TRA hii ni kodi au ni dhuluma?

TRA hii ni kodi au ni dhuluma?

Tatizo wafanyabiashara wengi hawana shule na hawatafuti maarifa ndo maana wanalalamika juu ya hii kodi...wewe uliesema cooperate tax? cooperate tax inalipwa na kampuni mbona...
Aliyesema "corporate tax" ni Kifaurongo siyo mimi. Hii inaitwa Kodi ya Zuio.
 
Last edited by a moderator:
Watanzania wengi mmezoea kutokufuata sheria. Hii kodi ipo kihalali, hizo ndio kazi za wabunge mliowachagua kama hamuitaki waende Bungeni wawawakilishe. Ni uhuni uliopitiliza kushindwa kulipa kodi ambayo ipo kisheria. Mimi nawaomba TRA wafuate sheria na kukusanya hii kodi kama ilivyo kwenye sheria tulizojiwekea. Wacheni kulalamika chin chini tumieni wabunge wenu kuiondoa kama hamtaki. TRA fanyeni kazi yenu hapa kazi tu!

Unajua maana ya withholding Tax, tuanzie hapo kwanza
 
Wanajamvi hii kodi ya zuwio (withholding tax) ipo kwa mujibu wa sheria na ni kweli anayebanwa kuilipa na TRA ni mpangaji na wengi hatulipi maana ni moja ya kodi zenye kero.
Ushauri:- 1.kodi ni kwa maendeleo ya Taifa hivyo TRA usichoke kutoa Elimu kwa wananchi ili waweze kuchangia maendeleo ya nchi yetu.
2.Kiwango cha kodi watu wengi wananalalamika ni kikubwa hivyo hebu viwango vipitiwe upya na ikiwezekana viwango vya kodi virekebishwe.[/QUOTE


Pia sheria inasema mikataba yote ya upangishaji ni lazima ilipiwe stamp duty TRA. Kwa hiyo TRA iweke itaratibu wa kuwashauri wapangaji walipie mikataba stamp duty na hapo mapato ya wenye nyumba yatajulikana na hivyo ni rahisi kuwafanyia makisio ya kodi na kuwafuata badala ya kuwasumbua wapangaji. Kwa watdioakaobughudhi wapangaji sheria ya ardhi ichukue mkondo wake.

Wenye nyumba za kupangisha wengi ukiacha NHC na mashirika ya hifadhi ya jamii ndiyo wakwepaji wakubwa wa kodi ya mapato. TRA wanafumbia macho kwa kuwa nao wana majumba na hawataki kulipa kodi na pia viongozi wengi wa umma kuanzia mawaziri, wabunge nk wanafahamu huu ukwepaji lakini kwa kuwa nao wanahusika wanaona ni sawa tu serikali kukosa mapato hayo.
 
Mkuu hii kodi inaitwa withholding tax, na withholding tax hii kwa tabia yake ni mpangaji anatakiwa kuikata kutoka ktk pesa utakayolipa kama pango alaf uiwakilishe tra kisha mpatia mwenye nyumba/frem copy ya kukiri malipo. Ukifanya tofauti inakula kwako.

Tatizo Kwa wafanyabiashara wengi tunaanza kufanya biashara bilakua na elimu pamoja na utaratib mzima wa kod zote zinazotuhusu ndo maana tukikutana na issues hata ndogo tu tunasumbuka.

Nashauri jarib kujifunza japo kwa kias kidogo kodi zote zikuhusuzo, na jinsi gani ya kukabiliana nazo.

Ukikata kodi hupati fremu. Ungemshauri zaidi kuhusu kulipia mkataba ushuru wa stempu ambao pia uko kwenye sheria hiyo ya withholding tax on rental income ili TRA wamfuate mwenye nyumba. Hii kodi haikusanyiki kwa wenye nyumba binafsi bila mgogoro na wapangaji.
 
Ni mfumo wa kipuuzi, mfumo ni wa kufumua huu
 
Kwa wale wafanyakazi wanajua kwamba kodi wanazotozwa kwa asilimia jinsi zilivyo ngumu na zinauma. Lakini kuna hii kodi tunayotozwa wafanyabishara kwa niaba ya wenye nyumba wetu naona wala siyo sahihi.

