Top 5 ya nyimbo za kumuombeleza Magufuli

Hizi nyimbo tano ndio zimekua bora kabisa kwangu zimetufariji sana kipindi cha maombolezo ya mpendwa wetu shujaa wa Afrika,jembe John Pombe Magufuli.

1.Bye Bye-Aslay

hii kali sana anavyoanza na ile mwana chatoo ehhh,mwana chato eeehhhh

wasalimie nyerere na karume,sefu

kufa usifiwe,ishi uzomeweeeeee

2.Ahsante Magufuli-Konde Gang

hawa wamepiga songi moja kali sana linafariji ukisikiliza machozi yanalenga unaona kama magu atafufuka asikie ahsante anazopewa

hongera kwa harmonize

3.Lala Magufuli-Diamond Platnumz ft Artist

hawa akina chege na chawa wote wa WCB wamepiga songi ila wamepigwa KO na harmonize,ingawa songi yao nayo kali hasa verse ya darasa na chorus ya Diamond ile

wametufariji sana

4.Magufuli-Peter Msechu

huyu bwana suala la msiba ni kama alilichukulia personally,kapiga ile remix ya wimbo wanapigaga misibani wa kinigeria ule bwana kauchapa kimagufuli umetoka vizuri sana

zile vocal zake kapanda na kushuka vizuri sana jamaa mwili wake na sauti havifanani kabisa

jamaa ni clone ya mzee John Komba

5.Kifo-RayVanny

kijana kaua sana na ile sauti yake ya kulia lia ni kama alikua anasubiri tu msiba ufike tujue kipaji chake

Na wewe weka top 5 yako au ongeza hapo

Bado tunaendeleza maombolezo ya siku 21,leo ni siku ya 16 hivi....
Uchafu MTUPU
 
Back
Top Bottom