The English of President Magufuli of Tanzania

Hivi mkuu ni nani aliyekuambia Rais wa china hajui kuzungumza kiingereza? Marais wote wa China yaani aliyepita na huyu wa saaa wanazungumza kiingereza kizuri tu ingawa sio native speakers.

Katika dunia ya sasa yenye kuhusisha meetings mbalimbali na international projects NI MUHIMU SANA KUJUA KIINGEREZA ikiwa ni international language na inayozungumzwa na viongozi wa nchi mbalimbali.

Wewe unataka Wakenya waendelee kufanya advert za rasilimali zetu huko nje kuwa ni zao? Jaribu kurefer back kwenye awamu ya tatu Zakhia Meghji alivyokuwa waziri wa Mali asili na Utalii ndio utajua kutokujua kiingereza kilivyotuponza.

Au unataka tuwe tunaletewa mikataba iliyoandikwa kwa very formal english tushindwe kuitathmini na kuichanganua?

Hao investors wanaokuja kuwekeza huku wanazungumza kiswahili?

Wafanyabiashara wa kitanzania wakifanya biashara na customers wa Egland,Ireland,USA,Canada,Jamaika n.k wanatumia kiswahili?

RAIS WETU AHAKIKISHE ANAZUNGUMZA KIINGEREZA FLUENTLY KWASABABU HATADEAL NA SISI WASWAHILI TU.
Utumwa wa kifikra. Unaweza kuwasiliana na mtu yeyote kwa lugha yako ya asili na kumpatia tafsiri. Ni uzuzu tu uliotutawala kudhani kuongea Kiingereza ndio maendeleo. By the way, Kiswahili ni lugha ya kimataifa
 
Kama haujui Twiga ni nembo ya Taifa Ila unajua Davido anavaa chupi gani na Wema mimba imetoka lini unataka nikuweke kwenye kundi gani!!!?? Nenda kasome WORLDATLAS Kama nilivyokuelekeza halafu kakojoe ulale. Au bado Unalala sebuleni kwa shemeji!!??
acha mbwembwe bwana mdogo nitajie akina kingkiki mc hammer na wengine wa enzi zangu. sasa nataka nikupe assignment mtoto mzuri tafuta tanzania coat of arms. kumbuka shemeji anakaa kwangu
 
Utajichosha bure achana nae huyo ni kama vitabu vya dini hana asilo lijua ,anabadilisha hoja mwanzo alikataa kwamba raisi sio nembo ya taifa akaja na madai yake nembo ya taifa ni twiga ,kuna waungwana wakamuuliza una uhakika na hicho akaishia kuwatukana

Sasa anaposema Twiga ni nembo ya Taifa sijui ni lini Twiga alisimama kwenye podium akawa anahutubia Mkutano wa umoja wa mataifa kwa niaba ya Watanzania ,
naona huyu atakuwa amepanic.
 
Utumwa wa kifikra. Unaweza kuwasiliana na mtu yeyote kwa lugha yako ya asili na kumpatia tafsiri. Ni uzuzu tu uliotutawala kudhani kuongea Kiingereza ndio maendeleo. By the way, Kiswahili ni lugha ya kimataifa
Kiswahili ni lugha ya kimataifa ndio na nakithamini sana ila Coverage yake haifikii hata robo ya English na je watu tunaodeal nao zaidi internationally katika almost all sphere of life ni watu wanaotumia lugha zipi?

Rais kujua lugha zaidi ya moja na hasa kiingereza ni added advantage.
 
Nad
Pumbavu sisi tuliomchagua atutumikie anatufaa hatukuchagua Rais kwa ajili ya watu wa nje huyo aliyekuwa anajua kizungu ukitakacho amekuachia nini wewe zobaa? RAIS wa China alikuja hapa anaongea kichina wewe na wajinga wenzio hamkuelewa alichotaka? Kumbuka huyo ni Rais wa watanzania na siyo Rais wa wakenya Uganda, Rwanda au Burundi.

