Thinking beyond measures: CCM ni 'mafundi' wa kutengeneza 'matukio' na 'Wapinzani feki'

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,517
Mwenyezi Mungu amenijalia akili ya kufikiri. Naitumia kufikiri vyema kuhusu 'saga' inayoendelea ndani ya CCM. Nimeamua kufikiri vingine tofauti na kuona kuna mtifuano ndani ya CCM na hivyo tuendelee kukaa mkao wa kula kuona mwisho wake. CCM ni mafundi na mabingwa wa kutengeneza matukio na wapinzani feki.

Wenye kuangalia vyema, kwa undani na kwa umakini watakubaliana nami kuwa CCM huanzisha songombingo kama lililopo sasa kila unapokaribia uchaguzi mkuu wa Urais, Ubunge na Udiwani. Anzia mwaka 1995 (Mzee Mrema alipohama CCM na kugombea Urais kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi).....kumbuka 2000 (Prof. Lipumba 'alipotikisa' ).....fuatia 2010 (Dr. Slaa alipomkosesha usingizi Mzee Kikwete) na tena usisahau 2015(Lowassa alipohamia CHADEMA na kuwa mgombea wao)

Fikirini tena na kwa umakini. Matukio yanayoendelea ndani ya CCM si ya bahati mbaya. Ni matukio yanayoratibiwa kwa umakini mkubwa na yenye tija kwa chama hicho. Wakati umma na upinzani ukijihusisha na matukio hayo, CCM huitumia nafasi hiyo kujipanga na kufanya mambo yao bila ya kujadiliwa. Mwisho wa matukio haya huwa na zao la 'wapinzani feki' watakaomwagwa kuelekea upinzani kuteka Majimbo na Kata. Na hata kuwa wagombea wa Urais.

Hakika, CCM ni very intelligent and genius katika kutengeneza matukio na wapinzani feki. Hupoteza maboya sana katika kukaribia uchaguzi mkuu. Kwa hilo wanahitaji pongezi!

Waione: Kiranga , tindo , BAK , Evarist Chahali , Daudi Mchambuzi, manengelo , Pascal Mayalla, hearly na wengineo
 
Yaani wewe ni miongoni mwa watu wachache hapa nchini wenye macho ya kuona mbali.
Furaha ya vyama vya upinzani nchini ni kuona mmomonyoko kwenye chama tawala na bahati mbaya iliyopo kwetu sisi watanzania ni wepesi sana KUSAHAU (sisi hatutunzi kumbukumbu). 2015 sakata la Lowasa na CCM lilileta taharuki nchini hadi EL anaenda upinzani na kupewa kijiti cha kupeperusha bendera ya wapinzani.
Tumesahau figisu alizopata WS na kuondoka CHADEMA na hatimaye EL anakuja kuonekana ni tegemeo la mwisho kwa wapinzani na akapewa majukumu ya kuwapeleka kunako nchi ya ahadi.
Kwanini tu wepesi kusahau hivi? Kwanini kila leo tumekuwa watu wa kufurahia mtikisiko wa CCM badala ya watu kukaa na kutengeneza upinzani imara usiotegemea ugomvi wa CCM. Mwenyekiti wa CHADEMA na viongozi wakuu wa chama hicho wala hawana nia ya kutwaa dola hapa nchini na mkitaka kuamini angalieni mwenendo wao chamani, haitakuja kutokea siku CCM ikatoka madarakani kama ambavyo wengi mnaamini endapo bado mtakuwa wazito katika kutunza kumbukumbu.
Sijawahi kuona chama cha upinzani nchini chenye nia ya kuchukua dola....
 
Huo mzunguko wote Mkubwa wa kutengeneza matukio ni kwaajili ya faida gani?.. uchaguzi??
Kwa hili saga la akina nape sidhani kama ni tukio la kutengeneza,kama mahakama,jeshi la wananchi,polisi,Bunge na tume ya uchaguzi vipo chini Yao kuna haja gani ya kutengeneza matukio?

Kwa katiba hii mbovu kuna haja gani ya kutengeneza sinema Kwa Sisi wenye akili tunajua kabisa haya maccm sikuzote wapo kwajli ya matumbo Yao Tu ndio maana huko ndani hawajatulia kuanzia magu Hadi mawaziri wake!
 
Huo mzunguko wote Mkubwa wa kutengeneza matukio ni kwaajili ya faida gani?.. uchaguzi??
Kwa hili saga la akina nape sidhani kama ni tukio la kutengeneza,kama mahakama,jeshi la wananchi,polisi,Bunge na tume ya uchaguzi vipo chini Yao kuna haja gani ya kutengeneza matukio?

