Tetemeko la ardhi limepita hapa Arusha

Tetemeko la ardhi limepita hapa Arusha

true

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2011
Posts
506
Reaction score
281
Tetemeko limepita muda huu hapa Arusha. Yaani niko naangalia taarifa ya habari, nilipokaa panatetemeka mpaka nikatoka nje mbio.. sijajua litakuwa na kipimo gani!! Ila ni likubwa.
 
Hapa Dodoma limepita tetemeko dogo la ardhi muda huu na kusababisha watu kukimbilia nje ya nyumba zao kwa hofu.

Hapa napokaa tumetikiswa kidogo na hamna athari kwani ni tetemeko dogo tu.
 
kuna tetemeko limepitikisa takribani sekunde 46 hivi hapa dodoma mjini milango ya saa mbili na dk 3 usiku huu likitokea kusini kuelekea kaskazini limekuja taratibu likazidi sana kama sekund 10 nusura nianze kutoka kwenye nyumba harafu likaendelea taratibu mpaka likaishia
 
Limekuwa na uwezo wa kudondosha bia zilizokuwa mezani mkuu!!
 
Ukitaka kujuwa kipimo likidondosha glasi ya bia mezani basi juwa ni la kawaida
 
Muwe na subra Allah ni mkubwa tuzidi kuomba msamaha kutokana na makosa mbali mbali tunayofanya ili tupate nusra yake hapa na kesho akhera.
 
Ukitaka kujuwa kipimo likidondosha glasi ya bia mezani basi juwa ni la kawaida

Kwa wale wenye marufuku na kipimo hicho wafanye nini? je glass ya maji inafaa kwa mbadala?
 
Tetemeko limepita muda huu hapa Arusha. Yaani niko naangalia taarifa ya habari, nilipokaa panatetemeka mpaka nikatoka nje mbio.. sijajua litakuwa na kipimo gani!! Ila ni likubwa.

blaza hiyo kitu imetokea lushoto kama dk 15 zilizo pita nilikua nime kaa kwenye kochi nashangaa mtetemo nyumba nzima ila ni kwa kiwango kidogo mnooo!
 
Duh! mi nimeshangaa kitanda kimeanza kutetemeka...kumbe ni tetemeko!
 
Tetemeko limepita muda huu hapa Arusha. Yaani niko naangalia taarifa ya habari, nilipokaa panatetemeka mpaka nikatoka nje mbio.. sijajua litakuwa na kipimo gani!! Ila ni likubwa.

Lipe salamu zangu kama litarudi.
 
Hata huku kwetu kijiji cha fufu limepita likadondosha tv yangu ya flat sony bravia orijino kabisa.
 
Tetemeko limepita muda huu hapa Arusha. Yaani niko naangalia taarifa ya habari, nilipokaa panatetemeka mpaka nikatoka nje mbio.. sijajua litakuwa na kipimo gani!! Ila ni likubwa.

Mwisho wa dunia umefika.. Tubu!
 
Back
Top Bottom