Nimependa huu uchambuzi kwani mwandishi bila kukusudia ametujuza sifa nyingi za mzee wasira
1. Kwanza kukubalika kwake na raisi aliyeko madarakani na kwamba anamtegemea sana katika ushauri, hii ni sifa njema
2. Kumbe viongozi kutoka lwao wanamkubali pia tofauti na baadhi ya wagombea wengine ambao wanatoka sehemu wasizoungwa mkongo
3. Mwandishi kama waliowengine wanakisa uchafu wa kumwagia mzee wasira matokeo yake ni kuzisha eti ufisadi, ubabe..rushwa vitu ambavyo mzee wasira hajawahi kutuhumiwa, mEe wasira amekuwa na msimamo thabiti juu ya mambo ya msingi ya kitaifa na kwa misimamo hiyo ameonekana kama mbabe, lakini utaakajr kimywa kama mtu anamtukana mwalimu nyerere na kukebehi muungano wetu??? Lakini pia amekuwa akijibu hoja kwa hoja na mara zote alipoamua kutetea jambo hata wapinzani huridhika maaana huwapa ukweli
4. Suala la kuhamia upinzani sio jambo la ajabu ndio maana ya demokrasia ya vyama vingi, uamuzi wa mzee wasira kwenda upinzani ulisukumwa na wanamchi ambao walimhitaji yeye kuwaongoza baada ya kumshinda mzee warioba kura za maoni lakini chama kikamteua mzee warioba badala yake kugombea kinyume na matakwa ya wananchi, baada ya kutafuta haki kwenye chama na kushindwa alikubali kushindwa ndipo wananchi wakamfuata na kutishia kufanya vurugu endapo hatagombea ndipo aliingia upinzani kwa ajiri ya kutetea haki yake na ya wananchi wanaomtaka ndio maana alipoenda upinzani alimshinda mzee warioba pamoja na kwamba upinzani haukuwa na nguvu wakati huo, baada ya kushindwa mzee warioba alikata rufaa na baadae uchaguzi kufutwa na wote kusimamishwa kutogombea, na lazima ijulikane wakati huo warioba alikuwa ndio waziri mkuu na mwalimu nyerere alikuwepo, badae mzee wasira alirudi ccm na kujisagisha ndani ya chama na kuendelea kukijenga mpaka leo.
Tokea hapo mzee wasira amekuwa akishika nyazifa mbalimbali serikalini na kwenye chama chake. Na kuonyesha kwamba ccm wanamtambua na kuheshimu demokrasia ndio maana kwenye uchaguzi wa halmashauri kuu mzee wasira aliongoza kwa kura nyingi alizopigiwa na wanaccm nankuibuka namba 1.
5. Wapo watu wachache sana wanompigia debe mzee wasira tofauti na watu wengine wanaoamini ni lazima watakuwa mataisi nchi by any means, mzee wasira anauzwa na sifa zake sio na wapiga debe wenye njaa na wanaotaka kuvuna pesa....
Nchi yetu ilipo inahitaji mtu mwenye sifa ya kuuelewa uchumi wa kimaendeleo, mtu anayehishimu maadili ya nchi, mtu mwenye msimamo wenye tija kwa nchi yake, mtu mwenye hekima na muadilifu mtu anayeweza kuleta umoja wa kitaifa na kuulinda muungano na mtu mwenye sifa hizi ni STEVEN MASATU WASIRA..