Umeandika mambo marefu nikadhani unaongea kitu cha maana kumbe upumbavu na ujinga uliokujaa mpaka sehemu ambazo siwezi andika hapa maana nitakuwa mpumbavu kama wewe usiyejali Taifa lako. Unamkashifu Rais kwa sababu ya ujinga wako hivi mpaka amepata PhD ya kemia siku zote ulikuwa unamsemea wewe hivi English imekuwa lugha ngumu ya kujifunza miaka mia moja tena nasema acha kashifa mpumbavu wewe.
wewe ndiye utakuwa mpumbavu na mjinga! Nikuoneshe upumbavu wako kidogo: kiingereza sio lugha rasmi ya serikali ya china na wala haitumiki km lugha rasmi ya kufundishia km hapa kwetu. Hivyo wachina hawalazimiki kuijua. Hapa kwetu kiingereza ni lugha rasmi ya mawasiliano kiserikali na pia ni lugha rasmi ya kufundishia. Hivyo tunategemea viongozi wa serikali waimudu kiasi cha kuridhisha. By the way mleta mada kashauri anolewe vizuri kwenye lugha ili asituaibishe kimataifa. Kiingeteza na kiswahili ni lugha zetu, lazima tuzijue zote. Na lszima ujue kwamba kiingerezs leo sio cha waingereza tena bali lugha ya dunia. Ndio maana hata Kagame francophone, anazungumza kiingereza fssaha!
 
Kuukataa ukweli ni sawa na kujaribu kukimbia kivuli chako. Ukweli huwa unauma hasa kwa wale ambao hawapendi kuusikia, lakini ukweli ni kama dawa unatibu kwa wale walio tayari kuukubali na kuufanyia kazi. Unakuweka huru na wala hutahitaji kubishana wala kumtukana mtu, maana ndani ya moyo wako unajua hiki ni kweli.
Watu wasiokubali ukweli ni wabishi, wana hasira na mara nyingi hutoa maneno makali kwa sababu ukweli unakuwa unachoma mioyo yao. Wanaumia sana na wanaishia kutukana na hata kupigana. Lazima tufike mahali tukubali kwamba ukweli lazima utaumiza upande mmoja, kwani haugawanyiki. Upande unaoumizwa na ukweli usitafute mchawi, mchawi ni wao wenyewe wanaotaka kukimbia kivuli chao.
Mleta uzi umeeleza ukweli, sijashangaa kuona wasiopenda kusikia ukweli wakihamaki na kutoa lugha zinazoonesha walivyoumia. Sio kila mara utasikia kile unachopenda kusikia, tuwe wavumilivu pia kusikia kile tusichokipenda. Huo ndio uungwana. Na wakati mwingine kama jambo hulipendi, we pita tu endelea na yako....yaani puuza tu ili usiumie bure.
MKUU HUO UKWELI HUJAUSEMA NI UPI MAANA HAPA KUNAPANDE MBILI ZINAVUTANA MIMI NAAMINI KUTOKUJUA KIINGEREZA SIO DHAMBI NA WALA HAKUZUII MAENDELEO YA NCHI,WENGINE HAPA WANAAMINI ILI RAIS ALETE AU AONGOZE KULETA MAENDELEO LAZIMA AJUE KIINGEREZA SASA HAPO HAPO HATUJUI UMESIMAMA UPANDE GANI.
 
Ushabiki wa kisiasa hautufai hapa, leteni utetezi wenye mashiko. Kama kiingereza hakina maana mbona hata huyo JPM kasoma toka sekondari hadi PhD kwa kutumia kiingerza hicho hicho. Leo vijana wetu wa sekondari na vyuo bado wanasoma kwa kutumia kiingereza hicho hicho alafu leo munasema hakifai? Kama ni kulaumu basi tuilaumu CCM yenu kwa sababu ndo imekiohodhi kiingereza kwa kushindwa kubadili lugha ya kutumia kuanzia sekondari hadi vyuo. Hapa nyie mbumbumbu munachojivunia na munayemkashifu ni nani kama siyo CCM?

