Thamani ya tsh 10,000/ kuelekea mwisho wa mwaka jijini: Gazeti la Uhuru limedanganya

Kinoamiguu

JF-Expert Member
Nov 29, 2018
10,526
13,015
Sijui kwanini wanapenda kudanganya wakati wenzao wakitoa takwimu wanakuwa wakali hata kuwaweka ndani.

Mhariri wa gazeti la Uhuru la leo ameandika ukiwa na 10elfu na ukiwa unaishi Tandika Maguruwe unaweza kupika/kuandaa pilau ya kuliwa na watu wanne 4. uongo.

Wametoa mchanganuo wa mahitaji ya kuandaa pilau na kubakiwa na chenji ya tsh 200.

Nimejiuliza maswali mengi sana lakini kubwa ni umuhimu wa habari ile mpaka kuwa kwenye front page? Mhariri yule anataka kusema watu wanaolalamika ugumu wa maisha ni waongo maana sikukuu inaweza kupita kwa elfu 10 tu? Hajui mahitaji ya sikukuu kwamba sio pilau tu kuna mengine kama nguo nk.

Je, mhariri yule anataka kutuaminisha kwamba watanzania wote wanaishi Tandika Maguruwe? Mbona kuna maeneo bei zinatofautiana sana na huko Maguruwe?

Anachotakiwa kujua mhariri wa gazeti la Uhuru na wanaomtuma ni kwamba maisha ya watu yameharibiwa na utawala huu kiasi cha sikukuu kukosa maana. aidha upatikanaji wa hiyo elfu 10 umekuwa mgumu kweli.

Chukulia mfano mkulima wa korosho wa kule Misasa/ Mkuranga hajalipwa pesa mpaka leo kwa kinachoitwa kukagua mashamba hiyo elfu 10 anaipataje?
msidanganye watu
 
Nilijua utakuja na mchanganuo wa hiyo 10000 na kuonesha uongo wao.Licha ya hivyo Mimi mwenyewe ukiniambia vyuma vimekaza nashindwa kuelewa. Hawa wanaolia vyuma kukaza ndio waliojazana Ubungo wanalia kukosa usafiri wa kwenda vijijini kwao kusherehekea Sikukuu.Wanapata wapi hela za kwenda Kula bata kijijini?Nilitegemea nione mwaka huu rate ya watu kurudi mikoani ni ndogo sana kulingana na vyuma kukaza maajabu ni idadi imekuwa kubwa sana.Huu ni mfano kwa Dar tu.
 
Sijui kwa nn wanapenda kudanganya wakati wenzao wakitoa takwimu wanakuwa wakali hata kuwaweka ndani.
Mhariri wa gazeti la Uhuru la leo ameandika ukiwa na 10elfu na ukiwa unaishi Tandika Maguruwe unaweza kupika/kuandaa pilau ya kuliwa na watu wanne 4. uongo.
wametoa mchanganuo wa mahitaji ya kuandaa pilau na kubakiwa na chenji ya tsh 200.
nimejiuliza maswali mengi sana lakini kubwa ni umuhimu wa habar ile mpaka kuwa kwenye front page? mhariri yule anataka kusema watu wanaolalamika ugumu wa maisha ni waongo maana sikukuu inaweza kupita kwa elfu 10 tu? hajui mahitaji ya sikukuu kwamba sio pilau tu kuna mengine kama nguo nk.
je, muhalili yule anataka kutuaminisha kwamba watanzania wote wanaishi tandika maguruwe? mbona kunamaeneo bei zinatofautiana sana na huko maguruwe?
Anachotakiwa kujua mhariri wa gazeti la Uhuru na wanaomtuma ni kwamba maisha ya watu yameharibiwa na utawala huu kiasi cha sikukuu kukosa maana. aidha upatikanaji wa hiyo elfu 10 umekuwa mgumu kweli. chukulia mfano mkulima wa korosho wa kule Misasa/ mkuranga hajalipwa pesa mpaka leo kwa kinachoitwa kukagua mashamba hiyo elfu 10 anaipataje?
msidanganye watu

Mahitaji ya chakula nyumbani (wastani wa walaji wasiopungua wanne per meal):-

1. Mchele 1kg -Sh. 2,000/=

2. Nyama (ng'ombe) 1kg - Sh. 8,000/=

3. Carrot 3 - Sh. 1,000/=

4. Mafuta kula (Alzeti -Singida) 1litre - Sh. 2,000/=

5. Nyanya 3 - Sh. 1,000/=

6. Mchicha 1 pc - Sh. 400/=

7. Kabichi 1 pc - Sh. 1,200/=

8. Ndimu, pilipili, n.k
Ngapi hizooooo?

I rest my case!!
 
