Uwezo mdogo kwa mtu kusema zamani lilikuwa chuo Cha kati ila sio Sasa?
Bila kuonyesha vigezo vipi vilivyopungua au kuongezeka.
Zipi hasa ni sifa za chuo kikuu, higher learning institution na College?
Unataka udemote tu, kwa hisia na bla bla zisizo na mashiko.
Hayo ya Zamani yanatoka wapi afu kumbuka nilichallenge orodha yako na sio kwamba zilikuwa Opinions zangu
Sasa iko hivi Hapa Tanzania kuna Vyuo vikuu ambavyo humo ndani kuna Vyuo vikuu kamili, na Vyuo vikuu vishiriki na hivi kwa kwa mujibu wa TCU viko 50 tu nchi nzima na vyote hivyo ni vyuo vikuu
Mfano
DUCE
MuCE
CUHAS
UDSM
St francis
Stella Marris
AMUCTA
UDSM
RUCU
SUA
SUZA
MWECAU
Hivi vyote ni Vyuo Vikuu na viko chini ya TCU/Tume ya Vyuo vikuu
NA kuna Taasisi za elimu ya Juu HLIs
NIT
CBE
IFM
ISW
DIT
MIPANGO
TIA Etc. HAwa wako regulated under NACTVET na hizi taasisi/ wengi tunaita tu vyuo maana kiswahili hakijitoshelezi misamiati vizuri huwa viko chini ya Wizara kama Fedha na Mipango, Sijui Maendeleo ya Jamii etc
Na mara nyingi vimefocus katika kutoa elimu ya aina moja tu utakuta kama ni Uchumi/Biashara/Fedha, Technlojia/ubunifu, Ustawi/maendeleo ya jamii au madini na utakuwa wanakuwa na Certificate hadi Degree!!
Hawa mfumk wao wa elimj pia wanaanza level 4 hadi 8 ikiwa na maana ni Degree
Vyuo vya KATi hakuna chuo cha kati kinachotoa Degree akuna kabisa wao ni Certificate/Diploma na level 4 hadi 6! Na hawa pia wako chini ya NACTVET
Ndio akina Lugalo, Kibaha, KAM, Nkinga, Butimba, Kreluu etc
NOte CBE kuwa ni college of Business haimaanishi ni chuo cha kati ile ni taasisi tu ya elimu ya Juu (labda kama miaka ya nyuma ilikuwa chuo cha kati) ila kwa sasa hiyo ni HLI
Kama na hapa hatutaelewana basi mkuu itabidi mjadala uishie hapa na tukubaliane kutoelewana