Thamani halisi ya binti

Thamani halisi ya binti

Nyenyere

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2010
Posts
14,842
Reaction score
10,765
Wakuu kumekucha tena. Nimejitia kuandika zaidi kuhusu mabinti kwa lengo moja tu, kujaribu kukifumbua macho kizazi kinachopotea kwa kasi. Najua majibizano na maneno makali yatokayo hasa kwa wanawake kwenye mada za namna hii lakini imefika wakati ukweli lazima usemwe.

Hapa naongelea mabinti wanawali ambao hawajamjua mume bado. Thamani halisi kabisa ya binti iko kwenye bikra yake. Mungu alipomuumba mwanamke alimwekea kiwambo (seal) ambacho ni ni muhimu kwa ajili ya kuweka agano na mume wake wa ndoa. Kama ijulikanavyo katika ulimwengu wa roho, maagano huwekwa kwa damu, ndio maana hicho kiwambo kinapotolewa damu humwagika kama ishara ya kuweka muhuri agano. Kiwambo hicho (hymen) ndio thamani kuu ya binti yeyote hapa duniani. Why?

Bikra ni ishara kuu kwamba binti hajamjua mume bado, kwamba anatambua thamani yake, kwamba uaminifu wake hautiliwi shaka kamwe, kwamba anaweza kujizuia na kujilinda hata mbele ya social pressure, kwamba ni mwenye tabia njema n.k. Binti bikira (mwana mwali) ukimtazama tu tabia na mwenendo wake huwa ni tofauti kabisa na mabinti wengine. Ni mwenye soni, ni mwenye kuepuka maongezi mabaya, ni mtiifu hata kwa wazazi n.k.

Ukimtazama binti aliyeyajua madyudyu utamtambua tu ,hili liko wazi kabisa. Hii haikutokea kwa bahati mbaya, ni mpangilio wa Mungu hali iwe hivyo. Hata kwa wale wasioamini Mungu bado mnaweza kushuhudia hiki nikisemacho. Hata wazazi huhitimisha mafunzo yao kwa binti pale anapoanza tu kushiriki ngono, kwani huhesabiwa kati ya watu wazima.

Sasa basi, tutazame madhara ya binti kujiingiza kwenye mapenzi kabla ya ndoa.

1. Atahesabiwa kati ya makahaba
Ni ukweli usiofichika kwamba mwanamke aliyeanza mapenzi mapema tangu awali aliitwa kahaba. Dunia ya leo imebadili kiasi maana halisi ya neno hilo kumaanisha ni mwanamke ajiuzaye. Lakini ni ukweli kuwa hata huyu ajitoaye huanza kutafuta matunzo kutoka kwa mwanamume anayejamiiana naye, huku ndiko kutafuta mapato (ujira) kwenyewe!! Kupoteza bikra huondoa kiwambo cha agano la mume, hivyo thamani ya mwanamke haipo tena. Hapa uaminifu hupimwa kwa maneno na si matendo tena ambapo ndoa hugeuka tendo la imani. Haipaswi kuwa hivyo, mwnamke ameumbiwa uaminifu tangu kuzaliwa kwake, mume anapaswa kumpima kwenye utii tu.

2. Ulimwengu wa mwili na roho hufunguka
Kama nilivyotoa utangulizi, binti akijiingiza tu kwenye ngono hujiona amekuwa. Tayari hakuna tena siri iliyofichika kwake kwani siri ya mwisho kwa mwanadamu ni tendo la ngono. Ataingia kwenye ulimwengu wa roho akiwa hayuko tayari, kwani tendo la ngono ni tendo la kiroho. Kwa sababu binti huyu hajawa tayari kuukabili ulimwengu, atasombwa na kila aina ya mafundisho kwani amejiingiza kwenye daraja la ujuaji. Kwake yeye si mwanamke mwenzake, si mwanamume wala wazazi wenye jipya la kumpa kwani mafunzo ya binti hukoma pale tu anapomjua mume.

3. Hujiondolea kabisa uwezekano wa kupata ndoa
Kuna tofauti kubwa kati ya kupata mume na kupata ndoa. Watu wengi wameingia kwenye ushirika wa kimahusiano wakidhani kuwa ni ndoa, mwishowe wameishia kujutia kwa kiwango kikubwa. Ushirika wa kimahusiano kwa maana kuwa tayari mwanamke alishafunga agano la ndoa na mwanamume mwingine kabla aliyemtoa bikra, agano la damu lidumulo mpaka kufa kwao, ndipo wakaja kupata mshirika wa kuishi naye kama mume na mke, wakifunga agano la mdomoni tu jambo ambalo ni maigizo ya mchana kweupe. Agano la ndoa ni la damu, binti awaache wazazi wake akiwa INTACT, akaanze maisha na mumewe. Hii ndio ndoa halisi, mengine ni ushirika tu wa mke na mume. Ndio maana ndoa za leo zimejaa malalamiko, manung'uniko, kukosa furaha, kukosa amani n.k.