Nilijua utakuja na mchanganuo wa hiyo 10000 na kuonesha uongo wao.Licha ya hivyo Mimi mwenyewe ukiniambia vyuma vimekaza nashindwa kuelewa. Hawa wanaolia vyuma kukaza ndio waliojazana Ubungo wanalia kukosa usafiri wa kwenda vijijini kwao kusherehekea Sikukuu.Wanapata wapi hela za kwenda Kula bata kijijini?Nilitegemea nione mwaka huu rate ya watu kurudi mikoani ni ndogo sana kulingana na vyuma kukaza maajabu ni idadi imekuwa kubwa sana.Huu ni mfano kwa Dar tu.
Endeleeni kuongoza misukule.
 
Mahitaji ya chakula nyumbani (wastani wa walaji wasiopungua wanne per meal):-

1. Mchele 1kg -Sh. 2,000/=

2. Nyama (ng'ombe) 1kg - Sh. 8,000/=

3. Carrot 3 - Sh. 1,000/=

4. Mafuta kula (Alzeti -Singida) 1litre - Sh. 2,000/=

5. Nyanya 3 - Sh. 1,000/=

6. Mchicha 1 pc - Sh. 400/=

7. Kabichi 1 pc - Sh. 1,200/=

8. Ndimu, pilipili, n.k
Ngapi hizooooo?

I rest my case!!

Mchele 1kg=nyama nusu=mafuta robo.

Anza upya.
 
Mahitaji ya chakula nyumbani (wastani wa walaji wasiopungua wanne per meal):-

1. Mchele 1kg -Sh. 2,000/=

2. Nyama (ng'ombe) 1kg - Sh. 8,000/=

3. Carrot 3 - Sh. 1,000/=

4. Mafuta kula (Alzeti -Singida) 1litre - Sh. 2,000/=

5. Nyanya 3 - Sh. 1,000/=

6. Mchicha 1 pc - Sh. 400/=

7. Kabichi 1 pc - Sh. 1,200/=

8. Ndimu, pilipili, n.k
Ngapi hizooooo?

I rest my case!!
Hivi kweli kupika pilau la kilo moja unahitaj Mafuta Lita moja?
 
Kwa mlo mmoja inawezekana ununue nyama nusu kilo 3,500, mchele kilo 1, 2,200, mafuta ya kupima ya 1,000, kopo la mkaa 1,000. Chumvi ya mia, viungo vya pilau vya 1,000, nyanya, tango na kitunguu kwa kachumbari 1,000 = 9,800
Huu ni mlo wa sikukuu au kawaida, Mimi ndo sijui sikukuu kumbe.
 
Duh sikuwahi fikiri kama kuna watu bado wanasoma Uhuru na Mzalendo huh!!
 
Nilijua utakuja na mchanganuo wa hiyo 10000 na kuonesha uongo wao.Licha ya hivyo Mimi mwenyewe ukiniambia vyuma vimekaza nashindwa kuelewa. Hawa wanaolia vyuma kukaza ndio waliojazana Ubungo wanalia kukosa usafiri wa kwenda vijijini kwao kusherehekea Sikukuu.Wanapata wapi hela za kwenda Kula bata kijijini?Nilitegemea nione mwaka huu rate ya watu kurudi mikoani ni ndogo sana kulingana na vyuma kukaza maajabu ni idadi imekuwa kubwa sana.Huu ni mfano kwa Dar tu.

Daladala zinajaza,na mpya zinaingia kila siku,magari bandari yanakombolewa kila siku,mtu anasema hela hakunaunabaki umeduwaa,hujui ni tatizo la macho ama nini!!!
 
15700
Mahitaji ya chakula nyumbani (wastani wa walaji wasiopungua wanne per meal):-

1. Mchele 1kg -Sh. 2,000/=

2. Nyama (ng'ombe) 1kg - Sh. 8,000/=

3. Carrot 3 - Sh. 1,000/=

4. Mafuta kula (Alzeti -Singida) 1litre - Sh. 2,000/=

5. Nyanya 3 - Sh. 1,000/=

6. Mchicha 1 pc - Sh. 400/=

7. Kabichi 1 pc - Sh. 1,200/=

8. Ndimu, pilipili, n.k
Ngapi hizooooo?

I rest my case!!
 
