Top 5 ya urais 2015

Ndugu zangu, mie nashangaa huyu kiongozi wetu wa sisiemu ambaye ameshuhudia uozo na ubakaji wa democrasia ndani ya chama chake katika chaguzi ambazio zimeendeshwa kwa rushwa na ushirikina kwani imeelezwa kwamba wengine walivaa hilizi kulinda nafasi wanazoziomba katika jumuia za chama, na amewaacha wakaendelea na ushindi wao wa haramu anaitakia mema sisiemu, mimi nathani anataka kuingia katika Historia ya Rais aliyefiwa na chama chake. Ningekuwa mimi kwa gharama yoyote ningefuta chaguzi zote na kuanza upya.
 
1.Lusinde a.k.a Kibajaji
2.Mwigulu Lameck Nchemba
3.Mangare Shibuda
4.Nape Nnauye
5Steven Massatu Wassira.
 
Hii nchi ilipofikia inahitaji kiongozi strong na mwenye mamlaka na aliyazaliwa kuwa kiongozi
siyo uongozi wa kulazimisha.Mpaka nimefikia umri huu mtu ambae nilimuona kuwa alizaliwa
kuwa kiongozi alikuwa J.K.Nyerere,na mwingine ambae bado yupo hai kwenye hili taifa ni
Dr W.Slaa.Either ukubali au ukae ukweli ni huo.
 
T.2015 CCM, unasema kuna sharti la mtu kuwa na Degree ili kugombea uraisi?ni Kifungu gani hicho cha katiba kinachomtaka mtu awe na degree moja ili awe mgombea uraisi naomba nisaidie ndugu wewe wa CCM.
 
Dr slaa, dr magufuli. Waliobaki hawataiweza nchi iliyooza ya Tanzania. Tumuunge mkono dr slaa aingoze tz na tuombe sana prof Lipumbe,magufuli,lisu,mwakyembe,zitto,mnyika, wachaguliwe kuwa mawaziri wa serikali iyo. Pia inafaa sana lowasa akawa katibu mkuu wizara ya ulinzi akawajibika kwa waziri wa ulinzi na idara ya usalama wa taifa ndg mabere marando. Hapa tunaweza kuwa na taifa la maendeleo makubwa. Tofauti na apo dr slaa au rais yeyote ajaye akiendekeza udini,ukabila au makundi ya vyama,kamwe taifa la tz litabaki duni. Kura yangu nitampa dr slaa kwa sharti la muundo wa mchanyato huo!
 
1.Arfi.
2. Chagulani.
3. Habibu
4. Zitto
5. Mtoi
 
rais ni taasisi nyeti sana ya nchi. haiwezekani watu waigombee namna hiyo! Mungu atupe kiongozi anayetufaa ambaye sio kati ya hao ambao tunawaona wanajipanga kuingia ikulu kwa nguvu zao zote! ikulu sio pa kukimbilia namna hiyo!
Mungu IBARIKI TZ...
 
Hebu tujiulize walioteuliwa na vyama vyao kugombea URAIS kuanzia kwa Mzee wetu Mwinyi, wale wa mwaka 1995, akina Mkapa, Cheyo, Mrema, Lipumba,..., wale wa mwaka 2000, akina Mkapa, Lipumba, Mrema,...., wale wa mwaka 2005, akina Kikwete, Mbowe, Lipumba,..., wale wa mwaka 2010, akina Kikwete, Dr Slaa, Lipumba tena,..., ni vigezo gani vilitumika kuwateua ili tuviepuke na kuwaepuka wagombea hawa ambao kwa maoni yangu hawatufai kwa taabu na shida tulizonazo nchi hii.
 
Mimi ningempa Yoyote tofauti no:2-3


 

Jamani tuache utani, Magufuli hawezi kuwa raisi wa maana....mbona tunaendelea kubahatisha!!!

Kiukweli..kwa sasa TZ hakuna mtu anaetakiwa kuiongoza nchi hii kama tunaipenda kweli kama DR Slaa!!
 
ukabila si kigezo cha kuchaguliwa kuwa rais ingelikuwa ni hivyo basi rais angetokea usukumani
 
zotto kabwe umemsahau nini maana yule kijana ni jembe hakuna mfano.
 
Magufuli anafaa kupokea order na kuitekeleza. Ila yeye hafai kua rais! Muondoe.


Umenikumbusha the Peter's Principle. Magufuli will have risen to his highest level of incompetence.
 
Nchi hii ina ugonjwa wa uchumi na utawala bora ajira afya uadilifu.mtu anaefaa ni profesa lipumba.atweka sawa uchumi.kuhusu utawala ataunda serikali ya umoja wa kitaifa,kutoka vyama aavyote,ajira na afya itakuja baada ya uchumi kukaa sawa kwakua na serikali ya umoja uadilifu ni automatic.mtu huyu kazisaidia chi nyingi kupitia umoja wa mataifa.kwa hiyo hao wote uliowataja watapewa majukumu ndani ya serikali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…