Tofauti ya JKT na JKU ni nini?

Tofauti ya JKT na JKU ni nini?

Samahani hivi naweza kujua tofauti ya JKT na jku na mishaara yao kwa mwenye uzoefu
Kifupi hakuna tofauti yoyote, ni kitu kile kile isipokuwa katika muungano, kuna majeshi na vyombo vya ulinzi ambavyo kisheria ni vya muungano na kuna majeshi na vyombo vya ulinzi ambavyo siyo vya muungano.

Majeshi na vyombo vya ulinzi ambavyo ni vya muungano ni JWTZ, Police na Magereza nk kama sikosei.

Lakini kule Zanzibar kuna vyombo vya ulinzi ambavyo si vya muungano ambavyo ni hiyo JKU,KMKM,Valantia nk.

Wale wa Muungano wao hutamba kote kote, anaweza kuhamishwa bara kwenda Zanzibar and vice versa na wasio wa muungano huhudumu eneo moja la muungano kutegemea upande alipo.


Hapa nimejibu kifupi, kama kutoa mwanga kwa sababu sijakariri sana taasisi za muungano na zisizo za muungano.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom