Thadei Ole Mushi: Hivi Tanzania tuna Think Tanks?

Alex Fredrick

JF-Expert Member
Jun 21, 2016
680
1,338
HIVI TANZANIA TUNA THINK TANKS?

Na Thadei Ole Mushi.

Bei ya mafuta imepanda sana lita moja ya Petrol kwa sasa inafika hadi Shilingi 3,000. Nimeangalia Lita moja ya Mafuta hadi inashushwa pale badarini ni shilingi 1,162.

Yakishafika tunaweka kodi na Tozo Mbalimbali hadi yanafikia zaidi ya 3,000.

Kazi ya Ewura ni kutangaza Bei Mpya tu badala ya Ku regulate na kuishauri serikali. Hawana kazi nyingine wao ni kutangaza tu.... hawawezi hata kunusa kinachoweza kutokea baadaye na kutoa Solutions. Nafikiri kwa Sasa Serikali inaweza kufanya yafuatayo.

1. Kwenye kila kipengele cha Tozo wapunguze angalau kwa Ailimia kadhaa, Mfano badala ya VAT kuwa asilimia 18 wafanye asilimia 10 katika kipindi hiki.

2. Kuna haja ya kuindoa Tozo nyingine kwa sasa zisiwepo hadi hali ya Uchumi wa Dunia utakapotengemaaa.

3. Serikali ipunguze Matumizi yake ambayo si ya lazima kwa sasa mfano kutembelea anuani za Makazi kwa Chopa.

Tusikae kimya.....kazi kubwa ya Serikali ni kuhakikisha maisha ya wananchi wake yanakuwa marahisi... tuchukue hatua angalau kidogo tu kuonyesha tunajali. Maumivu makubwa ya ongezeko hili la bei ya mafuta anaumia mwananchi wa kawaida kabisa huku chini.

Hivi tuna Think tanks za kushauri Serikali?

Pale Marekani Washington DC kuna kituo kinachoitwa "Peterson institute for International Economics" (PIIE).

Kituo hiki kazi yake kubwa ni kutafiti na kushauri masuala mbalimbali ya kiuchumi na mahusiano ya kiuchumi. Kwa Marekani ndipo "Think Tanks" wao wanapofanyia kazi. Ili uajiriwe hapa lazima kichwani pawe vizuri si suala la kushukuru kuondoka jalalani tu ila kweli uwe na independent Mind.

Hawa wajamaa wamepewa Uhuru mkubwa sana wa kutafiti na hawafichi kitu report yote wanaitangaza kama ilivyo, kule kwao top Researchers wote wapo hapa wanasugua akili na sio kitambi. Hawa wajamaa wakiitisha press kila mtu anasogelea TV, na kila Media inawasogelea.

Sio marekani tu nchi kibao kama China, India, Venezuela nk zina Pool ya Think Tanks yaani mtu au kiongozi akitaka kufanya jambo lazima awaone. Achana na Hawa unaosikia kuwa ni mshauri wa Rais masuala ya kisiasa au mshauri wa waziri mkuu. Hawa sifa yao lazima kwanza wawe Huru ndio maana kituo hiki cha Marekani ni private institute...

Mfano pale India wao wamegawanya Think Tanks wao kutokana na maeneo mbalimbali, wana vituo 48 vya Think Tanks kama ACDR hawa wanashughulika na Siasa tu, CICR hawa ni Kilimo tu nk.

Pale uarabuni kituo cha Bookings Doha Center January 30 mwaka 2019 waliitisha panel ya Think Tanks wote katika Zone yao. Waliohudhuria ni pamoja na Nader Kabbani, MKUU wa kituo cha utafiti cha (BDC), Ezzeddine Abdelmoula, manager wa utafiti wa Al Jazeera, Mahjoob Zweiri, mkuu wa Gulf Studies Center ya Qatar University, Sari Hanafi, professor wa American University wengine walikuwa Mohammad Almasri mkuu wa Arab Center kituo cha utafiti na undaji wa Sera, Osman Ayfarah, mtangazaji wa Al Jazeera na aliyesimamia majadiliano. Hawa wajamaa wanaiongelea miaka 50 ijayo, mojawapo ya recommendations walizotoa ni Viongozi wao wote kuchukua mawazo kabla ya kufanya chochote kwenye taasisi hizi za Think Tanks.