Kibaya zaidi mbali ya utetezi wote huo bado yeye rais mwenyewe anajichanganya kwa kuchanganya kiswahili na kiingereza!! Mtindo huu wa kuchanganya kiswahili na kiingereza umetumika sana na watu wengi wanaojifanya wamesoma. Hiki kinachoendelea kwa kuchanganya lugha kinatuabisha kwani udhaifu wa dhahiri umejionyesha kwamba hata tukiwa wasomi lugha ya kiingereza kwetu sisi watanzania ni ngumu sana. Ni vyema tukaweka wazi kwamba lugha ya kufundishia shuleni toka chekechea mpaka vyuoni iwe kiingereza na huko mtaani tutumie kiswahili. Kinyume na hapo wanasiasa, watawala na watu wenye uwezo wa kifedha watapeleka watoto wao shule zinazotumia kiingereza na kuishia kuja kuwananga watoto wa walalahoi.
 
Kuukataa ukweli ni sawa na kujaribu kukimbia kivuli chako. Ukweli huwa unauma hasa kwa wale ambao hawapendi kuusikia, lakini ukweli ni kama dawa unatibu kwa wale walio tayari kuukubali na kuufanyia kazi. Unakuweka huru na wala hutahitaji kubishana wala kumtukana mtu, maana ndani ya moyo wako unajua hiki ni kweli.
Watu wasiokubali ukweli ni wabishi, wana hasira na mara nyingi hutoa maneno makali kwa sababu ukweli unakuwa unachoma mioyo yao. Wanaumia sana na wanaishia kutukana na hata kupigana. Lazima tufike mahali tukubali kwamba ukweli lazima utaumiza upande mmoja, kwani haugawanyiki. Upande unaoumizwa na ukweli usitafute mchawi, mchawi ni wao wenyewe wanaotaka kukimbia kivuli chao.
Mleta uzi umeeleza ukweli, sijashangaa kuona wasiopenda kusikia ukweli wakihamaki na kutoa lugha zinazoonesha walivyoumia. Sio kila mara utasikia kile unachopenda kusikia, tuwe wavumilivu pia kusikia kile tusichokipenda. Huo ndio uungwana. Na wakati mwingine kama jambo hulipendi, we pita tu endelea na yako....yaani puuza tu ili usiumie bure.
Ukweli ni kwamba sie Watanzania tuna kasumba ya kupenda visivyo vyetu kuliko vilivyo vyetu.

Miaka kadhaa huko nyuma, mwalimu mmoja asili yake Wales aliniambia hivi: "ukiongea Kiingereza huku una lafidhi ya kigeni maana yake ni kwamba una lugha yako ya asili zaidi ya Kiingereza, na hiyo ni plus kwa sababu sie Waingereza hatuna muda wa kujifunza lugha za kigeni." Tangu wakati huo nikaachana na jitihada za kusaka lafidhi ya 'Kiingereza cha BBC."

Ni watu wenye matatizo ya akili wanaoweza kusumbuka kumkosoa kiongozi wa taifa lao kwa kuongea lugha ya kigeni kwa mapungufu kidogo. Sio lugha yetu anyway...
 
Correct urs first mr
Bolt na Kibanzi lol Hao marais wa Kenya,Uganda,Rwanda etc angejua wanaukubali mziki wa my President mmmmh hata hivyo mtoa mada analake jambo siamini kama kweli judgment yake kwa Kiongozi mzuri ni kuongea lugha fulani.
Hakuna kitu JPM ananifulahisha ni kuamini kwamba Nothing is Impossible kwa vitendo "Hapa ......"
 
Sidhani kama anahitaji kufahamu ndugu mleta mada. Kuna Raisi wengi sana hawafahamu hata punje ya kiingereza

Huu utetezi wako ni dhaifu sana, hizo nchi kiingereza inatumika kama lugha yao ya kufundishia? Hii mada ni kama tumeamua kujiabisha na vyema tukaachana nayo. Ila ni jambo linalotia hasira sana, watawala wanatangaza majukwaani kwamba kiswahili kiwe lugha ya kufundishia lakini wao wanapeleka watoto wao shule zinazofundisha kwa kiingereza, kama sio kufanyana majuha ni nini?
 
