TUJITEGEMEE
Platinum Member
- Nov 6, 2010
- 27,302
- 28,016
Huyu mzee mwoneeni huruma tu!
Kwa hali ya kawaida linakuwa jambo la kushangaza sana anayeitwa msajili wa vyama vya siasa kutoa maoni kama yale kwa chama cha siasa kwa nafasi aliyonayo.
Huyu mzee mwoneeni huruma tu!
Leo katika kipindi cha dakika 45 kinachorushwa na ITV, mzee John Tendwa ambaye ni msajili (mlezi) wa vyama vya siasa nchini amekosoa harakati mbalimbali za kisiasa zinazoendeshwa na CHADEMA nchini na kusema kuwa hazina tija zaidi zinachochea vurugu.
Kuhusu 'Operation sangara' ameikosoa akisema CHADEMA wameharakisha kufanya hivyo kwamba watachoka kabla ya uchaguzi hivyo kuifanya kutokuwa na manufaa yoyote. Kuhusu M4C, bila kufafanua vizuri, amesema haina tija yoyote kwani haijaandaliwa vizuri kwa vile CHADEMA wamekurupuka!
Binafsi namshauri mzee Tendwa afanye kazi yake ya usajiri na ulezi wa vyama vya siasa. Wananchi tumeona jinsi M4C na operation sangara zinavyowaamsha watanzania kujua na hatimaye kudai haki zao juu ya matumizi sahihi ya rasilimali za taifa.
Amewekwa pale ili afanye anayoyafanya sasa. Ni kada wa CCM huyo!!!Kwa hali ya kawaida linakuwa jambo la kushangaza sana anayeitwa msajili wa vyama vya siasa kutoa maoni kama yale kwa chama cha siasa kwa nafasi aliyonayo.
Refarii anachezesha gemu wakati huohuo anaumizwa na kandanda safi linalochezwa na timu moja dhidi ya nyingine.
Leo katika kipindi cha dakika 45 kinachorushwa na ITV, mzee John Tendwa ambaye ni msajili (mlezi) wa vyama vya siasa nchini amekosoa harakati mbalimbali za kisiasa zinazoendeshwa na CHADEMA nchini na kusema kuwa hazina tija zaidi zinachochea vurugu.
....
1 said:Wanasiasa waache kuchochea Udini-Tendwa
"Msajili wa vyama vya siasa John Tendwa ameitaka serikali kukomesha uchochezi wa kidini ambao anaamini unachochewa na baadhi ya vyama vya siasa.
Akizungumza katika mkutano wa Baraza la vyama vya siasa Tendwa amesema uchochezi wa kidini ni hatari na kuonya vyama vyenye tabia hiyo kuacha mara moja.
Tendwa amekuwa mara kadhaa akitoa lugha ambazo hajazifanyia utafiti na kuonekana kama kituko mbele ya jamii."