Nadhani hata hapa kwetu tuna watu wanaoweza kuunda tume ya wachumi wakafanya kazi na mwananchi wa chini akasaidika.

Ole Mushi
0712702602.
FB_IMG_1651644242065.jpg
 
Ameandika vitu ambavyo hana ufahamu navyo
Kwanza bei sasa hivi sio karibia 3000 bali ni zaidi ya 3000
Pia sio kweli kwa sasa bei ya mafuta hadi pale bandarini ni 1162.
Kuna mchezo umechezwa Ila pamoja na hayo bei kwa sasa ni around 1800 hadi yanafika bandarini
 
Ameandika vitu ambavyo hana ufahamu navyo
Kwanza bei sasa hivi sio karibia 3000 bali ni zaidi ya 3000
Pia sio kweli kwa sasa bei ya mafuta hadi pale bandarini ni 1162.
Kuna mchezo umechezwa Ila pamoja na hayo bei kwa sasa ni around 1800 hadi yanafika bandarini
PhD in Econometrics
 
Shida sio think tanks mbona Financial Intelligence Unit ipo imejaa vipanga wa finance, uchumi, na forensic auditing etc na huwa Wana detect any economic sabotage, money laundering schemes etc. Kwa hiyo kimakaratasi tunao hao think tanks.

Tatizo letu ni kuwa Katiba yetu Inasema Rais hawajibiki kuchukua ushauri wa mtu na hatokuwa responsible kwa Tatizo lolote litakalotokana na kupuuza ushauri huo!!

In fact hata bunge ambako Sheria ya bajeti inapitishwa wakiipinga vifungu vya bajeti ikiwemo hizo tozo na kupanda kwa bei za mafuta BUNGE LINAVUNJWA.

Kwa nchi za wenzetu hata Kenya tu maamuzi ya taasisi kama Ewura huwa yanapingwa mahakamani kabisa, sasa haya yote unayoshaurI hayawezi tekelezeka sababu hakuna uwajibikaji kwenye katiba ya sasa Kila kitu kinampa nguvu Rais na hahojiwi popote!!

So mnaweza shauri ila hamna chombo chochote Cha kuenforce maazimio ya hao washauri!!
 
zinahitajika fedha za kuendesha shughuli za serikali, jamani hali ni ngumuuuu
 
Sijawahai kuona CCM na Serikali yake kuna siku imeguswa na matatizo ya moja kwa moja ya Watanzania...!
 
Hapa hatuna kiongozi..... Kiongozi huwezi kuwa kila siku unatoa projections ambazo ziko obvious(sababu hakuna asiyejua kwamba mafuta yatapanda) badala ya kusema hatua mlizochukua ili kukabiliana na hiko kinachokuja.

Kauli zake zinamaanisha wao kama waongoza nchi wameshasurrender na mfumuko uliopo, yaani hawana la kufanya ndiyo maana hawana plans zoozote(zingekuwepo angezisema).

Na kwa kuthibitisha hilo ndiyo maana yeye mwenyewe alirudisha ile tozo ya 100/= kwa kila lita baada ya waziri wa nishati kuifuta, hii inamaanisha serikali kama serikali imesurrender kwenye huu mfumuko.


THIS IS VERY STRANGE, AND ITS VERY DANGEROUS TO HAVE SUCH POLITICAL LEADERS IN THE TOP LEVEL OF THE COUNTRY.


Screenshot_20220504-121616.jpg
 
zinahitajika fedha za kuendesha shughuli za serikali, jamani hali ni ngumuuuu
Ndo inatakiwa serikali kubana matumizi yasiyo ya lazima ili kunusuru maisha ya watu.......vigogo wanafanya anasa na magari ya V8 sijui VXR wakati uchumi hauwezi kubeba hizo luxuries, badala yake mnabakia kuweka tozo kila mahali na kusababisha bidhaa na huduma kupanda bei na kuongeza ukali wa maisha kwa watanzania wengi maskini.
 
