Mwl
gfsonwin! Nami nimekuwa nikijiuliza maswali kama yako kuhusu huduma ya Ngwajima! Maan kimsingi kujenga kanisa kungemsaidia sana kutulia sehemu moja maana hata hapo TP mwaka huu ataondolewa maana ni eneo la NSSF kama sio NHC.. wanataraji kuanza mradi wa ujenzi wa nyumba za kisasa!
Bila shaka katika hili Gwajima ana tatizo kwenye huduma yake maana ata kiafya pale si salama kwa waumini maana vumbi na jua kali..mtu anaweza kuugua akafikiri ana mapepo kumbe ni mazingira!....
Mi nafikiri hili ndio tatizo kuu la huduma ya Ngwajima maana hana makazi maalum na cha kushangaza ana magari na kila kitu lakini nashindwa kuelewa kwanini wana shindwa kununua mahekari huko nje ya mji wakajenga kanisa maana sadaka anapata za kutosha!
Na moja ya sifa ya waumu wa Ngwajima wanauwezo wa kumfata kila atakapo kwenda ..kwa hiyo hata akijenga huko nje ya mji watakwenda na uzuri wana magari ya kuwachukua waumini!
Katika hili Ngwajima ana nishangaza,pengine tutapata majibu maana waumini wake wapo humu wengi.