Mimi nimepanga kwa mtu nalipa laki mbili kwa mwezi, eti TRA wanataka mimi kwa kila laki mbili ninayolipa kama Pango, nikatwe asilimia kumi. Yaani natakiwa nilipe lakini mbili na elfu arobaini (240,000) kama Kodi ya zuio kwa kodi anayotakiwa kulipa mwenye nyumba wangu kwa mwaka.

Maelezo yao ni kwamba wewe mpangaji uende ukamdai mwenye nyumba wako kodi uliyokatwa na TRA. Swali langu wakati TRA wanajua wapi nilipopanga ni kwa nini wasitengeneze mfumo wa kupata hela yao ya kodi toka kwa mwenye nyumba wangu?

Iweje mimi nilazimishwe kulipa kodi kwa niaba ya mwenye nyumba wangu? Hivi kwa mazingira ya Tanzania ni rahisi kumwambia mwenye nyumba wako akurudishie kodi uliyokatwa na TRA?

Hii ni kodi nyingin tofauti na ile mpangaji analilpa kama withholding tax on rent?

Kwa kawaida, huwa kuna utaratibu kwa mpangaji kumlipia mwenye nyumba kwa kupeleka asiliami fulani ya kodi unayotoa kama kodi. Halafu unaambatanisha nakala ya risiti ya kodi na kodi anachukua mwenye nyumba. Kodi hii haipashwi ulipwa kwa gharama za mpangaji. Ila unakata kwenye gharama za pango, kisha unampa mwenye nyumba salio pamoja na risiti kwa kuw andiye anayepata mapato.

TRA kama wanafanya vinginevyo ni upumbavu na unyanyasaji wa raia usiokuwa na hta chembe ya akili. Mpangaji amemifunga mkanda kupata fedha za pango, halafu tena anaambiwa atafute na fedha za kumkopesha mwenye nyumba ambaye ki msingi ndiye anayepata mapato.

Hapa ni kukosa ubunifu au kutokujali na kuwaumiza binadamu. Kama wameshindwa kazi waondoke waje wenye akili hai wafanye kazi kwa haki na kweli.

Sioni sababu kwa nini wasizungmze na wamiliki wa majengo yote ya kibiashara. Watoe elimu ya kodi kwa hao wamiliki na kisha wawakomiti kulipa kodi, na kuwaambia kwamba kodi hiyo itakatwa kutoka fedha za pango wanazolipwa na wapangaji wao. Hii ni sheria ya nchi na wala si negotiable. Kwa kuwalinda wapangaji wasifukuzwa ama kupandishiwa kodi, wawa commit how wamiiki na wawape tahadhari juu ya madhara ya kuvunja sheria kwa kukwepa kulipa kodi halali.

Suala la kodi halipashwi kuwafany akwa hila ama vita. Ni suala la uzalendo na uwajibikaji kama tu kuna mazingira ya haki na kweli.
Siyo unadai wapangaji walipe kodi kuongeza mapato huku unakwepesha maelfu ya ma container bandarini. Nini hii kama si ungomvi na raia unaofanywa kufisha uharifu?
 
Wameamua kumkomesha magufuli na ccm maana amewanyima ulaji,chezea wa Tanzania,wanataka achukiwe kelele za kumkataa zianze,anatumbua majipu bila ganzi lazima waskiao maumivu watafute njia mbadala wa kupambana
Hahahaha

Wajua Bhana sie watanzania tuna vijimambo sana Hapa kuna tatizo ta kimfumo na kiutendaji sasa Viongozi wetu tulio wapa dhamana ya kukusanya kodi wame weka mfumo wao ila kuufanyia kazi hawawezi kiutendaji na hata kiubunifu mawazo yao yame gotea hapo hawawzi tena wao walikuwa ni kupanga deals tuuu na kutunyonya sasa inapotokea Changes na wana jua kabisa changes is inevitable wana na taka ku sabotage utaratibu ambao waliojipangia na wakauhalibu tayari sasa hawautaki urudi tena kwani ndio utakuwa mwisho wao wa kuchuma kirahisi.

