Kwangu mimi Nape Nnauye ni kama Zito Kabwe wote ni career Politicians, hakuna kingine wanajua isipokuwa Siasa, na ni Siasa za Majungu, Fitina na Mipasho, wanaishi hivyo, sasa sijui watu kama hawa unafanya nao nini?
Unajua mtu mwenye profession yake utasema umrudishe labda Chuoni akafundishe, au umkabidhi Chuo Kikuu aendeshe, lkn sasa Nape Nnauye unafanya naye nini?
Kwa maana kiumri kwa kiasi fulani bado ni mdogo, na kuacha kupiga Gitaa sijui ana ujuzi gani mwingine nje ya Siasa, na hiyo ndiyo kwangu The Nape question, what to do with him?
Nape bado ni kinda katika kufahamu namna serikali inavyofanya kazi.
Nape aliaminiwa sana mpaka kuingizwa kwenye baraza la mawaziri la serikali ya awamu ya tano.
Lakini kuna mambo ambayo amekosea na ambayo ni lazima jifunze asije kurudia haya makosa:
1. Kuitisha haraka mkutano na wandishi wa habari na kutoa tamko alotoa kuhusu Makonda.
2. Kutoa tamko la kuunda tume hata kabla hajaitisha maelezo ya pande zote mbili.
Na hii si mara ya kwanza kwa Nape kufanya hivyo kwani tuliona alivyokuja na kauli baada ya orodha ya kwanza ya wanaojishughulisha na biashara ya madawa ilipotangazwa na Makonda.
Hivyo Nape anapaswa kujifunza utaratibu na protokali za kufanya linapotokea jambo kama hili ili asionekane kama anavyoonekana sasa kwamba hana uzoefu yaani "he lacks experience".
Lakini si ajabu, kwani binadamu tunajifunza kutokana na makosa.
Hali ni hivyohivyo kwa Makonda kwani naye amekosea kwenda pale studio bila taarifa na akiwa na askari wenye silaha za moto.
Isipokuwa kusema kwamba amevamia pale kituoni ni uzushi kwani ameingia pale kama watu wengine ambao wangeweza kuingia "main entrance".
Pia, akataka kuingia studio yenyewe na akafunguliwa mlango na akaingia jambo ambalo linapaswa kuulizwa yule security guard kwamba kwanini hakutaka kuwa shujaa kumzuia makonda asiingie ndani ya Studio?
CCTV hainyeshi "any struggle" kwa Makonda kuingia mahali pale kiasi cha kusema amevamia.
Nape na Makonda "have responsibility to face the consequences of their actions."
Ila kwa sasa ni muhimu kujifunza kutokana na makosa walotenda na kusonga mbele kulitumikia taifa.
Ila mkuu, naweza kuona wapi unaelekea na suali lako, isipokuwa Nape hiyo wizara inamfaa na ni bora aendelee hapohapo kwani amesomea fani inayoshabihiana na wizara aliyopo.