4. Hugeuka mwanaharakati kwenye mahusiano
Baadhi ya sifa za mke wa ndoa ni heshima na adabu, aibu kwa mume, kutambua nafasi ya mume kwenye ndoa, uaminifu (huthibitishwa na bikra si maneno tu) n.k. Mwanamke aliyejiingiza kwenye ngono kabla, amefunguka ufahamu na kujidhani anaijua dunia kama wanaume tu, hivyo tofauti waliyonayo ni sex organs tu. Wengi wao hugeuka wanaharakati kwenye ndoa zao (ndoa kwa maana mpya) wakidai usawa kwenye mambo mbalimbali ambayo kimsingi ni mgawanyo wa majukumu. Hawaoni tofauti kati ya mtu mke na mtu mume, wasiokuwa na adabu wala heshima. Inashangaza kuwasikia wakidai, mwanamume angebebeshwa mimba kwa japo dakika moja tu asingeweza wakati kumbe huo ni uumbaji, na kama mwanamume huyu angebeba kweli mimba basi angekoma kuitwa mwanamume kwani ni tendo la mwanamke hilo. Ni aina ya wanawake walioharibika akili zao kwa kujazwa mafundisho ya uongo yaliyo kinyume na asili ya mwanadamu.

Hawa ni aina ya wanawake ambao wanadhani wanayajua mapenzi vema, huja na list ya "mimi nataka mume wangu awe na a, b, c..... kwa sababu wameshazibuka. Binti mwenye kulinfa usichana wake hatohangaika asilani kutafuta kijana mwenye kukidhi orodha ndeefu ya sifa kwani bado hajui mapenzi ni nini. Atatulia huku akisubiri ampate mume sahihi kwa kipimo cha wazaxi.

Kimsingi kuoa mwanamke wa namna hii ni bahati nasibu, kwani lolote laweza kuwa ndani ya ndoa. Aweza kuwa mtaratibu na msikivu kabla ya ndoa hasa wakati wa uchumba kusudi amnase mwanamume, kisha ndipo hufungua makucha. Pia kwa sababu ameshaonja ya dunia kabla, hujiingiza kwenye makundi ya wanawake waliozoelea ngono, ambao akili zao zimetawaliwa na namna ya dunia hii, kiasi kwamba apatapo mwanamume wa kumwoa hubadili mwonekano wa nje ili tu afanikishe lengo, kisha matatizo huhamia ndani.

Ni ukweli ndoa nyingi zama zetu zinakwenda kwa kauli mbiu ya kuvumiliana na kuchukuliana mizigo. Kama unabisha fuatilia aina ya mafundisho yatolewayo kwenye semina mbalimbali za ndoa, iwe kwenye dini au tu kwingineko. Vijana wanafunzwa kuwavumilia wake kwenye madhaifu ambayo kimsingi sio madhaifu, ni tabia, pia mabjnti wanafundishwa jinsi ya kuwazuga waume zao ili wawanase kwenye mtego wa penzi. Semina na machapisho ya "JINSI YA KUMTULIZA MUME na mengine ya JINSI YA KUMRIDHISHA MWANAMKE ndio yametamalaki katika zama hizi. Mwanamke akifundishwa jinsi ya kumridhisha mwanamke aliyezoelea maisha ya ukahaba wakati mwanamke naye akifundishwa jinsi ya kumtuliza mwanamume asiyeridhika na kilichomo ndani ya mkewe. Yaani ni ulimwengu wa maigizo tu, hakuna uhalisia.

Najua neno hili ni gumu mno, hivyo nimejiandaa kutupiwa mawe!!
 
Inaaminika kuwa wakina dada wamebeba mafanikio ya waume zao na ndiyo sababu wanatakiwa kutojihusisha na tendo la ndoa na mtu yeyote isipokuwa mume wake.

