa na sheria na taratibu ,haiendeshwi kama mtu ananvyojitakia mwenyewe,makanisa na maeneo yote yanayofanya ibada yana utaratibu ,yanasimamiwa na mamlaka ya nchi chini ya sheria husika,TRA,wanafanya kazi chini ya tararibu na sheria husika,ukaguzi wanaofanya Tra,ni wakawaida pale wanapohisi kuna mapato ya serikali, nashangaa kakobe askofu wa siku nyingi tena amesoma kwa kiwango chake anashangaa kukaguliwa na vyombo vya serikali,yeye mwenyewe kakiri anapesa kuliko serikali na waziri anayetaka aende akamkopeshe,alitegemea nini? Serikali isiende kuchukua mapato yake?kama alikua anabeep safari hii namba ataisoma.
 
Jamani nchi ,ni ya wananchi wote,ninaendeshwa na sheria na taratibu ,haiendeshwi kama mtu ananvyojitakia mwenyewe,makanisa na maeneo yote yanayofanya ibada yana utaratibu ,yanasimamiwa na mamlaka ya nchi chini ya sheria husika,TRA,wanafanya kazi chini ya tararibu na sheria husika,ukaguzi wanaofanya Tra,ni wakawaida pale wanapohisi kuna mapato ya serikali, nashangaa kakobe askofu wa siku nyingi tena amesoma kwa kiwango chake anashangaa kukaguliwa na vyombo vya serikali,yeye mwenyewe kakiri anapesa kuliko serikali na waziri anayetaka aende akamkopeshe,alitegemea nini? Serikali isiende kuchukua mapato yake?kama alikua anabeep safari hii namba ataisoma.


Kama ni kukaguliwa amekaguliwa, Na report I katika kwamba Hana mradi wowote wa biashara, Hata parka Na pants hafugi, Yeye ni injili baasi, issue ni Baada ya kukaguliwa Na kuona hakuna kodi, Na aliyekabidhiwa kazi kutoa report yake, ghafula amehamishwa kazi Na kupelekwa mkoani, halafu amepewa kazi mtu mwingine, mbaya zaidi anaenda kukagua Nguo, anasalula moja moja eti anatafuta mradi wenye kodi ya serikali! Je hii ni TRA ? Au kuna hila ndani yake? Wanakagua sadaka zinatolewa kiasi gani? Na zinatumikaje, Sheria gani inaruhusi hili?? Na kama ni hivyo, basi wafanye kwenye makanisa yote Na misikiti yote, siyo kwa kakobe tu.
 
Jamani nchi ,ni ya wananchi wote,ninaendeshwa na sheria na taratibu ,haiendeshwi kama mtu ananvyojitakia mwenyewe,makanisa na maeneo yote yanayofanya ibada yana utaratibu ,yanasimamiwa na mamlaka ya nchi chini ya sheria husika,TRA,wanafanya kazi chini ya tararibu na sheria husika,ukaguzi wanaofanya Tra,ni wakawaida pale wanapohisi kuna mapato ya serikali, nashangaa kakobe askofu wa siku nyingi tena amesoma kwa kiwango chake anashangaa kukaguliwa na vyombo vya serikali,yeye mwenyewe kakiri anapesa kuliko serikali na waziri anayetaka aende akamkopeshe,alitegemea nini? Serikali isiende kuchukua mapato yake?kama alikua anabeep safari hii namba ataisoma.
Acha uongo. Kwahiyo kwenye hayo mabegi ya nguo ndo kunakuwa na miradi inayotakiwa kukatwa kodi.!?
 
Jamani nchi ,ni ya wananchi wote,ninaendeshwa na sheria na taratibu ,haiendeshwi kama mtu ananvyojitakia mwenyewe,makanisa na maeneo yote yanayofanya ibada yana utaratibu ,yanasimamiwa na mamlaka ya nchi chini ya sheria husika,TRA,wanafanya kazi chini ya tararibu na sheria husika,ukaguzi wanaofanya Tra,ni wakawaida pale wanapohisi kuna mapato ya serikali, nashangaa kakobe askofu wa siku nyingi tena amesoma kwa kiwango chake anashangaa kukaguliwa na vyombo vya serikali,yeye mwenyewe kakiri anapesa kuliko serikali na waziri anayetaka aende akamkopeshe,alitegemea nini? Serikali isiende kuchukua mapato yake?kama alikua anabeep safari hii namba ataisoma.
Sheria gani? TRA na kukagua nguo majumbani mwa watu imeanza lini?