My Take:

TRA wasipo kuja na utaratibu mpya katika kipindi hiki watajitia kitanzi kwanza patakuwepo na chuki kubwa saaana baina yao na walipa kodi wengine watatishiwa hadi maisha hii yote ni uzembe wa viongozi walioko TRA na walio kabidhiwa dhamana ya kuongoza taasisi nzima ya TRA kwani hawakuona mbele kutatokea nini

This is collator Damage na aihepukiki kabisasa ona mawazo yenu finyu kweli mimi naweza mfata Landlord wangu anirudishie hilo salio kweli mmekosa mfumo wa kufikiri nini kifanyike, Na kwenda kwenu huko ulaya miaka yote hamkuwa na research zozote au kuchunguza wenzenu wanakusanyaje kodi?

Msikurupuke hiyo style JPM atawatoa mkuku tena


 
Tabby ndiyo hiyo "with holding tax on rent" tatizo letu ni mfumo unaotumiwa kuipata hiyo kodi na kama Mpangaji atakuwa na ubavu wa kumdai mwenye nyumba baada ya kukatwa hiyo kodi na TRA?

Ingawa ng'adi lawi katoa mwanga wa njia gani itumike ili kuwalazimisha TRA kumdai mwenye nyumba badala ya Mpangaji. Ushauri wake ni vyema wapangaji wakaenda kusajili mikataba yao ya upangaji kwa kulipia "Stamp duty" TRA. Nadhani nitafanya hivi na kuwashauri na wapangaji wengine.
 
Last edited by a moderator:
Kwa wale wafanyakazi wanajua kwamba kodi wanazotozwa kwa asilimia jinsi zilivyo ngumu na zinauma. Lakini kuna hii kodi tunayotozwa wafanyabishara kwa niaba ya wenye nyumba wetu naona wala siyo sahihi.

Mimi nimepanga kwa mtu nalipa laki mbili kwa mwezi, eti TRA wanataka mimi kwa kila laki mbili ninayolipa kama Pango, nikatwe asilimia kumi. Yaani natakiwa nilipe lakini mbili na elfu arobaini (240,000) kama Kodi ya zuio kwa kodi anayotakiwa kulipa mwenye nyumba wangu kwa mwaka.

Maelezo yao ni kwamba wewe mpangaji uende ukamdai mwenye nyumba wako kodi uliyokatwa na TRA. Swali langu wakati TRA wanajua wapi nilipopanga ni kwa nini wasitengeneze mfumo wa kupata hela yao ya kodi toka kwa mwenye nyumba wangu?

Iweje mimi nilazimishwe kulipa kodi kwa niaba ya mwenye nyumba wangu? Hivi kwa mazingira ya Tanzania ni rahisi kumwambia mwenye nyumba wako akurudishie kodi uliyokatwa na TRA?

Hiyo kodi siyo burden kwako, inaitwa withholding tax, kwahyo wewe ni withholder, jukumju lako ni ku i withhold (kuizuia) kutoka kwenye pesa ya pango unayotakiwa kumlipa landlord wako, kwa mfano kama mkataba wa pango unasema ni laki nne utazuia 10% ya laki nne na utamlipa landlord TZS 360,000, na utampatia landlord wako withholding certificate kama udhibitisho wa malipo hayo ya kodi! narudia tena withholding tax siyo burden kwako.
 
Umeona eee, miaka 5 ijayo watakuwa wamemhujumu jpm vyakutosha
 
Hiyo kodi siyo burden kwako, inaitwa withholding tax, kwahyo wewe ni withholder, jukumju lako ni ku i withhold (kuizuia) kutoka kwenye pesa ya pango unayotakiwa kumlipa landlord wako, kwa mfano kama mkataba wa pango unasema ni laki nne utazuia 10% ya laki nne na utamlipa landlord TZS 360,000, na utampatia landlord wako withholding certificate kama udhibitisho wa malipo hayo ya kodi! narudia tena withholding tax siyo burden kwako.
Kwa mazingira ya Tanzania? Yaani kwa jinsi tunavyoishi kwa kubembeleza kwenye hizi nyumba tunamofanyia biashara halafu wewe unaongea kirahisi kwamba siyo mzigo kwetu? Yaani hawa wenye nyumba uwaambie umekata kodi yake kwa kuwa eti wewe ulikatwa kwa niaba yake na TRA, mtaelewana kweli!!?
 
