Tigo sasa mnakeraa kwa hili

Tigo sasa mnakeraa kwa hili

kichuminyi

JF-Expert Member
Joined
Mar 4, 2014
Posts
234
Reaction score
173
Jana saa 2 asubuhi nilinunua umeme kwa tigo pesa lkn nilikaa zaidi ya dk 20 sikupata token, nilipo wapigia wakadai muda si mrefu watatuma. Nikaamua kujaribu kwa Airtel money nashukuru Mungu ndani ya dk nikapata umeme.
Sasa hawa tigo toka jana saa 2 asubuhi mpaka sasa hivi hamna cha umeme na hela yangu wameichukua kurudisha hawataki. HUU KWELI NI UUNGWANA? Kama kuna tatizo kati yao na Tanesco kwa nini wachukue hela ya mteja? Si warudishe , nitoe hela ninunue kwingine.
Huku sio kurahisisha ni kukerehesha.
Ndio maana jina la hii kampuni ikapewa wale wagawa .....
JIREKEBISHENI.
Sirudii tena
 
Mkuu, jaribu kutembelea tanesco iliyokaribu nawe, kuna namba zipo kwenye mbao zao za matangazo, yaan kama umenunua umeme kwa njia ya cm kama we, kama token hazijatumwa, ukipiga hiyo namba wanakusomea on the spot
 
mi nliwahi kununua umeme nkapata meseji baada ya wiki mbili..hapana chezea hawa jamaa
 
Namba yao ya kuwapigia Tanesco; 0784 768584. Lakini muda wote ipo buys na hata ukiwapata watakuambia usubiri tu utatumiwa,mie nimechoka mwenyewe kuwapigia pigia maana nilinunua umeme toka tarehe 28/4 hadi leo bado.
 
Kwanza pole sana ila tatizo ni tigo wenyewe na siyo Tanesco cha msingi ukipata tatizo unaliga Simu maalumu ya Tanesco ila kama hauna Namba yao hata Namba ya imegencey ya kanda yako pia watakusaidia cha kufanya na utapata uduma bila shida.
 
Namba yao ya kuwapigia Tanesco; 0784 768584. Lakini muda wote ipo buys na hata ukiwapata watakuambia usubiri tu utatumiwa,mie nimechoka mwenyewe kuwapigia pigia maana nilinunua umeme toka tarehe 28/4 hadi leo bado.
Asante ngoja nijaribu
 
Sasa hivi mimi naenda kununua kwenye Ofisi za Tanesco.
 
Mi imenitokea ivyo,,,nimenunua kwa voda nimefanikiwa
 
Wapigie watakurudishia pesa, mimi nilikaa more than 24Hrs nikawapigia wakarudisha
 
Nikusaidie mdau sasa usiende moja moja lipia luku,bali nenda namba tatu kupata majina ya kampuni chagua namba mbili luku fuata maelekezo ukishamaliza papo hapo utapata sms
 
Katika mtandao uliokuwa bora kabisa kwenye swala la kununua Umeme,tiGO ilikuwa namba moja. Ulikuwa ukinunua umeme kama kuna shida ya mtandao ndani ya dk 3 unarudishiwa hela yako papo hapo,na hapa ulikuwa unatumia Menu ya tiGO Pesa namba 4-lipia bill yako then namba moja kununua Luku,but baada ya kubadili na kuwa namba 4-malipo kisha namba 3-kupata majina ya kampuni hapa ndipo tatizo lilipoanzia,ukinunua umeme tuu either umeliwa au umelala giza.
 
Mkuu, jaribu kutembelea tanesco iliyokaribu nawe, kuna namba zipo kwenye mbao zao za matangazo, yaan kama umenunua umeme kwa njia ya cm kama we, kama token hazijatumwa, ukipiga hiyo namba wanakusomea on the spot
Mkkuu ungetusaidia kutuwekea hizo namba maana wengi tumeliwa pesa bila token hasa wakati ule wa matatizo ya mtandao pesa zilkwenda bila tokeni labda tungejua tungeziokoa
 
Back
Top Bottom