The Manchester City (The Citizens) | Special Thread

DOGO acha mihemko, Rodri alikuja kama upgrade ya Fernandinho na sio replacement. Wakati Silva KDB tayari alikuwa kwenye Top of his game.

Kijana hujajua kuwa Upgrade bado ni replacement, mkuu tofauti ni kwamba replacement yetu imekuwa upgrade.

Alafu acha kubadilisha maana ya maneno. Ukisema Rodri alikuwa upgrade ya Fernandinho, basi unathibitisha hoja yangu, alikuwa successor wa Fernandinho, akaja akawa bora zaidi. Hiyo ndio maana ya replacement nzuri sio lazima awe copy ya aliyemtangulia.

Kuhusu KDB, City Walikuwa na mchezaji aliyekuwa tayari anainuka, halafu role yake ikabadilika na kupanuka baada ya Silva kuondoka.

Point ni kwamba City imewahi kupoteza legends, ikapata succession ambayo haikuwa copy paste, na timu ikaendelea kuwa bora.
 

Je hivi sasa timu ipo bora? kwa miaka miwili sasa City wamekuwa ni kichwa kibovu.
 
2022/23 na 2023/24 City ilichukua ligi, halafu 2024/25 ikashuka hadi nafasi ya 3, na 2025/26 ikarudi nafasi ya 2.

Kama unataka kusema City imekuwa ‘kichwa kibovu’, sawa, hiyo ni opinion yako. Lakini kwenye ligi yenyewe imetoka nafasi ya 3 hadi nafasi ya 2 msimu uliofuata. Sasa wewe unataka City ishinde kila mwaka ndio uone haijawa kichwa kibovu?

Nenda kwanza kaishauri timu yako ifike hiyo level. Kwa sasa City imeanza 2026/27 kwa mechi mbili, points 6, baada ya kuifunga Bournemouth 2–1 na Crystal Palace 4–1.
 
Tangu mwaka 2010 hadi sasa, Manchester City imekusanya mafanikio makubwa

8× Premier League
1× UEFA Champions League
3× FA Cup
6× League Cup
1× FIFA Club World Cup
1× UEFA Super Cup

Na rekodi ambayo hakuna timu nyingine ya England imewahi kufanya
Manchester City ndiyo timu pekee England iliyowahi kushinda Premier League mara 4 mfululizo.

Haya siyo maneno ya ushabiki haya ni mafanikio yanayoonekana kwenye historia na kwenye makabati ya klabu.
Manchester City FC
 
Liverpool na Man UTD washawahi kubeba ×4 au mtasema enzi hizo Ligi ilkuwa haitwii premier league, walkuwa wanacheza zama za mawe gizani.
 
Hapo ndipo umepanic kidogo. Liverpool walishinda ligi 4 mfululizo 1981/82–1983/84, lakini hiyo ilikuwa First Division, sio Premier League. Manchester United hawajawahi kushinda Premier League mara 4 mfululizorekodi yao ni mara 3.


Sisi tunaposema City ndiyo pekee England iliyoshinda Premier League mara 4 mfululizo, tunazungumzia Premier League, iliyoanza 1992. Rekodi rasmi ya Premier League inasema wazi Manchester City 4 consecutive PL titles, 2020/21–2023/24.


Kwa hiyo hakuna anayesema Liverpool au United hawana historia kubwa. Tunazungumzia tu rekodi hii maalum ya Premier League. Usichanganye First Division na Premier League halafu uje kusema City imejitungia rekodi.
 
Liverpool na Man UTD washawahi kubeba ×4 au mtasema enzi hizo Ligi ilkuwa haitwii premier league, walkuwa wanacheza zama za mawe gizani.
Liverpool ndio waliowahi kushinda First Division mara 4 mfululizo (1981/82–1983/84). Sio Man U.
 
MANCHESTER CITY | SAFARI YA ULAYA IMEANZA


Mashabiki wa The Citizens, safari ya kutafuta tena ubingwa wa Ulaya imeanza rasmi.


FC Porto 0–2 Manchester City
City imeanza kampeni yake kwa ushindi mzuri ugenini, na sasa macho yanaelekezwa kwenye mechi zinazofuata.


RATIBA YA MAN CITY – UEFA CHAMPIONS LEAGUE


Man City vs PSG — 14 Oktoba
Man City vs AEK Athens — 20 Oktoba
RB Leipzig vs Man City — 4 Novemba
Man City vs Napoli — 24 Novemba
Barcelona vs Man City — 8 Desemba
Lens vs Man City — 20 Januari 2027
Man City vs Sporting CP — 27 Januari 2027


MECHI ZA KUZIFUATILIA KWA KARIBU


Man City vs PSG
Barcelona vs Man City
Man City vs Napoli
RB Leipzig vs Man City


Lengo la City ni moja: kutwaa tena UEFA Champions League.


Kwa mtazamo wako, Man City ana nafasi gani ya kufika fainali na kutwaa ubingwa msimu huu?


#ManCity #MCFC #UCL #ChampionsLeague
 
Plastic fans wamerudi kwenye timu zao baada ya Pep kuondoka.
Plastic fans hahahahaha, Pep ameondoka, City bado anashinda. Kama huu ndio uzalendo wenu, basi endeleeni kujifariji na historia. Sisi tumeacha historia nyuma na tunaendelea kutoa vichapo tu.
 
Mnasubiri Nov-Dec mpate fans wapya muifukuzie Arsenal
Nov–Dec? Mmmmh Sawa, tutawafukuzia Arsenal. Ila wewe kwanza tuambie unaishabikia timu gani, maana unaongea kama shabiki wa Arsenal, United na Chelsea kwa zamu. Kama huna timu ya kusimamia, kaa pembeni uangalie City wakikimbiza Arsenal huku wewe ukibadilisha jezi kila wiki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…