jMali
Biblia inanifundisha kwamba, nitumie kidogo nilicho nacho kabla sijapata kikubwa. Rwanda wamedhihirisha hicho kidogo walichopewa, wanakitumia kwa ufanisi.
Kwamba kuna Warwanda wanakimbilia Tanzania, inafaa ifahamike Tanzania kuna raslimali nyingi ikilinganishwa na Rwanda, Kenya, Burundi na Uganda hata zikiungana.
Mimi binafsi nimeishi Bongo na kuona fursa nyingi sana, mtu akijituma vizuri tu, anaondoka kwenye lindi la umaskini. Ni hizi fursa ndizo zinafanya mnaona wageni wakija huko Tanzania. Nchi wanazotoka zina ufanisi, hata fursa za uwekezaji zipo, lakini raslimali ni kiduchu.
Sasa mtaendelea kuona nchi zinatajwa kuwa bora katika kila kitu, lakini bado wanakuja Tanzania kwa ajili ya wingi wa raslimali Bongo.