Ikiaminika kuwa nyota ya mafanikio ya Mwanaume ipo katika ubikira pale tendo la ndoa linapofanyika kwa Mara ya kwanza Na mume wake anaiachilia hiyo baraka kwake.
Hii ni moja ya sababu kwanini apatae mke apata kitu chema..apata kibali kwa Bwana



*Sababu zinazowapelekea vijana wengi kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa
-mapenzi Kama njia ya kuonyesha upendo(sex as an expression of love)
.
-hofu ya kupoteza mahusiano
-mazingira ya furaha kupitiliza/sherehe/ulevi
.
-mavaz yanayoonyesha sehemu za maungo ya mwanamke
-kwa kuamini kuwa akiutoa mwili wake atapendwa zaidi
.
-wapo vijana wanaojiingiza ktk mahusiano ya kingono tu kwa hofu ya kutokuonekana hawawezi kufanya mapenzi ktk Rika lake au kwa Marafiki zake(my friends will think there's something wrong with me if I won't have sex)
.
-Wapo vijana walioaminishwa kuwa wanahitaji kuwa na uzoefu wa mambo ya mapenzi ili wasije wakaaibika siku ya ndoa yao
.
Wengine wameaminishwa kuwa wasipofanya mapenzi kabla ya ndoa wanaweza kuja kuumia siku wakija kufanya ndoani, hivyo ni Bora kuanza kufanya mazoezi mapema.
.
Elimu dunia,maneno ya upotoshaji
Mf usipofanya utakuwa zuzu,utapata ugonjwa wa kuchekacheka



*Namna wachumba wanavyoweza kuanguka katika zinaa
-kwa kukaa maeneo ya uficho wakiwa pekeyao

-kwa kujaribu kulala kitanda kimoja

-kwa kuvaa mavazi yenye ushawishi wa kimapenzi mnapotembeleana

-kwa kupenda kutembeleana nyakati za usiku

- mikao ya kimapenzi mkiwa pekeyenu

-Kujali(care)kunakopitiliza

-kwa kuwa na Marafiki wanaokushawishi kufanya mapenzi na mchumba wako.
1kor15:33
Msidanganyike, mazungumzo mabaya huharibu tabia njema
 
Naona
Inaaminika kuwa wakina dada wamebeba matanikio ya waume zao na ndiyo sababu wanatakiwa kutojihusisha na tendo la ndoa na mtu yeyote isipokuwa mume wake.

Ikiaminika kuwa nyota ya mafanikio ya Mwanaume ipo katika ubikira pale tendo la ndoa linapofanyika kwa Mara ya kwanza Na mume wake anaiachilia hiyo baraka kwake.
Hii ni moja ya sababu kwanini apatae mke apata kitu chema..apata kibali kwa Bwana



*Sababu zinazowapelekea vijana wengi kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa
-mapenzi Kama njia ya kuonyesha upendo(sex as an expression of love)
.
-hofu ya kupoteza mahusiano
-mazingira ya furaha kupitiliza/sherehe/ulevi
.
-mavaz yanayoonyesha sehemu za maungo ya mwanamke
-kwa kuamini kuwa akiutoa mwili wake atapendwa zaidi
.
-wapo vijana wanaojiingiza ktk mahusiano ya kingono tu kwa hofu ya kutokuonekana hawawezi kufanya mapenzi ktk Rika lake au kwa Marafiki zake(my friends will think there's something wrong with me if I won't have sex)
.
-Wapo vijana walioaminishwa kuwa wanahitaji kuwa na uzoefu wa mambo ya mapenzi ili wasije wakaaibika siku ya ndoa yao
.
Wengine wameaminishwa kuwa wasipofanya mapenzi kabla ya ndoa wanaweza kuja kuumia siku wakija kufanya ndoani, hivyo ni Bora kuanza kufanya mazoezi mapema.
.
Elimu dunia,maneno ya upotoshaji
Mf usipofanya utakuwa zuzu,utapata ugonjwa wa kuchekacheka



*Namna wachumba wanavyoweza kuanguka katika zinaa
-kwa kukaa maeneo ya uficho wakiwa pekeyao

-kwa kujaribu kulala kitanda kimoja

-kwa kuvaa mavazi yenye ushawishi wa kimapenzi mnapotembeleana

-kwa kupenda kutembeleana nyakati za usiku

- mikao ya kimapenzi mkiwa pekeyenu

-Kujali(care)kunakopitiliza

-kwa kuwa na Marafiki wanaokushawishi kufanya mapenzi na mchumba wako.
1kor15:33
Msidanganyike, mizungumzo mabaya huharibu tabia njema
Naona unashindiliaa
 
Bibie umeolewa?
Inaaminika kuwa wakina dada wamebeba matanikio ya waume zao na ndiyo sababu wanatakiwa kutojihusisha na tendo la ndoa na mtu yeyote isipokuwa mume wake.

