Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,794
GWAJIBOY AKIMKARIBISHA JPM: Mheshimiwa Rais karibu sana jimbo la Kawe. Watu wa Kawe wamekusanyika hapa kwa wingi kukupongeza kwa kazi kubwa uliyowafanyia. Kwa miaka mitano ya uongozi wako umetatua kero ya muda mrefu ya maji maeneo mengi ya jimbo letu.
Umepeleka umeme kata nyingi, umejenga vyumba vya madarasa kwenye kata karibu zote, umetanua barabara ya Bagamoyo kutoka Morocco hadi Mwenge ili kupunguza msongamano, umejenga barabara nyingi za mitaa kwa kiwango cha lami na zinapitika muda wote. Mheshimiwa Rais tunakushukuru sana.
GWAJIBOY AKIMZUNGUMZIA MDEE: Mheshimiwa Rais jimbo hili ni kama halina Mbunge. Kwa miaka mitano ya viti maalumu na 10 ya ubunge huyu mama hajali shida za wananchi kabisa. Maeneo mengi ya jimbo letu yana shida ya maji. Kata ya Mabwepande, Madale na Goba maji yanatoka mara moja tu kwa wiki na wakati mwingine hadi wiki mbili hayatoki.
Baadhi ya maeneo mtandao wa umeme haujafika kama kule Kisauke na Mbopo. Maeneo ya Mabwepande kuna uhaba wa vyumba vya madarasa watoto wanasongamana darasani na wengine wanakaa chini. Barabara nyingi za mitaa hazijakarabatiwa na hazipitiki. Mbunge yupo tu hakuna anachofanya. Kazi yake ni kuchochea migomo na kutoka bungeni.
Umepeleka umeme kata nyingi, umejenga vyumba vya madarasa kwenye kata karibu zote, umetanua barabara ya Bagamoyo kutoka Morocco hadi Mwenge ili kupunguza msongamano, umejenga barabara nyingi za mitaa kwa kiwango cha lami na zinapitika muda wote. Mheshimiwa Rais tunakushukuru sana.
GWAJIBOY AKIMZUNGUMZIA MDEE: Mheshimiwa Rais jimbo hili ni kama halina Mbunge. Kwa miaka mitano ya viti maalumu na 10 ya ubunge huyu mama hajali shida za wananchi kabisa. Maeneo mengi ya jimbo letu yana shida ya maji. Kata ya Mabwepande, Madale na Goba maji yanatoka mara moja tu kwa wiki na wakati mwingine hadi wiki mbili hayatoki.
Baadhi ya maeneo mtandao wa umeme haujafika kama kule Kisauke na Mbopo. Maeneo ya Mabwepande kuna uhaba wa vyumba vya madarasa watoto wanasongamana darasani na wengine wanakaa chini. Barabara nyingi za mitaa hazijakarabatiwa na hazipitiki. Mbunge yupo tu hakuna anachofanya. Kazi yake ni kuchochea migomo na kutoka bungeni.