Ndo inatakiwa serikali kubana matumizi yasiyo ya lazima ili kunusuru maisha ya watu.......vigogo wanafanya anasa na magari ya V8 sijui VXR wakati uchumi hauwezi kubeba hizo luxuries, badala yake mnabakia kuweka tozo kila mahali na kusababisha bidhaa na huduma kupanda bei na kuongeza ukali wa maisha kwa watanzania wengi maskini.
Yaani ukigusia suala la viongozi kuacha kutumia ma V8 lazima wskuone wewe siyo raia
 
Wabunge hivi Wana kazi gan kule ? Mi naona hata hizo posho za 300k wanazopewa kila kikao ziondolewe na wapewe hata 50k tu ya kulipia chumba na chakula
 
Hii nchi kwenye hii awamu ya tano tulichagua vilaza wote kipindi cha magufuli tulikuwa tunasma magufuli siyo mfariji hasa yanapotokea majanga ya kijamii Ila Kwa uyuu mama naye Hana plani yoyote linapotokea swala la kiuchumi au ajira nilitegemea apunguze zile Kodi zinazotolewa kwenye mafuta Ila dah Aya ngoja tuone
 
HIVI TANZANIA TUNA THINK TANKS?

Na Thadei Ole Mushi.

Bei ya mafuta imepanda sana lita moja ya Petrol kwa sasa inafika hadi Shilingi 3,000. Nimeangalia Lita moja ya Mafuta hadi inashushwa pale badarini ni shilingi 1,162.

Yakishafika tunaweka kodi na Tozo Mbalimbali hadi yanafikia zaidi ya 3,000.

Kazi ya Ewura ni kutangaza Bei Mpya tu badala ya Ku regulate na kuishauri serikali. Hawana kazi nyingine wao ni kutangaza tu.... hawawezi hata kunusa kinachoweza kutokea baadaye na kutoa Solutions. Nafikiri kwa Sasa Serikali inaweza kufanya yafuatayo.

1. Kwenye kila kipengele cha Tozo wapunguze angalau kwa Ailimia kadhaa, Mfano badala ya VAT kuwa asilimia 18 wafanye asilimia 10 katika kipindi hiki.

2. Kuna haja ya kuindoa Tozo nyingine kwa sasa zisiwepo hadi hali ya Uchumi wa Dunia utakapotengemaaa.

3. Serikali ipunguze Matumizi yake ambayo si ya lazima kwa sasa mfano kutembelea anuani za Makazi kwa Chopa.

Tusikae kimya.....kazi kubwa ya Serikali ni kuhakikisha maisha ya wananchi wake yanakuwa marahisi... tuchukue hatua angalau kidogo tu kuonyesha tunajali. Maumivu makubwa ya ongezeko hili la bei ya mafuta anaumia mwananchi wa kawaida kabisa huku chini.

Hivi tuna Think tanks za kushauri Serikali?

Pale Marekani Washington DC kuna kituo kinachoitwa "Peterson institute for International Economics" (PIIE).

Kituo hiki kazi yake kubwa ni kutafiti na kushauri masuala mbalimbali ya kiuchumi na mahusiano ya kiuchumi. Kwa Marekani ndipo "Think Tanks" wao wanapofanyia kazi. Ili uajiriwe hapa lazima kichwani pawe vizuri si suala la kushukuru kuondoka jalalani tu ila kweli uwe na independent Mind.

Hawa wajamaa wamepewa Uhuru mkubwa sana wa kutafiti na hawafichi kitu report yote wanaitangaza kama ilivyo, kule kwao top Researchers wote wapo hapa wanasugua akili na sio kitambi. Hawa wajamaa wakiitisha press kila mtu anasogelea TV, na kila Media inawasogelea.

Sio marekani tu nchi kibao kama China, India, Venezuela nk zina Pool ya Think Tanks yaani mtu au kiongozi akitaka kufanya jambo lazima awaone. Achana na Hawa unaosikia kuwa ni mshauri wa Rais masuala ya kisiasa au mshauri wa waziri mkuu. Hawa sifa yao lazima kwanza wawe Huru ndio maana kituo hiki cha Marekani ni private institute...

Mfano pale India wao wamegawanya Think Tanks wao kutokana na maeneo mbalimbali, wana vituo 48 vya Think Tanks kama ACDR hawa wanashughulika na Siasa tu, CICR hawa ni Kilimo tu nk.

Pale uarabuni kituo cha Bookings Doha Center January 30 mwaka 2019 waliitisha panel ya Think Tanks wote katika Zone yao. Waliohudhuria ni pamoja na Nader Kabbani, MKUU wa kituo cha utafiti cha (BDC), Ezzeddine Abdelmoula, manager wa utafiti wa Al Jazeera, Mahjoob Zweiri, mkuu wa Gulf Studies Center ya Qatar University, Sari Hanafi, professor wa American University wengine walikuwa Mohammad Almasri mkuu wa Arab Center kituo cha utafiti na undaji wa Sera, Osman Ayfarah, mtangazaji wa Al Jazeera na aliyesimamia majadiliano. Hawa wajamaa wanaiongelea miaka 50 ijayo, mojawapo ya recommendations walizotoa ni Viongozi wao wote kuchukua mawazo kabla ya kufanya chochote kwenye taasisi hizi za Think Tanks.