Daladala zinajaza,na mpya zinaingia kila siku,magari bandari yanakombolewa kila siku,mtu anasema hela hakunaunabaki umeduwaa,hujui ni tatizo la macho ama nini!!!
Hahahahahahah huwa sielewi kabisa huu wimbo wa vyuma kukaza. Mimi naona ni propaganda tu. Ukipita viwanja vya Kula bata huko tabata unashindwa kuelewa hawa ndio watanzania wanaolia vyuma vimekaza au ni wageni tu.
 
Huu ni mlo wa sikukuu au kawaida, Mimi ndo sijui sikukuu kumbe.

Sikukuu ni jambo jingine, lakini kama unataka chakula cha kutosha watu wanne kwa ulaji wa kawaida kwa mlo mmoja inawezekana maana mahesabu halisi ndio hayo.
 
hao hawana ishu, mfano mi nakula kilo peke yangu, na hao watatu wengine watakula nini? kwa watu wa nne kilo moja haitoshi! elfu kumi tu labda niwe peke yangu ingawa bado naiona haitoshi pia!
 
Wacheni mzaha na maisha ya watu.
Naomba nisiendelee nitatoa povu bila sababu wadanganyeni wajinga.
 
Kwa mlo mmoja inawezekana ununue nyama nusu kilo 3,500, mchele kilo 1, 2,200, mafuta ya kupima ya 1,000, kopo la mkaa 1,000. Chumvi ya mia, viungo vya pilau vya 1,000, nyanya, tango na kitunguu kwa kachumbari 1,000 = 9,800
Tena hapo umejibana sana aisee
 
Kwa mlo mmoja inawezekana ununue nyama nusu kilo 3,500, mchele kilo 1, 2,200, mafuta ya kupima ya 1,000, kopo la mkaa 1,000. Chumvi ya mia, viungo vya pilau vya 1,000, nyanya, tango na kitunguu kwa kachumbari 1,000 = 9,800
Dah...yaani sikukuu bila soda....kweli?
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Mahitaji ya chakula nyumbani (wastani wa walaji wasiopungua wanne per meal):-

1. Mchele 1kg -Sh. 2,000/=

2. Nyama (ng'ombe) 1kg - Sh. 8,000/=

3. Carrot 3 - Sh. 1,000/=

4. Mafuta kula (Alzeti -Singida) 1litre - Sh. 2,000/=

5. Nyanya 3 - Sh. 1,000/=

6. Mchicha 1 pc - Sh. 400/=

7. Kabichi 1 pc - Sh. 1,200/=

8. Ndimu, pilipili, n.k
Ngapi hizooooo?

I rest my case!!
Mh labda kwa bei za ushuwani mkuu
Mchele kg 1 bei kuna 1500-22
Mahitaji ya chakula nyumbani (wastani wa walaji wasiopungua wanne per meal):-

1. Mchele 1kg -Sh. 2,000/=

2. Nyama (ng'ombe) 1kg - Sh. 8,000/=

3. Carrot 3 - Sh. 1,000/=

4. Mafuta kula (Alzeti -Singida) 1litre - Sh. 2,000/=

5. Nyanya 3 - Sh. 1,000/=

6. Mchicha 1 pc - Sh. 400/=

7. Kabichi 1 pc - Sh. 1,200/=

8. Ndimu, pilipili, n.k
Ngapi hizooooo?

I rest my case!!
Labda kwa bei za ushuwani kwa Hulu uswazi

Mchele kg 1 kuna 1500-2200

Nyama kg1 - sh 6000 nusu 3500 Inatosha

Carrot 3 Sh 300 @ 100

Mafuta ya pilau sh 500 yanatosha

Nyanya fungu 500

Mchicha fungu 400

Kabichi robo 500

Viazi fungu 500

pilipili hoho 3 sh 300

Ndimu 2- 200

Pilipili Kali 1 sh 100
 
Sikukuu ni jambo jingine, lakini kama unataka chakula cha kutosha watu wanne kwa ulaji wa kawaida kwa mlo mmoja inawezekana maana mahesabu halisi ndio hayo.
Chakula cha kawaida sawa, lakini cha sikukuu kama walivyosema wao!! Sijui lakini.
 
Back
Top Bottom