MTAZAMO
JF-Expert Member
- Feb 8, 2011
- 19,643
- 33,438
Wakuu,
Ni dhahiri TFF kuna shida kubwa na inaelekea kupelekeshwa na siasa za Kariakoo. Kuna mtiririko wa matukio ambao unaacha doa kubwa ambalo ipo siku hizi nyufa tutajenga ukuta. Haya ni machache yanayofikirisha sana;
1) Mkataba wa GSM na TFF uliopigiwa kelele na jinsi ulivyofutika imebaki gizani ila maswali mengi yamesalia.
2) Sakata la Manara na adhabu yake, Yanga na Manara kuvunja maelekezo ya TFF siku ya wananchi. Tuliambiwa Hersi na Manara watahojiwa na hatua kuchukuliwa lakini hakuna kilichotokea.
3) Manara kufanya tukio hilo no.2 na kuendelea kuishutumu wazi TFF na Rais wake baada ya kifungo kupitia page yake rasmi lakini tumesikia rufaa yake imetupwa ila kwa busara adhabu imepunguzwa, sasa hapo kwenye busara si dalili ya Manara hakustahili adhabu iliyotolewa mwanzo?
4) Sakata la Kisinda ambalo TFF walisema Yanga wamezidisha idadi lakini mwezi mmoja toka ligi ianze wanampitisha mchezaji huyo huyo kwa "busara". Mbaya zaidi dirisha lilishafungwa! Mnajua kitachokuja mbele?
5) Barua za mawasiliano ya kiofisi kuvujishwa kwa wachambuzi na kusomwa hadharani. Hii ni dalili kuna "viongozi" walikuwa pia " vitani" hadi wakavuka mipaka.
Hapa tukubaliane kuna vita kati ya Manara, Yanga na TFF ambayo pengine wadau wa mpira hawajui source yake. Kufikia hatua kanuni zinawekwa pembeni kupisha "busara" tumeweka msingi mbaya ambao inakuja siku yataibuka mengi. Busara si mbadala wa Kanuni ila kuwepo kwa dalili za compromise ili yaishe.
Kama mnawaonea Yanga na Manara futeni hizo adhabu na muombe radhi maana tayari mna kila dalili za kuwa compromised kinyume na taratibu za uendeshaji wa taasisi yoyote yenye kanuni zilizo wazi. Inawezekana mnapata pressure nyingi za nje na zimewazidi uwezo.
Rais Karia simamia mpira achana na siasa za Kariakoo zitakuponza na jifunze kwa mzee Tenga alivyoendesha mpira wetu bila sarakasi za kiwango hiki. Hizi sarakasi za Yanga na TFF zinaacha alama mbaya ambayo haitakuja kufutwa kwa busara bali kurudi kwenye kanuni zinazoongoza mpira.
Tunafatilia .....
Ni dhahiri TFF kuna shida kubwa na inaelekea kupelekeshwa na siasa za Kariakoo. Kuna mtiririko wa matukio ambao unaacha doa kubwa ambalo ipo siku hizi nyufa tutajenga ukuta. Haya ni machache yanayofikirisha sana;
1) Mkataba wa GSM na TFF uliopigiwa kelele na jinsi ulivyofutika imebaki gizani ila maswali mengi yamesalia.
2) Sakata la Manara na adhabu yake, Yanga na Manara kuvunja maelekezo ya TFF siku ya wananchi. Tuliambiwa Hersi na Manara watahojiwa na hatua kuchukuliwa lakini hakuna kilichotokea.
3) Manara kufanya tukio hilo no.2 na kuendelea kuishutumu wazi TFF na Rais wake baada ya kifungo kupitia page yake rasmi lakini tumesikia rufaa yake imetupwa ila kwa busara adhabu imepunguzwa, sasa hapo kwenye busara si dalili ya Manara hakustahili adhabu iliyotolewa mwanzo?
4) Sakata la Kisinda ambalo TFF walisema Yanga wamezidisha idadi lakini mwezi mmoja toka ligi ianze wanampitisha mchezaji huyo huyo kwa "busara". Mbaya zaidi dirisha lilishafungwa! Mnajua kitachokuja mbele?
5) Barua za mawasiliano ya kiofisi kuvujishwa kwa wachambuzi na kusomwa hadharani. Hii ni dalili kuna "viongozi" walikuwa pia " vitani" hadi wakavuka mipaka.
Hapa tukubaliane kuna vita kati ya Manara, Yanga na TFF ambayo pengine wadau wa mpira hawajui source yake. Kufikia hatua kanuni zinawekwa pembeni kupisha "busara" tumeweka msingi mbaya ambao inakuja siku yataibuka mengi. Busara si mbadala wa Kanuni ila kuwepo kwa dalili za compromise ili yaishe.
Kama mnawaonea Yanga na Manara futeni hizo adhabu na muombe radhi maana tayari mna kila dalili za kuwa compromised kinyume na taratibu za uendeshaji wa taasisi yoyote yenye kanuni zilizo wazi. Inawezekana mnapata pressure nyingi za nje na zimewazidi uwezo.
Rais Karia simamia mpira achana na siasa za Kariakoo zitakuponza na jifunze kwa mzee Tenga alivyoendesha mpira wetu bila sarakasi za kiwango hiki. Hizi sarakasi za Yanga na TFF zinaacha alama mbaya ambayo haitakuja kufutwa kwa busara bali kurudi kwenye kanuni zinazoongoza mpira.
Tunafatilia .....