Watu Kama wewe mleta mada uko tayari kumsamehe mtu anayemtafuna mkeo kwa sababu tu amekuomba msamaha kiingereza. Watwana hamuishi kwenye jamii ya Kitanzania. Umeshawahi kumsikia Xi Jinping akiongea kiingereza!!??? Umeshawahi kumsikia Francois Hollande akiongea kiingereza!!!??? Umeshawahi kumsikia Putin akiongea Kiingereza!!?? Umeshawahi kumsikia Kim Jong-Un akiongea kiingereza!!!???
Acha utwana Nyamafu wee...
Ameshawahi kumsikia Angela merkel akiongea kiingereza?lakini uchumi wa ujerumani ni stable tangu amekuwa rais
 
Hahahahahahah...Mungu wangu eeeeeeehhh...wewe ndio umeharibu kabisaaaaa...afadhali bro magu...duh....jamani kama huju kiingereza andika hata kingoni....duh

cc Nyani Ngabu
Freeland mie sio mwingeleza kama rais ndio maana does na do ni mgogoro! But that does not mean I'm useless like you! Point yangu ilikuwa wazi, do we miss anything by this guy (my president) having bad command of your English? He is delivering! That is all I need!
 
Watu Kama wewe mleta mada uko tayari kumsamehe mtu anayemtafuna mkeo kwa sababu tu amekuomba msamaha kiingereza. Watwana hamuishi kwenye jamii ya Kitanzania. Umeshawahi kumsikia Xi Jinping akiongea kiingereza!!??? Umeshawahi kumsikia Francois Hollande akiongea kiingereza!!!??? Umeshawahi kumsikia Putin akiongea Kiingereza!!?? Umeshawahi kumsikia Kim Jong-Un akiongea kiingereza!!!???
Acha utwana Nyamafu wee...
Ingawa wanaomponda rais kwa kuongea kiingereza kibovu nao wakitumia kiingereza kibovu vile vile, sitaki kukuunga mkono kwamifano yako. Karibu wote ukiowataja lugha zao zinatumika kimataifa ikiwemo huko UN. Lugha ni mhimu sana katika mahusiano ya kimataifa, ndiyo maana tutake tusitake inabidi tu tuzijue hizo lugha za kimataifa au kama Nyerere alivyokiita kiingereza, "kiswahili cha kimataifa".
 
Kwa upumbavu wako huohuo Kikwete alivyohutubia Kiswahili ule mkutano wa AU ilikuwa lugha rasmi ya AU au? Haya wachina haohao wanafanya biashara sana duniani lakini kiingereza chako hawakijui na mambo yanakwenda wewe unamshambulia Rais kwa hajui English mpaka anachukua PhD siku zote alikuwa na mkalimani ambaye ni mpumbavu kama wewe? Je, wajua Phd ya kemia inasomwa miaka mingapi na ufanyeje ndipo ukubalike kwenye jumuiya ya wasomi Duniani? Kumbuka Magufuli amesoma seminary na Lugha ndiko iliko lala sasa wewe unaleta ujinga wako halafu tukuangalie tu waambie wajinga wenzio hapa hunipati.
 
Ameshawahi kumsikia Angela merkel akiongea kiingereza?lakini uchumi wa ujerumani ni stable tangu amekuwa rais
Tumhukumu Magufuli kwa uongozi wake wala sio Kiingereza chake. Most of us Watanzania twaongea broken English anyway.
 
inaonesha ana hasira za kukimbilia kuokata mawe. najiuliza mbona anajihami kwa matusi mtoto wa kiume
Sijui ana vicheo gani sasa anataka kuleta upumbavu wa vyeo vyake humu Jamii Forum ,kama asipo jihami kwa matusi anakimbilia kupiga watu mikwara wanaume humu ,
 
Back
Top Bottom