Mr Q,
Unajua Mturuki si Mzungu na si Mwaarabu. Ila kwa historia, wamekaa karibu na watu wa Europe kuliko wa Asia. Hata ukimwangalia Father of Nation wa Turkey - ATATURK, kakaa zaidi ki-Europe. Kwa sababu hiyo, tabia za watu wa Istanbul zipo zaidi ki-Ulaya na si ki-Asia. Ndiyo maana hata timu zao za Mpira kama Galatasaray wakipambana na Basiktas, zinapigwa kwelikweli mtaani kama sijui wamekutana Hooligans wa UK.
Waturuki ni wafanya biashara wazuri sana na mfano mzuri ni Mahoteli ya Kitalii, shirika lao la ndege Turkish Air, Viwanda vya Electronics na funga kazi ni Viwanda vya nguo. Ni wachapa kazi na wana technology ya juu mno kwa sasa. Kama wangeliingizwa Europen Union na kuanza kufanya kazi kwa Standard za juu za EU, basi wangelibadilika haraka na kuwa ni moja ya nchi nzuri sana ndani ya EU. Pia kinawasaidia kwamba, wengi wao wako nchi za West kama akina Ozil wa Arsenal ambaye ni Mgeruman. German wapo Waturuki wengi mno. Pia mtu kama CEO wa Coca-cola ambaye na yeye ni Nusu Mturuki. Ukiongeza na MAFIA ya Waturuki, jamaa wana hela yao nzuri sana.
Kwa kusema hayo, inabidi nimalizie kuwa, inapokuja kuvuta watalii, jamaa hawajambo. Huo msikiti peke yake unaingiza fedha nyingi sana. Inadaiwa kuwa kuna sehemu hadi leo misa zinafanyika na huko nafikiri ndiyo unavua viatu ila kuna sehemu pamewekwa kwa sasa kama sehemu ya watalii kutembea (UNESCO) na nafikiri hata wao hawawezi kupagusa bila kuomba kibali cha Unesco hata kama ni matengenezo. Ila wao ndiyo wanafaidika kwa kuwa ni Official sehemu ya kihistoria na hivyo watalii ni wengi sana.
Mturuki wa Istanbul kwa sasa yupo Europe na mbali na ASIA. Sidhani huko hata hizi mila za kuoa Bikira wanazifuata kwa sababu nilishakutana na Mabinti wengi wa Istanbul wakijirusha na Wanaume na kupata Bange na Pombe kwa wingi sana.