Pia hii kodi ukifanya utafiti tra wanaipata kiasi kidogo kwa kujiondoa kuikusanya wao wenyewe ambapo hupelekea mikataba inayopelekwa tra kuwa tofauti na halisia ili kukwepa hiyo kodi. Ss kwa uvivu wao wa kuikusanya inapelekea kuleta usumbufu na pia kukusanya kiasi kidogo cha kodi kwa kudanganywa mikataba.
Pia wanakosa kodi kwa nyumba ambazo watu hawafanyi biashara za kuishi ambazo ni nyingi.
TRA badilikeni
 
Hii ni kodi ambayo MWENYE NYUMBA NDIO MSTAHIKI WA KULIPA ! na kwamwe si mpangaji! yeyote anaepokea kodi ya nyumba basi ni stahiki yake kulipa 10% ya kile anachokipokea kutoka kwa mpagnaji!

wenye nyumba wengi hawalipi hii kodi na inafanya kukosesha mapato serikali na wakati mwengine mpangaji anabebeshwa zigo ambalo si lake!

Hata unaponunua kiwanja yule muuzaji ndie anaetakiwa kukatwa 10% lakini mara nyingi mnunuzi hulipishwa zigo hili! kama wadau walivosema Elimu inahitajika hapa kwa wananchi wote ili watu wajue sharia inasemaje na nani anatakiwa kulipa nini!

Tatizo kubwa hapo awali watu hawakuona umuhimu wa kulipa kodi! kwa sababu nyngi ziliishia kwenye matumbo ya semina, warsha, makongamano! ila sasa hivi tunaona jinsi magufuli anavochakarika! ni wakati sisi wananchi kumuunga mkono kwa kulipa kodi kwa maendeleo ya nchi yetu kwa kuwa tumepata MKOMBOZI!
 
Aliyesema "corporate tax" ni Kifaurongo siyo mimi. Hii inaitwa Kodi ya Zuio.
a "

Ni kweli nashukuru kwa aliyeliona hilo kosa, sababu ya haraka ya kujibu, nilipaswa kuiita 'Withholding tax" lakini maudhui ni yaleyale.

Kwa kawaida mlipa kodi hii anapaswa kabla ya kumlipa aliyempa huduma kulipa pungufu akionyesha na kiasi cha kodi iliyolipwa au itakayolipwa TRA kama kodi ya zuio
 
Kwa wale wafanyakazi wanajua kwamba kodi wanazotozwa kwa asilimia jinsi zilivyo ngumu na zinauma. Lakini kuna hii kodi tunayotozwa wafanyabishara kwa niaba ya wenye nyumba wetu naona wala siyo sahihi.

Mimi nimepanga kwa mtu nalipa laki mbili kwa mwezi, eti TRA wanataka mimi kwa kila laki mbili ninayolipa kama Pango, nikatwe asilimia kumi. Yaani natakiwa nilipe lakini mbili na elfu arobaini (240,000) kama Kodi ya zuio kwa kodi anayotakiwa kulipa mwenye nyumba wangu kwa mwaka.

Maelezo yao ni kwamba wewe mpangaji uende ukamdai mwenye nyumba wako kodi uliyokatwa na TRA. Swali langu wakati TRA wanajua wapi nilipopanga ni kwa nini wasitengeneze mfumo wa kupata hela yao ya kodi toka kwa mwenye nyumba wangu?

Iweje mimi nilazimishwe kulipa kodi kwa niaba ya mwenye nyumba wangu? Hivi kwa mazingira ya Tanzania ni rahisi kumwambia mwenye nyumba wako akurudishie kodi uliyokatwa na TRA?

Umeandika jambo la maana sana mkuu,kinachofanyika hapa ni ubabe tu! Hakuna urafiki kati ya mlipa kodi na mamlaka ya mapato.Binafsi hili suala linaniumiza sana na linastaajabisha.
 
Back
Top Bottom