Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Huyu Mwanakijiji mtoto wa Nyerere kapotelea wapi kwenye hii thread? nataka sababu kwa nini wazanzibar wakiridhia kujiondoa hawataweza!
sasa kuitana majina ndio kunafanya hoja ziwe na nguvu? Wazanzibari hawawezi kuvunja muungano bila kusababisha vita.. nyinyi mnafanya mchezo. Kuna nchi moja inaitwa Tanzania na uhaini au kujaribu kuivunja ni kosa kubwa zaidi dhidi ya jamhuri hiyo. Najua watu mnachukulia kiutani utani tu. Muungano wa Tanzania ni halali kisheria, kihistoria na kimantiki. Na ni kweli wanaoleta fyoko fyoko watatiwa ndani na hautavunjika ati kwa sababu watu wanakasirishwa na mambo fulani. Hakuna muungano mkamilifu duniani na ni jukumu la wananchi na taasisi mbalimbali za nchi hiyo mara zote kufanya kazi ya kuujenga na kuuboresha. NInachosikia watu wanacholalamikia siyo muungano hasa bali ni mambo mbalimbali ambayo tunayita "kero". Sasa badala ya kuwashughulikia viongozi wabovu wasio na maono ya kutatua muungano au kukiondoa madarakani chama ambacho hakina uwezo wa kuboresha muungano watu wanataka kukimbia.
Tuna katabia kauoga kakuogopa kushughulikia matatizo kwa sababu "they are too hard" au hatutaki kuwakwaza. Hili ndilo lililosababisha hata hoja ya Utanganyika kwani badala ya kushughulikia waliovunja katiba kwa kuingiza Zanzibar OIC wao wakataka kuanzisha Tanganyika. Na ndivyo ilivyo sasa, matatizo ya muungano ni yapi - watu wanasema "siupendi"! Asilimia labda 80 wa Watanzania wote hawajawahi kuwa raia wa Zanzibar au Tanganyika!!
Watanzania tuna matatizo sana.. hatutaki kushughulikia mambo magumu tunafikiri kujenga muungano ni kuunganisha michanga tu halatu tunaenda kulala kusubiri ujijenge. Angalia Waingereza wanavyohangaika na muungano wao, angalia Wacanada na suala la Quebec, angalia hata RSA, angalia Mexico, Marekani ndio usiseme kabisa, wao ndugu zao wa KUsini waliamua kabisa kujitenga na kutangaza rais wao! guess what.. they went to war to protect the union!! SAsa sisi Watanzania tukiwaambia tutakwenda vitani kulinda muungano waoga wanaanza "not worthy it!".. ndio aina ya viongozi tulionao!