TECNO Tanzania
Senior Member
- Jul 6, 2016
- 192
- 217
Baada ya uvumi wa mda mrefu sasa Kampuni ya TECNO tume wafikishia wateja wetu toleo letu la POP 7. Hivyo basi kwa Watanzania wote ambao wanataka kumiliki simu kali ya kijanja kwa bei poa kapisa tunasema POP 7 ndo mkombozi wa bajeti zao.
Toleo hili la POP 7 sasa linapatikana nchi nzima kwenye maduka yetu yote. Hivyo basi kwa yule mpendwa wako anaetaka kumiliki simu janja (smartphone) kwa mara ya kwanza unaweza kumwambia POP 7 inapatikana nchi nzima.
Simu hii imekuja na sifa bora zaidi katika mtiririko wa POP. Na ndio maana tumekuja na Slogan inayosema ‘’Amini katika Ubora’’ maana mabadiliko makubwa yamefanyika katika POP 7.
STORAGE
Storage ndo mpango mzima kwenye toleo hili la POP 7 maana toleo hili lina uwezo wa RAM ya 4GB ambayo unaweza kuiongezea 3GB (Memory Fusion) mpaka kufika 7GB RAM. Na ina uhifadhi wa kawaida ROM ya 32GB & 64GB.
CAMERA
Kwenye upande wa kamera POP 7 imekuja na camera nzuri ambayo kwa mtumiaji wa simu hii anaweza kuchukua kumbukumbu nzuri azitakazo. Kamera ya mbele ikiwa na 5MP na kamera ya nyuma ikiwa na 13MP + QVGA with Dual Flash.
BATTERY
Simu hii ina betri lenye uwezo mkubwa sana wa kutunza chaji ambalo lina 5000mAh hivyo basi litamuwezesha mtumiaji kutumia simu yake kwa muda mrefu bila kupata usumbufu wa chaji. Lakini pia jambo zuri ni kwamba toleo hili litakuwa linatumia chaji za Type ‘C’.
DISPLAY
POP 7 ina kioo kipana chenye inchi 6.6 HD ambacho umuwezesha mtumiaji kutumia na kuangalia taarifa mbalimbali vizuri bila shida yoyote.
SECURITY
Sasa utapata ulinzi bora kabisa kwenye toleo la POP 7 maana limekuja na njia mbili nufaika, ambapo mtumiaji utaweza kufungua simu yako kwa na njia ya Uso (Face Unclock) au kwa alama ya kidole kwa nyuma (Fingerprint). Fungua simu yako kwa haraka zaidi kwa kutumia toleo la POP 7.
TECNO POP 7 Pro kwa sasa inapatikana kwenye maduka yetu kwa shilingi 250,000/= tu za Kitanzania. Tunasema PESA KIDOGO UBORA ZAIDI.
Kwa maelezo zaidi piga namba; 0744 545 254 au 0678 035 208.