Mimi mwenyewe kila kikianza tu huwa nahepa nahamia kwingine
Wanataka kuonyesha kuwa wanajua kiingereza, hamna sababu nyingine
Habari wana-JF.
Mimi naomba kuuliza kipindi hiki cha TBC cha "This Week in Perspective" kinachorushwa kila Ijumaa kuanzia saa 3:30 usiku mpaka saa 4:00 usiku kinamlenga nani hasa kwani watanzania wengi ambao kodi zao ndio zinatumika kuendesha kituo hiki hawaelewi vizuri lugha ya kingereza inayotumika katika kipindi hiki.Hivi kama wawakilishi wa wanananchi wenyewe(wabunge) kingereza ni tatizo sasa hao wananchi wa kawaida hali ikoje?
Mimi nafikiri wakati umefika kwa uongozi wa TBC kutafakari kama kipindi hiki kina tija kwakweli hasa kwa kuangalia watanzania walio wengi.TBC wanaweza hata kufanya utafiti mdogo ili wawezi kujiridhisha na idadi ya watanzania wanaofuatilia kipindi hicho na kuona kama kuna umuhimu wa kuendelea nacho.
Ni vema kipini hicho kikarushwa katika lugha ya kiswahili kwani mambo mengi yanayojadiliwa katika kipindi hicho ni ya kitaifa na yanamuhusu mtanzania wa kawaida.
Pia,kwa ushauri tu,TBC wanaweza kuanzisha TBC English Service kama kuna umuhimu wa kuwa na vipindi kwa lugha ya kingereza.
Sikuzote nyie mnaojiita wasomi eti na ma-masters,ma-phd ndio vilaza wakubwa kushinda hata STD seven ya kizazi hiki.We kila siku km nchi mnataka mkuze lugha ya kiswahili,wakati huo huo TV ya taifa inajipendekeza kwa lugha ya kigeni.ukizingatia ni 2% ya wabongo wanaojua kingereza.si ukilaza huo?.
na ukifatilia cv ya mkurugenzi wa TBC,ana ma-digrii kibao.ila check anachofanya.hata hana washauri!!
Mie kipindi changu siku ya ijumaa ni KIPIMA JOTO cha ITV cha masako.hayo ma perspective mwayajua nyie wasomi.
Dah; hivi bado kipo...!? TBC1 mara ya mwisho kuiangalia ilikuwa kuna kipindi kizuri kinaitwa MCHAKATO MAJIMBONI
Dah; hivi bado kipo...!? TBC1 mara ya mwisho kuiangalia ilikuwa kuna kipindi kizuri kinaitwa MCHAKATO MAJIMBONI
Watanzania hebu tubadilikeni jamani,hatuwezi kuwa watu wa kulalamika tu kila kitu,tupo ktk dunia ya utandawazi na ni jambo zuri tukiwa na tamaduni ya kujifunza Lugha nyingine ili tuweze faidika na fursa za pande zote za dunia hii,tukishikiria Kiswahili tu bila kujifunza vingine hata hicho Kiswahili kitakufa kwani hakuna atakayekisambaza sehemu nyingine,tupende Lugha yetu Sawa lakini tusijifunge kujifunza vingine,wengi bado tupo hatua ya chini ya kujielewa,hatujui Kama hatuelewi ni nini cha kufanya.
Hebu tumia akili kidogo tu kuielewa point yangu,ni kweli Watanzania hatujui Kama hatuelewi ndio maana mipango yote huwa ni ya kubahatisha tu,kuwa na kipindi cha Lugha za kigeni sio tatizo,na kuwa na watu wachache wanaofuatilia hicho kipindi kwa sababu ya Lugha sio tatizo la anayekiandaa,inabidi baadhi ya watu wafanye jitihada ya kujifunza,na sio kutaka kuwa na standard moja tu ya maisha sababu wengine wako comfortable na level waliyonayo.Hongera unayejua nini cha kufanya.
Hiki kipindi hakiendani na uhalisia wa mtanzania. Hakina elimu jumuishi kwa watanzania wa chini. Sioni mantiki yake.