Tigo ni Wasumbufu Sana

Tigo ni Wasumbufu Sana

Watairudisha kama ndo tabia yao
Litafika hadi kwa Waziri ohooo
wezi sana hawa jamaa!

na kuna siku nyingine niligombana nao sana

nimenunua kifurushi cha sms cha mwezi nikawa na chat na shemeji yenu, cha kuskitisha baada ya kutuma sms kama 10 hivi , nikaona sms zinagoma

nikijaribu kutuma kwenda namba nyingine zinaenda, ikabidi niwapigie tigo kuwaeleza lile tatizo

walichonijibu , nikaona kweli hii kampuni hamna kitu kabisa

wakanambia sitakiwi kutuma sms nyingi kwenda kwenye namba moja

nikawauliza mnanipangia matumizi? kama ndio hivyo toeni elimu kwa wateja wenu wooote kwamba kifurushi chenu cha sms kina masharti kadhaa wa kadhaa ili mtu aamue ajiunge au asijiunge

sio mnakimbilia tu kukata pesa halafu unakuja kumpangia mtu matokeo, niligombana nao sana mwisho wakaja kuniachia nitume sms kama kawaida

kama kuna mfanyakazi wa tigo humu jukwaani wasilisha haya malalamikowaambie tumeshaanza kuwaandika majukwaani

sasa wasipokuwa makini tutafungua jukwaa special kwa ajili yao maana kero zimekuwa nyingi na hamzifanyii kazi
 
Back
Top Bottom