TFF, Benchi la Ufundi la Taifa Stars huko CHAN 2021 nimeshamaliza Kazi kwa Kikosi hiki Namibia leo na Guinea Wiki ijayo wanakufa!

ANGALIZO

Tafadhali kisibadilishwe na pia Kicheze kama ambavyo nimekipanga kwani Kiunyangindo kimeonyesha Mafanikio na tutashinda mechi zilizobakia.

Kikosi cha Kuanza kiwe hiki tu....

1. Aishi Manula
2. Shomary Kapombe
3. Yassin Mustafa
4. Ibrahim Ame ( kama bado hajapona aanze Dickson Job )
5. Bakari Mwamnyeto
6. Erasto Nyoni ( kama bado hajapata ruhusa ya Vipimo vya CORONA aanze Feisal Salum )
7. Deus Kaseke
8. Said Ndemla
9. Ditram Nchimbi
10. John Boko ( kama bado hajawa vizuri Kiafya aanze Adam Adam )
11. Farid Mussa ( na huyu asibadilishwe hadi dakika zote 90 kwani ndiyo atakuwa mwiba kwa Wapinzani au Kutufungia pia )

Wachezaji wa Akiba wawe hawa tu....

1. Juma Kaseja
2. Edward Manyama
3. Dickson Job
4. Feisal Salum
5. Adam Adam
6. Lucas Kikoti
7. Ayoub Lyanga

Sihitaji malipo yoyote kwa Unyangindo ( Ushirikina ) nilioufanya hapa Nyumbani Pemba ninapoishi kwani nimejitolea Kuipigania Tanzania yangu. Naomba kwa aliye karibu na Rais wa TFF Karia au Katibu Mkuu Kidao au Msemaji Ndimbo au Benchi la Ufundi la Taifa Stars wawafikishie upesi mno huu Uzi wangu na hasa hasa hiki Kikosi kwani nina uhakika nacho na Kikipangwa kama nilivyokipanga hapa Watanzania wote kuanzia leo tutafurahi na kusahau Machungu yote kwani Namibia leo na Guinea wiki ijayo watakufa ( watafungwa ) mapema tu.

Nahodha wa leo ahakikishe sana tunaanzia Goli la Kusini ili mwisho tuje kumalizia la Kaskazini na ule Mzigo ( Hirizi ) leo avalishwe Farid / Deus tu.
Umetisha mkuu hasa hapo kwa Faridi Mussa
 
Huyu kocha wa namibia naoa alibet hii mechi...sasa ndio substitution gani ile? Unamtoa mtu ambaye ndio anapeleka mashabulizi kwa wapinzani!!
 
Katika nafasi ya Ibrahim Ame acheze Dickson Job, ya Erasto Nyoni acheze Feisal Salum na ya John Boko acheze Adam Adam. Tutashinda msihofie.
Kuhusu Farid ni kama ulivyosema, uchawi kweli noma. Kwa hiyo hilo goli ndo basi tena!?
 
We jamaa nomaa, hebu tutabirie na game ya tarehe 27 je tutamuweza Guinea?
Tatizo lenu Members wa JF mna dharau halafu ni Wanafiki mno ila wengine tumezaliwa tayari tunajiamini na tuna uhakika na kile tunachokifanya.
 
Tatizo lenu Members wa JF mna dharau halafu ni Wanafiki mno ila wengine tumezaliwa tayari tunajiamini na tuna uhakika na kile tunachokifanya.
Shida ni kwamba humu JF kila mtu anajifanya mjuaji hata kama hana alijualo. MKUU,ILA MIMI NILISHAKUELEWA SANA KWENYE ENEO LA SOKA..

Utasikia mwanaJF anasema "ushirikina na soka wapi na wapi"?, mara Oooh " usilete imani za kijinga hapa!" au "kama uchawi una msaada kwenye soka si Tanzania ingeshabeba World Cup, na timu za Sumbawanga zingekuwa zinatesa Ligi ya Mabingwa Afrika?" Basi mi nabaki nawaangalia tu.

Cha ajabu,jitu hilo hilo unakuta linatoka familia ya washirikina, mwanasiasa au mwanasoka mahiri linayemkubali ndo mshirikina no.1, bado yule Askofu,Mchungaji,Padre na Shehe wake. Mi huwa nayaangalia tu.
 
Shida ni kwamba humu JF kila mtu anajifanya mjuaji hata kama hana alijualo. MKUU,ILA MIMI NILISHAKUELEWA SANA KWENYE ENEO LA SOKA..

Utasikia mwanaJF anasema "ushirikina na soka wapi na wapi"?, mara Oooh " usilete imani za kijinga hapa!" au "kama uchawi una msaada kwenye soka si Tanzania ingeshabeba World Cup, na timu za Sumbawanga zingekuwa zinatesa Ligi ya Mabingwa Afrika?" Basi mi nabaki nawaangalia tu.

Cha ajabu,jitu hilo hilo unakuta linatoka familia ya washirikina, mwanasiasa au mwanasoka mahiri linayemkubali ndo mshirikina no.1, bado yule Askofu,Mchungaji,Padre na Shehe wake. Mi huwa nayaangalia tu.
Halafu kuna Watu utawasikia wanasema kuwa Brazil hakuna Uchawi wakati hakuna Watu wanaojua Kuroga japo wana Vipaji vya Soka kama Brazil.
 
Back
Top Bottom