Kwa katiba hii mbovu kuna haja gani ya kutengeneza sinema Kwa Sisi wenye akili tunajua kabisa haya maccm sikuzote wapo kwajli ya matumbo Yao Tu ndio maana huko ndani hawajatulia kuanzia magu Hadi mawaziri wake!
Hayo huhalalisha Mkuu….jiongeze:D:D:D
 
Najaribu tu kuwaza kwa sauti. Hivi mwaka 2014 kulikuwa na songombingo ipi?
Manake mafisadi Papa walikuwa kipindo Cha kwnza Cha mzee wa msoga

BTW upinzani watakuwa Ni watu dhaifu Sana ikiwa Kama wataubeba mgogoro huu na kuanza kuushabikia badala ya kujenga upinzani wao wenyewe

Lkn niwatoe hofu mpinzani wa kweli atatika ccm lkn muda bado wa kufanya hivyo. Saa ya Bwana bado haijakaribia
 
Hakika, CCM ni very intelligent and genius katika kutengeneza matukio na wapinzani feki. Hupoteza maboya sana katika kukaribia uchaguzi mkuu. Kwa hilo wanahitaji pongezi!
Nilishawahi sema mahali fulani, kuwa kama akili inayotumia CCM kushinda chaguzi ingekuwa inatumika kuifanya Tanzania kuwa na maendeleo, amini nakwambia tungekuwa ni the best economy in Africa saivi,

CCM inatumia akili nyingi sana na mahesabu ya mbali
 
Mwenyezi Mungu amenijalia akili ya kufikiri. Naitumia kufikiri vyema kuhusu 'saga' inayoendelea ndani ya CCM. Nimeamua kufikiri vingine tofauti na kuona kuna mtifuano ndani ya CCM na hivyo tuendelee kukaa mkao wa kula kuona mwisho wake. CCM ni mafundi na mabingwa wa kutengeneza matukio na wapinzani feki.

Wenye kuangalia vyema, kwa undani na kwa umakini watakubaliana nami kuwa CCM huanzisha songombingo kama lililopo sasa kila unapokaribia uchaguzi mkuu wa Urais, Ubunge na Udiwani. Anzia mwaka 1995 (Mzee Mrema alipohama CCM na kugombea Urais kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi).....kumbuka 2000 (Prof. Lipumba 'alipotikisa' ).....fuatia 2010 (Dr. Slaa alipomkosesha usingizi Mzee Kikwete) na tena usisahau 2015(Lowassa alipohamia CHADEMA na kuwa mgombea wao)

Fikirini tena na kwa umakini. Matukio yanayoendelea ndani ya CCM si ya bahati mbaya. Ni matukio yanayoratibiwa kwa umakini mkubwa na yenye tija kwa chama hicho. Wakati umma na upinzani ukijihusisha na matukio hayo, CCM huitumia nafasi hiyo kujipanga na kufanya mambo yao bila ya kujadiliwa. Mwisho wa matukio haya huwa na zao la 'wapinzani feki' watakaomwagwa kuelekea upinzani kuteka Majimbo na Kata. Na hata kuwa wagombea wa Urais.

Hakika, CCM ni very intelligent and genius katika kutengeneza matukio na wapinzani feki. Hupoteza maboya sana katika kukaribia uchaguzi mkuu. Kwa hilo wanahitaji pongezi!

Waione: Kiranga , tindo , BAK , Evarist Chahali , Daudi Mchambuzi, manengelo , Pascal Mayalla, hearly na wengineo
Mkuu nakubaliana na wewe kushikilia mawazo yako lakino napingana na wewe kusema saga la sasa linalingana na yaliyopita. kumbuka sasa hivi ni kutokana na uongozi dhaifu, wenye chuki na hila wa Magufuli. Sio ugomvi wa kugombea, ni ugomvi unaotokana na dharau manyanyaso ya wao kwa wao. Sisi cha moto tumeshakizoea ndio maana hatutishiki lakini kwa hili ccm is real, sio mchongo.
 
Mkuu nakubaliana na wewe kushikilia mawazo yako lakino napingana na wewe kusema saga la sasa linalingana na yaliyopita. kumbuka sasa hivi ni kutokana na uongozi dhaifu, wenye chuki na hila wa Magufuli. Sio ugomvi wa kugombea, ni ugomvi unaotokana na dharau manyanyaso ya wao kwa wao. Sisi cha moto tumeshakizoea ndio maana hatutishiki lakini kwa hili ccm is real, sio mchongo.
Ngoja uone watakavyoshikana mikono na kukumbatiana wakiaminisha umma kuwa wao ni wamoja na wanaweza kutatua changamoto :D :D
 
Najaribu tu kuwaza kwa sauti. Hivi mwaka 2014 kulikuwa na songombingo ipi?
Manake mafisadi Papa walikuwa kipindo Cha kwnza Cha mzee wa msoga

BTW upinzani watakuwa Ni watu dhaifu Sana ikiwa Kama wataubeba mgogoro huu na kuanza kuushabikia badala ya kujenga upinzani wao wenyewe

Lkn niwatoe hofu mpinzani wa kweli atatika ccm lkn muda bado wa kufanya hivyo. Saa ya Bwana bado haijakaribia
2014 kulikuwa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na ilikuwa mwaka mmoja kama sasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2015.
 
Mkuu Kwangu Matukio makubwa na kwa wasiyo wanaccm nyakati za Uchaguzi ni Kuuawa kwa Albino, Watu kuchunwa ngozi nk. Haya Mimi yananichukiza.
CCM Matukio yote wala si mbinu ni Uroho wa Madaraka sababu, Vyeo kwa CCM ni Ulaji. Sasa wanahaha Maslahi yao yakibanwa.
Mrema ,Lipumba, Lowasa..nk wote ni Waroho wa Pesa na Madaraka FACT.
 
kipingamizi kikubwa alichonacho magufuri ni kupitishwa tu kwa mara nyingine na chama chake basi lakini kwingine atazoa kura kama zote kwa wananchi.Na hii yote ni kutokana na mfumo alioujenga ikiwa ni pamoja na kudhoofisha upinzani
 
Back
Top Bottom