Nadhani hata hapa kwetu tuna watu wanaoweza kuunda tume ya wachumi wakafanya kazi na mwananchi wa chini akasaidika.

Ole Mushi
0712702602.View attachment 2211041
Huu ni uongo,mafuta hayawezi kufika Dar port kwa 1162 afu eti ghafla yawe sh.3,000 plus..

Huu ni uongo wa mchana kweupe..

Nitoe ushauri kwa Serikali na niliwahi kutoa na ntakuwa narudia hapa..

Ni hivi,watu wengi wananunua bidhaa bila kudai risiti na wauzaji wanaangalia mtu usoni ndio wanamkatia risiti.

Hivyo basi undeni taskforce kila mahala na zikae mitaani,wapeni hiyo Kazi askari na migambo washirikiane na TRA.

Iwe ni doria mchana na usiku,mkikamata mtu kanunua bidhaa bila risiti mzi confiscate hizo bidhaa na zipigwe mnada Ili kufidia Kodi iliyokwepa na muuzaji apigwe faini ya kutosha..

Mkifanya hili zoezi kuwa endelevu kila mtu atadai risiti mwenyewe na atatoa mwenyewe na hapo sasa hamtahitaji kuweka Kodi kwenye mafuta..

Simple tuu .
 
Huu ni uongo,mafuta hayawezi kufika Dar port kwa 1162 afu eti ghafla yawe sh.3,000 plus..

Huu ni uongo wa mchana kweupe..

Nitoe ushauri kwa Serikali na niliwahi kutoa na ntakuwa narudia hapa..

Ni hivi,watu wengi wananunua bidhaa bila kudai risiti na wauzaji wanaangalia mtu usoni ndio wanamkatia risiti.

Hivyo basi undeni taskforce kila mahala na zikae mitaani,wapeni hiyo Kazi askari na migambo washirikiane na TRA.

Iwe ni doria mchana na usiku,mkikamata mtu kanunua bidhaa bila risiti mzi confiscate hizo bidhaa na zipigwe mnada Ili kufidia Kodi iliyokwepa na muuzaji apigwe faini ya kutosha..

Mkifanya hili zoezi kuwa endelevu kila mtu atadai risiti mwenyewe na atatoa mwenyewe na hapo sasa hamtahitaji kuweka Kodi kwenye mafuta..

Simple tuu .
Umesoma andiko na kulielewa vizuri
 
Ameandika vitu ambavyo hana ufahamu navyo
Kwanza bei sasa hivi sio karibia 3000 bali ni zaidi ya 3000
Pia sio kweli kwa sasa bei ya mafuta hadi pale bandarini ni 1162.
Kuna mchezo umechezwa Ila pamoja na hayo bei kwa sasa ni around 1800 hadi yanafika bandarini

Sasa Hapo umeandika Nini? Vijana wajinga amuwezi kuisha ulishindwa kumrekebisha mpka umkosoe?
 
Hapa hatuna kiongozi..... Kiongozi huwezi kuwa kila siku unatoa projections ambazo ziko obvious(sababu hakuna asiyejua kwamba mafuta yatapanda) badala ya kusema hatua mlizochukua ili kukabiliana na hiko kinachokuja.

Kauli zake zinamaanisha wao kama waongoza nchi wameshasurrender na mfumuko uliopo, yaani hawana la kufanya ndiyo maana hawana plans zoozote(zingekuwepo angezisema).

Na kwa kuthibitisha hilo ndiyo maana yeye mwenyewe alirudisha ile tozo ya 100/= kwa kila lita baada ya waziri wa nishati kuifuta, hii inamaanisha serikali kama serikali imesurrender kwenye huu mfumuko.


THIS IS VERY STRANGE, AND ITS VERY DANGEROUS TO HAVE SUCH POLITICAL LEADERS IN THE TOP LEVEL OF THE COUNTRY.


View attachment 2211064
Zwazwa huyu hangaya
 
Back
Top Bottom