Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,564
- 2,483
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umewakutanisha wanahabari 150 kutoka maeneo mbalimbali nchi ili kuwawezesha kuelewa sheria za uchaguzi,maadili ya kazi,usalama kazini na wajibu wao katika kulinda haki za binadamu kipindi cha uchaguzi mkuu ujao wa Oktoba 2025.
Akizungumza Mei 2,2025 wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika Jijini Dar es salaam Mratibu wa THRDC Wakili Onesmo Olengurumwa,amesema ni muhimu wanahabari wakapewa maarifa ya kisheria ili waweze kuripoti habari za uchaguzi kwa weledi,usalama na bila upendeleo.
Aidha ametoa wito kwa vyama vya siasa,taasisi binafsi,serikali na wadau wengine wa uchaguzi kufanya majadiliano ya kitaifa kuhusu mageuzi ya mfumo wa uchaguzi ili kupunguza malalamiko hasa kutoka kwa vyama vya upinzani kuhusu kutokuwepo kwa usawa na uaminifu katika mchakato wa uchaguzi.
Mafunzo hayo ambayo pia ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yanayofanyika kila ifikapo Mei 3,yamewaelekeza wanahabari namna ya kuzingatia taratibu za usalama wao binafsi,panoja na uandishi wenye uwajibikaji na kuheshimu kanuni za kitaaluma wakati wa kuripoti kampeni,upigaji kura na matokeo ya uchaguzi.
Source: Safari media
Akizungumza Mei 2,2025 wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika Jijini Dar es salaam Mratibu wa THRDC Wakili Onesmo Olengurumwa,amesema ni muhimu wanahabari wakapewa maarifa ya kisheria ili waweze kuripoti habari za uchaguzi kwa weledi,usalama na bila upendeleo.
Aidha ametoa wito kwa vyama vya siasa,taasisi binafsi,serikali na wadau wengine wa uchaguzi kufanya majadiliano ya kitaifa kuhusu mageuzi ya mfumo wa uchaguzi ili kupunguza malalamiko hasa kutoka kwa vyama vya upinzani kuhusu kutokuwepo kwa usawa na uaminifu katika mchakato wa uchaguzi.
Mafunzo hayo ambayo pia ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yanayofanyika kila ifikapo Mei 3,yamewaelekeza wanahabari namna ya kuzingatia taratibu za usalama wao binafsi,panoja na uandishi wenye uwajibikaji na kuheshimu kanuni za kitaaluma wakati wa kuripoti kampeni,upigaji kura na matokeo ya uchaguzi.
Source: Safari media