Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeendesha mafunzo kwa Askari wa Jeshi la Polisi mkoani Arusha kuhusiana na uzingatiwaji wa haki za binadamu na misingi ya Utawala Bora katika mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
Akizungumza na Askari hao leo Septemba 17, 2025, Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo Bw. Mohamed Hamadi amesema kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya mpango wa tume kufikisha elimu kwa makundi mbalimbali katika jamii ikiwemo Jeshi la Polisi kwa ajili ya kukumbushana haki na wajibu wao katika kulinda haki za binadamu
Aidha, tume hiyo pamoja na mambo mengine ilipata fursa ya kusikiliza maoni mbalimbali kutoka kwa washiriki wa mafunzo hayo kwa ajili ya kuboresha utendaji wa kazi
Naye Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP Faraja Sangwa amesema mafunzo hayo yamekuwa na tija katika kuboresha utendaji wao wa kazi na kuahidi kuwa wataendelea kuhakikisha wanazingatia haki za binadamu katika utekelezaji wa majukumu yao
Akizungumza na Askari hao leo Septemba 17, 2025, Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo Bw. Mohamed Hamadi amesema kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya mpango wa tume kufikisha elimu kwa makundi mbalimbali katika jamii ikiwemo Jeshi la Polisi kwa ajili ya kukumbushana haki na wajibu wao katika kulinda haki za binadamu
Aidha, tume hiyo pamoja na mambo mengine ilipata fursa ya kusikiliza maoni mbalimbali kutoka kwa washiriki wa mafunzo hayo kwa ajili ya kuboresha utendaji wa kazi
Naye Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP Faraja Sangwa amesema mafunzo hayo yamekuwa na tija katika kuboresha utendaji wao wa kazi na kuahidi kuwa wataendelea kuhakikisha wanazingatia haki za binadamu katika utekelezaji wa majukumu yao