David Serikali
Member
- Mar 2, 2012
- 57
- 17
Masaa kadhaa yasiyozidi siku moja yakiwa yamepita tangu kuripotiwa kwa kujiunga na mtandao wa kijamii wa sura ya kitabu ( Facebook) na shirika la utangazaji la CBN NEWS Rais Barack Obama kafikisha wafuasi zaidi ya milioni arobaini na tano (45mil)
Kwa niaba ya Ikulu ya Marekani, Rais Barack Obama kafikia uamuzi wa kujiunga na mtandao wa kijamii wa sura ya kitabu (Facebook) kuongeza nguvu katika mapambano ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia Nchi kama kiongozi mwenye ushawishi mkubwa Duniani.
Muda mfupi baada ya kufungua ukurasa wa sura ya kitabu huo ikulu ya marekani ili-upload video ya Rais Barack Obama akinukuliwa akisema "Natumai mtachukulia huu kuwa ukumbi ambao tunaweza kutumia kujadiliana kuhusu masuala muhimu kuhusu taifa letu"asema kwenye video hiyo. Lengo kuu la likiwa ni kuhimiza ulimwengu kuunga mkono juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.