DullyJr
JF-Expert Member
- Apr 10, 2011
- 13,979
- 11,816
Habari za uhakika kutoka TPLB naambiwa mechi ya Tabora United na Yanga inachezwa Dodoma na ile ya Tabora United na Simba ndiyo itachezwa Tabora.
Hii dhana ya upendeleo kwa Yanga itaendelea kuwatafuna TPLB/TFF aidha kwa makusudi au kwa bahati mbaya.
Msimu uliopita yalikuwa haya haya ambapo Yanga hawakucheza Nyankumbu mechi yao na Geita ikachezwa KIRUMBA, Simba wakacheza mechi yao Nyankumbu.
Mechi ya Manungu kati ya Mtibwa na Yanga ilichezwa katikati ya dhana ya kwamba Yanga hawatocheza Manungu baada ya kiwanja kuonekana kibovuuuu lakini walicheza hali iliyofuta hiyo dhana, mechi hii ya Tabora pia kwamba Yanga hawatoenda Tabora na yametimia, kuweni makini watu wa mpira hatunaga siri.
Msimu huu yamejirudia yaleyale ya msimu uliopita, Yanga mechi na Tabora inachezwa Dodoma ila Tabora na Simba itachezwa Tabora, sababu ni zile zile kiwanja kinafungiwa halafu kinafunguliwa siku chache kabla ya mechi ya Yanga halafu wanasema kanuni inakataa kutumia hicho kiwanja kwahiyo Yanga wanakuwa kwenye faida.
Naambiwa kiwanja kimefunguliwa leo kwahiyo kanuni inataka baada ya siku 7 ndipo kianze kutumika, Yanga mechi yao ipo tarehe 23/12 siku 2 tu mbele, wakati ile ya Tabora na Simba ipo tarehe 29/12 siku 8 mbele ambapo ni ndani ya muda wa kikanuni.
Kumekuwa na dhana ya Yanga kupata “feva” kutoka kwa TFF/TPLB, wanaoharibu zaidi ni wapambe wanaojisifu kwamba Viongozi Wakuu Yanga na TFF wana nasaba kwahiyo wanafanya wanayotaka. Msiache dhana hii ikamea itapanda mbegu mbaya.
Siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.
Credit to: Bin Kazumari Mtipa (The voice of the voiceless)
Hii dhana ya upendeleo kwa Yanga itaendelea kuwatafuna TPLB/TFF aidha kwa makusudi au kwa bahati mbaya.
Msimu uliopita yalikuwa haya haya ambapo Yanga hawakucheza Nyankumbu mechi yao na Geita ikachezwa KIRUMBA, Simba wakacheza mechi yao Nyankumbu.
Mechi ya Manungu kati ya Mtibwa na Yanga ilichezwa katikati ya dhana ya kwamba Yanga hawatocheza Manungu baada ya kiwanja kuonekana kibovuuuu lakini walicheza hali iliyofuta hiyo dhana, mechi hii ya Tabora pia kwamba Yanga hawatoenda Tabora na yametimia, kuweni makini watu wa mpira hatunaga siri.
Msimu huu yamejirudia yaleyale ya msimu uliopita, Yanga mechi na Tabora inachezwa Dodoma ila Tabora na Simba itachezwa Tabora, sababu ni zile zile kiwanja kinafungiwa halafu kinafunguliwa siku chache kabla ya mechi ya Yanga halafu wanasema kanuni inakataa kutumia hicho kiwanja kwahiyo Yanga wanakuwa kwenye faida.
Naambiwa kiwanja kimefunguliwa leo kwahiyo kanuni inataka baada ya siku 7 ndipo kianze kutumika, Yanga mechi yao ipo tarehe 23/12 siku 2 tu mbele, wakati ile ya Tabora na Simba ipo tarehe 29/12 siku 8 mbele ambapo ni ndani ya muda wa kikanuni.
Kumekuwa na dhana ya Yanga kupata “feva” kutoka kwa TFF/TPLB, wanaoharibu zaidi ni wapambe wanaojisifu kwamba Viongozi Wakuu Yanga na TFF wana nasaba kwahiyo wanafanya wanayotaka. Msiache dhana hii ikamea itapanda mbegu mbaya.
Siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.
Credit to: Bin Kazumari Mtipa (The voice of the voiceless)