Acha kujitoa ufahamu
 
Watu wanashangaa TRA kukagua hadi nguo zote nyumbani za familia yote.Ni kawaida sio matajiri wakubwa wote huweka pesa benki au kwenye miradi .Wengine utajiri wao huutumia kwenye mavazi.mfano unakuta mke ana chain ya almasi ya bilioni kadhaa au mkufu wa dhahabu wa kuvaa kiunoni au miguuni wa bilion kadhaa au ana nguo za bei ya mamilioni ya shilingi.Kule kusasambua masanduku ya nguo za kakobe ni kujhakikishia thamani ya hizo Mali zake ziwemo nguo zake za Ndani. MTU akisema yeye tajiri kuliko serikali Mali zake zote zikiwemo chupi inabidi zifanyiwe tathmini na TRA ili kupata jumla ya utajiri wake na wa familia yake una thamani ya shilingi ngapi .Kakobe kayataka akiambiwa usichanganye dini na siasa hasikii.TRA waacheni wafanye kazi mwisho watatoa ripoti. Unaweza kuta Kakobe ana SAA ya mikononi yenye thamani ya bilioni kadhaa. Na akawa MTU anayevaa SAA ya ghali kuliko MTU yeyote duniani.
 
Ndiyo Nyumba yake, aliijenga tangu miaka ya themanini; kwa gharama ya Milioni 2; kabla hajawa mtumishi wa Mungu; baada ya kuingia katika utumishi, maisha yake yote ameyatoa kwaajili ya huduma.
Duuuhh
 
nimegundua hiii nchi ili uishi kwa amani kama ni mtu mwenye status katika jamii mfano kiongozi mkubwa wa dini, mwanasiasa, msanii mkubwa, mfanyabiashara mkubwa n.k jitahidi sana kuwa mkimya, chunga kinywa chako, ishi kwa kufuata utaratibu, lipa kodi kama inavyostahili hakika utaishi kwa amani, mambo ya uanaharakati waachie wanasiasa.

hii awamu ni tofauti sana na awamu zilizopita, soma alama za nyakati
 
Hapo kodi sio tatatizo Bali kuikosoa serikali lakini ikumbukwe taasisi za kidini zipo kwa ajili ya jamii na pindi wanapoona kuna mambo hayaendi vizuri wana haki ya kusema lakini hapa tz mambo yanakuwa tofauti naamini wakitoka kwa kakobe wanaenda kwa gwajima.
 
Jamani nchi ,ni ya wananchi wote,ninaendeshwa na sheria na taratibu ,haiendeshwi kama mtu ananvyojitakia mwenyewe,makanisa na maeneo yote yanayofanya ibada yana utaratibu ,yanasimamiwa na mamlaka ya nchi chini ya sheria husika,TRA,wanafanya kazi chini ya tararibu na sheria husika,ukaguzi wanaofanya Tra,ni wakawaida pale wanapohisi kuna mapato ya serikali, nashangaa kakobe askofu wa siku nyingi tena amesoma kwa kiwango chake anashangaa kukaguliwa na vyombo vya serikali,yeye mwenyewe kakiri anapesa kuliko serikali na waziri anayetaka aende akamkopeshe,alitegemea nini? Serikali isiende kuchukua mapato yake?kama alikua anabeep safari hii namba ataisoma.
Hizi sheria za tiaraei zimeanza kufuatwa baada ya kuambia nanii atubu? hii ni janja janja janja yakutaka kunyamazisha watu wasihoji wala kukosoa hii sirikali ya maraika mtukufu.
 
Back
Top Bottom