Ikiaminika kuwa nyota ya mafanikio ya Mwanaume ipo katika ubikira pale tendo la ndoa linapofanyika kwa Mara ya kwanza Na mume wake anaiachilia hiyo baraka kwake.
Hii ni moja ya sababu kwanini apatae mke apata kitu chema..apata kibali kwa Bwana



*Sababu zinazowapelekea vijana wengi kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa
-mapenzi Kama njia ya kuonyesha upendo(sex as an expression of love)
.
-hofu ya kupoteza mahusiano
-mazingira ya furaha kupitiliza/sherehe/ulevi
.
-mavaz yanayoonyesha sehemu za maungo ya mwanamke
-kwa kuamini kuwa akiutoa mwili wake atapendwa zaidi
.
-wapo vijana wanaojiingiza ktk mahusiano ya kingono tu kwa hofu ya kutokuonekana hawawezi kufanya mapenzi ktk Rika lake au kwa Marafiki zake(my friends will think there's something wrong with me if I won't have sex)
.
-Wapo vijana walioaminishwa kuwa wanahitaji kuwa na uzoefu wa mambo ya mapenzi ili wasije wakaaibika siku ya ndoa yao
.
Wengine wameaminishwa kuwa wasipofanya mapenzi kabla ya ndoa wanaweza kuja kuumia siku wakija kufanya ndoani, hivyo ni Bora kuanza kufanya mazoezi mapema.
.
Elimu dunia,maneno ya upotoshaji
Mf usipofanya utakuwa zuzu,utapata ugonjwa wa kuchekacheka



*Namna wachumba wanavyoweza kuanguka katika zinaa
-kwa kukaa maeneo ya uficho wakiwa pekeyao

-kwa kujaribu kulala kitanda kimoja

-kwa kuvaa mavazi yenye ushawishi wa kimapenzi mnapotembeleana

-kwa kupenda kutembeleana nyakati za usiku

- mikao ya kimapenzi mkiwa pekeyenu

-Kujali(care)kunakopitiliza

-kwa kuwa na Marafiki wanaokushawishi kufanya mapenzi na mchumba wako.
1kor15:33
Msidanganyike, mazungumzo mabaya huharibu tabia njema
 
hawa mbuzi wanaskiaga basi..

ongeza volume mkuu mengine yako back bancher huko..
 
Inaaminika kuwa wakina dada wamebeba mafanikio ya waume zao na ndiyo sababu wanatakiwa kutojihusisha na tendo la ndoa na mtu yeyote isipokuwa mume wake.

Ikiaminika kuwa nyota ya mafanikio ya Mwanaume ipo katika ubikira pale tendo la ndoa linapofanyika kwa Mara ya kwanza Na mume wake anaiachilia hiyo baraka kwake.
Hii ni moja ya sababu kwanini apatae mke apata kitu chema..apata kibali kwa Bwana



*Sababu zinazowapelekea vijana wengi kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa
-mapenzi Kama njia ya kuonyesha upendo(sex as an expression of love)
.
-hofu ya kupoteza mahusiano
-mazingira ya furaha kupitiliza/sherehe/ulevi
.
-mavaz yanayoonyesha sehemu za maungo ya mwanamke
-kwa kuamini kuwa akiutoa mwili wake atapendwa zaidi
.
-wapo vijana wanaojiingiza ktk mahusiano ya kingono tu kwa hofu ya kutokuonekana hawawezi kufanya mapenzi ktk Rika lake au kwa Marafiki zake(my friends will think there's something wrong with me if I won't have sex)
.
-Wapo vijana walioaminishwa kuwa wanahitaji kuwa na uzoefu wa mambo ya mapenzi ili wasije wakaaibika siku ya ndoa yao
.
Wengine wameaminishwa kuwa wasipofanya mapenzi kabla ya ndoa wanaweza kuja kuumia siku wakija kufanya ndoani, hivyo ni Bora kuanza kufanya mazoezi mapema.
.
Elimu dunia,maneno ya upotoshaji
Mf usipofanya utakuwa zuzu,utapata ugonjwa wa kuchekacheka



*Namna wachumba wanavyoweza kuanguka katika zinaa
-kwa kukaa maeneo ya uficho wakiwa pekeyao

-kwa kujaribu kulala kitanda kimoja

-kwa kuvaa mavazi yenye ushawishi wa kimapenzi mnapotembeleana

-kwa kupenda kutembeleana nyakati za usiku

- mikao ya kimapenzi mkiwa pekeyenu

-Kujali(care)kunakopitiliza

-kwa kuwa na Marafiki wanaokushawishi kufanya mapenzi na mchumba wako.
1kor15:33
Msidanganyike, mazungumzo mabaya huharibu tabia njema
Uchafu umeanzia hapo uliposema kuwa mafanikio ya Mwanaume yamebebwa na Mwanamke,

*Hivi akili zako zina akili kabisa kabisa kichwani Mwakib?

*Mafanikio anatoa Binadamu au Mungu?

SOMA ZAIDI HAPA

KUMBUKUMBU LA TORATI 8:18.
 
Back
Top Bottom